Makamba: maiti ya kijana iliyokutwa ikining’inia juu ya mti

Makamba: maiti ya kijana iliyokutwa ikining’inia juu ya mti

Mwili wa Cédric Nkeshimana uligunduliwa Jumanne hii. Alitundikwa kwenye mti katika mji mkuu wa jimbo la Makamba (kusini mwa Burundi). Mazingira ya kifo chake bado hayajulikani.Polisi wamewakamata washukiwa wawili kama sehemu ya uchunguzi.

HABARI SOS Media Burundi

Asubuhi na mapema wapita njia waligundua maiti hiyo katika wilaya ya Makamba 2, kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari.

“Wapita njia waliona mwili ukining’inia kutoka kwa mti kwa kutumia kamba wakati wa alfajiri,” vyanzo vya ndani vinasema.

Uongozi na polisi walienda eneo la tukio kuangalia ukweli.

Wakazi wanaonyesha kuwa “tulimtambua marehemu mara moja. Ni Cédric Nkeshimana, kijana aliyehitimu katika shule ya uuguzi. Alifanya kazi katika duka la dawa katika mji mkuu wa mkoa.”

Mazingira ya kifo chake bado hayajajulikana. Walioshuhudia wanasema kuwa marehemu hakuwa na majeraha yoyote na kwamba hakuwa amevaa viatu vyake. Wanaamini huenda kijana huyo aliuawa kabla ya wahalifu hao kughushi kujitoa mhanga, kwa sababu wanasema waliona alama mpya za gari chini ya mti aliokuwa akining’inia.

Lakini vyanzo kutoka katika wilaya ya mpakani ya Mabanda (jimbo hilohilo la Makamba) anakotoka vinathibitisha kuwa Cédric Nkeshimana tayari alishajaribu kujiua siku za nyuma.

Polisi wanasema wamewakamata washukiwa wawili kama sehemu ya uchunguzi wao.

Mwili wa marehemu ukipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa.

Kumbuka kuwa vyanzo hivyohivyo vya Mabanda vinathibitisha kuwa mmoja wa ndugu zake naye alikutwa amefariki hivi karibuni katika mazingira ambayo bado hayajawekwa wazi.

——-

Mahali ambapo mwili wa Cédric Nkeshimana uligunduliwa, Agosti 20, 2024 (SOS Médias Burundi)

Previous Mugina: anayedaiwa kuwa mwizi aliyeuawa na Imbonerakure
Next Makamba: tishio la magonjwa kutoka kwa mikono michafu soko kuu

You might also like

Criminalité

Gitega: Mfungwa aliyepigwa risasi na afisa wa polisi, familia yadai haki itendeke

SOS Médias Burundi Gitega, Aprili 14, 2025 – Mfungwa aliuawa kwa kupigwa risasi Jumapili, Aprili 13, katika wilaya ya Nyabiharage, katikati mwa jiji la Gitega (mji mkuu wa kisiasa) na

Criminalité

Burundi: Familia yakumbwa na maafa kufuatia shambulio la guruneti huko Karusi; wawili wafariki, watatu wajeruhiwa vibaya

SOS Médias Burundi Karusi, Agosti 4, 2026 – Familia moja imekumbwa na maafa kufuatia shambulio la guruneti lililofanyika jioni ya Jumatatu, Agosti 3, katika kilima cha Nyagoba, Kaunti ya Karusi,

Criminalité

Cibitoke: Zaidi ya waasi 100 wa FLN wa Rwanda wauawa na jeshi la Burundi huko Kibira

SOS Media Burundi Mabayi, Mei 8, 2025 – Zaidi ya waasi 100 wa Rwanda kutoka FLN (National Liberation Front) waliuawa wakati wa mapigano makali na jeshi la Burundi katika msitu