Makamba: maiti ya kijana iliyokutwa ikining’inia juu ya mti
Mwili wa Cédric Nkeshimana uligunduliwa Jumanne hii. Alitundikwa kwenye mti katika mji mkuu wa jimbo la Makamba (kusini mwa Burundi). Mazingira ya kifo chake bado hayajulikani.Polisi wamewakamata washukiwa wawili kama sehemu ya uchunguzi.
HABARI SOS Media Burundi
Asubuhi na mapema wapita njia waligundua maiti hiyo katika wilaya ya Makamba 2, kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari.
“Wapita njia waliona mwili ukining’inia kutoka kwa mti kwa kutumia kamba wakati wa alfajiri,” vyanzo vya ndani vinasema.
Uongozi na polisi walienda eneo la tukio kuangalia ukweli.
Wakazi wanaonyesha kuwa “tulimtambua marehemu mara moja. Ni Cédric Nkeshimana, kijana aliyehitimu katika shule ya uuguzi. Alifanya kazi katika duka la dawa katika mji mkuu wa mkoa.”
Mazingira ya kifo chake bado hayajajulikana. Walioshuhudia wanasema kuwa marehemu hakuwa na majeraha yoyote na kwamba hakuwa amevaa viatu vyake. Wanaamini huenda kijana huyo aliuawa kabla ya wahalifu hao kughushi kujitoa mhanga, kwa sababu wanasema waliona alama mpya za gari chini ya mti aliokuwa akining’inia.
Lakini vyanzo kutoka katika wilaya ya mpakani ya Mabanda (jimbo hilohilo la Makamba) anakotoka vinathibitisha kuwa Cédric Nkeshimana tayari alishajaribu kujiua siku za nyuma.
Polisi wanasema wamewakamata washukiwa wawili kama sehemu ya uchunguzi wao.
Mwili wa marehemu ukipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa.
Kumbuka kuwa vyanzo hivyohivyo vya Mabanda vinathibitisha kuwa mmoja wa ndugu zake naye alikutwa amefariki hivi karibuni katika mazingira ambayo bado hayajawekwa wazi.
——-
Mahali ambapo mwili wa Cédric Nkeshimana uligunduliwa, Agosti 20, 2024 (SOS Médias Burundi)
You might also like
Burundi–DRC: Gitega yalazimishwa kuomba kurudishwa kwa wanajeshi wake na kivuko cha kibinadamu
SOS Médias Burundi Bukavu, Desemba 11, 2025 – “Askari wa Burundi waliokamatwa watakabidhiwa kwa mamlaka ya nchi yao kwa kufuata kikamilifu haki za binadamu,” alisema Lawrence Kanyuka, msemaji wa AFC/M23,
Buhumuza: Kipindupindu na msongamano wa watu unatishia kambi ya Wakimbizi ya Busuma
SOS Médias Burundi Ruyigi, Desemba 19, 2025 – Kambi ya wakimbizi ya Busuma, iliyoko kwenye kilima cha jina moja katika wilaya ya Ruyigi, mkoa wa Buhumuza (mashariki mwa Burundi), inakabiliwa
Rwanda: Kadi ya biometriska inayoweza kubadilisha maisha ya wakimbizi
SOS Médias Burundi Mahama, Rwanda, Juni 16, 2026 – Rwanda inaendelea na mabadiliko yake ya kidijitali kwa kusambaza taratibu za kitambulisho kipya cha kibayometriki kwa raia na wakazi wake wote.
