Bujumbura: mwandishi Sandra Muhoza ahukumiwa kifungo cha miezi 21 kwa makosa mawili
Mwenzetu alihukumiwa na mahakama ya Mukaza katikati mwa jiji la kibiashara la Bujumbura. Uamuzi huo ulianguka Jumatatu hii, Desemba 16. Shirika la Waandishi waHabari wasio kua na mpika (RSF), ambalo linashutumu “uamuzi usio wa haki wa kisiasa”, lilitoa wito kwa mfumo wa haki wa Burundi kubadili uamuzi wake.
HABARI SOS Médias Burundi
Shirika la Wanahabari wasio kuwa na mipaka, ambalo limeendelea kushutumu kukamatwa na kuwekwa kizuizini kwa Sandra Muhoza, lilitangaza Jumatatu kuwa alihukumiwa kifungo cha miezi 18 kwa “kudhoofisha uadilifu wa eneo la kitaifa” na miezi mitatu kwa “chuki ya rangi”.
Kwa mujibu wa Shirika linalotetea haki za waandishi wa habari lenye makao yake makuu mjini Paris nchini Ufaransa, kwa kulaani mwenzetu, mamlaka ya Burundi “inaendelea kwa ukaidi mfululizo wa vitendo vya ukandamizaji kipofu wa uhuru wa vyombo vya habari”.
Akinukuliwa na RSF, Prosper Niyoyankana, mmoja wa mawakili wa Sandra Muhoza, alizingatia hukumu hii “kuwa ya ushabiki na iliyochochewa na nia ya wazi ya kumnyamazisha mtu yeyote nje ya hatua ya serikali.”
Wakili mwingine aliiambia SOS Médias Burundi Jumatatu jioni kwamba “Tutakata rufaa dhidi ya uamuzi huu na kutaka mteja wetu aachiliwe bila masharti kwa sababu tayari ametumikia robo ya hukumu hii.”
“Kuhukumiwa kwa Sandra Muhoza bila ya haki ni hatua ya hivi punde ya ukandamizaji wa mamlaka dhidi ya waandishi wa habari. Uamuzi ambao unakuja wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi wa wabunge na manispaa. Wakati mwandishi huyo anashitakiwa kwa sababu ya “taarifa zinazokihusisha chama tawala. , kuna mashaka machache juu ya kuwekwa kisiasa kwa hukumu hii,” alisema Sadibou Marong, mkuu wa dawati la RSF Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“RSF inashutumu vikali uamuzi uliochochewa na masuala ya kisiasa na kutoa wito kwa mamlaka ya mahakama kumwachilia mara moja mwandishi wa habari Sandra Muhoza,” alijibu.
https://www.sosmediasburundi.org/2024/11/12/bujumbura-le-parquet-a-requis-12-ans-de-prison-contre-la-journaliste-sandra-muhoza/
Hakukuwa na majibu ya moja kwa moja kutoka kwa mamlaka za kisheria katika taifa hilo dogo la Afrika Mashariki. RSF ilielezea shutuma zilizotolewa dhidi ya mwenzetu kama “uongo”.
You might also like
Cibitoke: utekaji nyara wa wanachama 4 wa chama cha siasa
Mkuu wa chama cha CDP (Conseil des Patriotes) katika mkoa mpya wa Bujumbura na wanachama wengine watatu wa chama hiki hawajapatikana tangu Jumapili Septemba 15. Chama kinashutumu Imbonerakure (wanachama wa
Picha ya wiki: wafanyakazi hawawezi kukidhi mahitaji yao ya kimsingi kulingana na mashirikisho mawili ya vyama vya ndani
CSB (Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi wa Burundi) na COSYBU (Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi vya Burundi) wanasikitishwa na hali ya sasa ya kiuchumi na mapato ya kutosha miongoni
Siku ya Kimataifa ya Wakimbizi: kati ya matumaini na kujiuzulu miongoni mwa wakimbizi wa Burundi
Tarehe 20 Juni kila mwaka, dunia huadhimisha Siku ya Wakimbizi. Fursa ya kuwafikiria na kutetea, kulinda na kuendeleza haki zao, kulingana na UNHCR. Kwa zaidi ya Warundi 300,000 ambao bado
