Rumonge: karibu wafanyakazi 130 wa afya wanadai malimbikizo ya mishahara ya miezi 3 hadi 10

Rumonge: karibu wafanyakazi 130 wa afya wanadai malimbikizo ya mishahara ya miezi 3 hadi 10

Wafanyakazi walio chini ya kandarasi katika vituo viwili vya awali vya afya vya ukanda wa Bitare Minago na Birimba katika eneo la Rumonge, katika wilaya ya Rumonge na jimbo (kusini-magharibi mwa Burundi) wamekaa miezi 6 bila mshahara.

Duru za kimatibabu katika hospitali ya Amahoro zinasema kuwa tatizo la malimbikizo ya mishahara pia linawakumba wafanyakazi wa kandarasi wa hospitali ya Amahoro iliyoko Birimba katika mji wa Rumonge. Wote wanadai kuratibiwa

HABARI SOS Media Burundi

Watumishi hawa wamekerwa na kitendo cha kutopokea mishahara yao ilhali wanaendelea kuleta mapato katika miundo hii ya huduma za afya.

Badhi yao wanasema hawawezi tena kukabiliana na kupanda kwa bei za mahitaji ya kimsingi, bila njia yoyote ya kujikimu.

Wanadai kwamba swali linalohusiana na mshahara wao litatuliwe haraka iwezekanavyo.

Wanaamini kuwa haki yao ya kulipwa inakiukwa na kanisa la Anglikana la Rumonge, mwajiri mkuu na meneja wa hospitali na vituo hivyo vya afya.

Vyanzo vya matibabu huko Rumonge vinaripoti kuwa hospitali zilizo chini ya makubaliano zinakabiliwa na ugumu wa kuwa na fedha kwa ajili ya uendeshaji wao.

Hospitali hizi zinadai bili milioni kadhaa ambazo hazijalipwa kutoka kwa Wizara ya Afya kufuatia kutorejeshwa kwa gharama za huduma zinazotolewa kwa watumiaji wa kadi za bima ya afya, watoto chini ya miaka 5 na wajawazito.

Vyanzo hivyo hivyo vinaeleza kuwa kucheleweshwa kwa malipo ya fedha hizo kuna madhara makubwa kwa hospitali za kibinafsi na za mikataba ambazo hushirikiana na Wizara ya Afya kutekeleza sera hizi mbili za serikali.

Ni hali hii ambayo, kwa mujibu wa vyanzo hivi, inaeleza kwa nini hospitali fulani zinashindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.

Ikumbukwe kuwa, kwa upande mwingine, watumishi walio chini ya hadhi ya Utumishi wa Umma wanaofanya kazi katika hospitali hizi na vituo vya afya chini ya makubaliano ya Anglikana wanaendelea kupokea mishahara yao bila tatizo lolote. Mishahara yao inalipwa na serikali.

————

Hospitali ya Amahoro katika mji mkuu wa Rumonge, mojawapo ya miundo ya afya ambayo haiwezi tena kulipa mishahara kwa wafanyakazi wake (SOS Médias Burundi)

Previous Makamba: Warundi wapigwa marufuku kupata mafuta nchini Tanzania
Next DRC: uasi mpya wa ndani ungeungana na M23

You might also like

Jamii

Burundi : ni lazima iwepo sera ya misharaha inayovutia ili kuwazuia waganga kwenda nje ya nchi (Chama cha wafanyakazi)

Mishahara midogo pamoja na ukosefu vifaa vya kutosha ndio sababu kuu ya waganga wa Burundi kutoroka na kwenda kuhudumu katika nchi zingine. Ni tamko la kiongozi wa chama cha kutetea

Jamii

Burundi: Spika wa Bunge la Kitaifa anapiga marufuku manaibu kukemea mzozo uliopo na anakusudia kurejesha hukumu ya kifo kwa wale wanaovuruga uchumi

Baraza la bunge la Burundi mnamo Alhamisi lilichambua na kupitisha mswada wa kuunda bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa kifedha wa 2024-2025. Baadhi ya manaibu wamekashifu tangu Jumatano wakati

Jamii

Bubanza: Mahindi ya kukaanga, chanzo cha mapato kidogo kwenye barabara za umma

Katika kituo cha kibiashara cha Bubanza, magharibi mwa Burundi, mazingira ya soko kuu na stendi za viburudisho yanajaa akina mama wanaochoma mahindi ili kuwauzia wapita njia. Sikio la mahindi ya