Bujumbura: mwandishi Sandra Muhoza ahukumiwa kifungo cha miezi 21 kwa makosa mawili
Mwenzetu alihukumiwa na mahakama ya Mukaza katikati mwa jiji la kibiashara la Bujumbura. Uamuzi huo ulianguka Jumatatu hii, Desemba 16. Shirika la Waandishi waHabari wasio kua na mpika (RSF), ambalo linashutumu “uamuzi usio wa haki wa kisiasa”, lilitoa wito kwa mfumo wa haki wa Burundi kubadili uamuzi wake.
HABARI SOS Médias Burundi
Shirika la Wanahabari wasio kuwa na mipaka, ambalo limeendelea kushutumu kukamatwa na kuwekwa kizuizini kwa Sandra Muhoza, lilitangaza Jumatatu kuwa alihukumiwa kifungo cha miezi 18 kwa “kudhoofisha uadilifu wa eneo la kitaifa” na miezi mitatu kwa “chuki ya rangi”.
Kwa mujibu wa Shirika linalotetea haki za waandishi wa habari lenye makao yake makuu mjini Paris nchini Ufaransa, kwa kulaani mwenzetu, mamlaka ya Burundi “inaendelea kwa ukaidi mfululizo wa vitendo vya ukandamizaji kipofu wa uhuru wa vyombo vya habari”.
Akinukuliwa na RSF, Prosper Niyoyankana, mmoja wa mawakili wa Sandra Muhoza, alizingatia hukumu hii “kuwa ya ushabiki na iliyochochewa na nia ya wazi ya kumnyamazisha mtu yeyote nje ya hatua ya serikali.”
Wakili mwingine aliiambia SOS Médias Burundi Jumatatu jioni kwamba “Tutakata rufaa dhidi ya uamuzi huu na kutaka mteja wetu aachiliwe bila masharti kwa sababu tayari ametumikia robo ya hukumu hii.”
“Kuhukumiwa kwa Sandra Muhoza bila ya haki ni hatua ya hivi punde ya ukandamizaji wa mamlaka dhidi ya waandishi wa habari. Uamuzi ambao unakuja wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi wa wabunge na manispaa. Wakati mwandishi huyo anashitakiwa kwa sababu ya “taarifa zinazokihusisha chama tawala. , kuna mashaka machache juu ya kuwekwa kisiasa kwa hukumu hii,” alisema Sadibou Marong, mkuu wa dawati la RSF Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“RSF inashutumu vikali uamuzi uliochochewa na masuala ya kisiasa na kutoa wito kwa mamlaka ya mahakama kumwachilia mara moja mwandishi wa habari Sandra Muhoza,” alijibu.
https://www.sosmediasburundi.org/2024/11/12/bujumbura-le-parquet-a-requis-12-ans-de-prison-contre-la-journaliste-sandra-muhoza/
Hakukuwa na majibu ya moja kwa moja kutoka kwa mamlaka za kisheria katika taifa hilo dogo la Afrika Mashariki. RSF ilielezea shutuma zilizotolewa dhidi ya mwenzetu kama “uongo”.
You might also like
Bujumbura: watendaji watatu wa rais wahamishiwa katika gereza la Mpimba
Jean Baptiste Baribonekeza, mkuu wa zamani wa Tume Huru ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu, CNIDH, Cyrille Sibomana na Arcade Harerimana, waliwasili katika gereza la Bujumbura linalojulikana kwa jina la
Burundi: Vitisho kwa wanahabari, wanahabari wawili waachiliwa baada ya usiku mbili vizuizini
SOS Médias Burundi Bujumbura, Februari 20, 2026 – Mwanasheria Mkuu katika Mahakama ya Rufaa ya Ntahangwa, kaskazini mwa mji mkuu wa kiuchumi Bujumbura, Eraste Ndayiragije, aliamuru kuachiliwa kwa muda Ijumaa
Kirundo: mtoto mwenye asili ya Kitanzania kizuizini kwa sababu tu ya kuvuka mpaka kwa kutojua
Kirundo: mtoto mwenye asili ya Kitanzania kizuizini kwa sababu tu ya kuvuka mpaka kwa kutojua. Mtoto mwenye asili ya Tanzania mwenye umri wa miaka minane hadi tisa amezuiliwa katika seli
