Bubanza: Mkurugenzi wa magereza asimamishwa kazi kwa utovu wa usimamizi
SOS Médias Burundi
Bubanza, Machi 26, 2026 — Gereza la Bubanza, lililoko katika tarafa ya Bubanza, mkoa wa Bujumbura magharibi mwa Burundi, liko katikati ya kashfa ya usimamizi mbovu. Mkurugenzi wake, Samuel Kayanda, amesimamishwa kazi kiutawala akisubiri hatua za kisheria au za kinidhamu.
Kwa mujibu wa ushahidi thabiti kutoka kwa wafungwa, mkurugenzi w towa gereza anatuhumiwa kuanzisha mpango wa rushwa ndani ya gereza hilo. Wafungwa hao wanadai kuwa aliwaibia kiasi cha kati ya 100,000 hadi 300,000 za Burundi ili kubadilishana na baadhi ya marupurupu. Hizi ni pamoja na umiliki wa simu za mkononi—ambazo ni marufuku gerezani—na ahadi ya kupewa vyeo vya kuwawakilisha wafungwa wengine, pamoja na uwezekano wa kuboresha hali zao gerezani.
Mbali na vitendo hivyo vinavyokemewa, hali ya maisha ndani ya gereza hilo pia imeibua wasiwasi mkubwa. Wafungwa wanaripoti kukabiliwa na uhaba wa chakula kwa wiki moja, ambapo walikula maharagwe tu, bila mahindi au mihogo kujumuishwa katika mgao wao. Walakini, kulingana na vyanzo vingine vya ndani, vifaa viliwasilishwa mara kwa mara.
Katika kukabiliana na hali hiyo, jeshi la magereza lilifanya hafla ya makabidhiano na maofisa wapya wa magereza siku ya Jumamosi, Machi 21, 2026. Mabadiliko haya yaliambatana na mapendekezo yaliyolenga usimamizi mkali na wa uwazi wa gereza la Bubanza. Tangu mabadiliko haya, wafungwa wanaripoti kuona uboreshaji, hasa kwa kurudi kwa unga wa mahindi kwenye mlo wao wa kila siku.
Kesi ya Samuel Kayanda inaendelea kuvutia maoni ya wananchi wa eneo hilo, huku gereza la Bubanza likionyesha changamoto zinazokabili vituo vya magereza katika taifa hilo dogo la Afrika Mashariki, huku baadhi ya vituo vina hadi asilimia 700 ya idadi iliyokusudiwa ya wafungwa.
You might also like
Uswisi: Mashirika na wataalamu waibua wasiwasi kuhusu kurudi Burundi na kutoa Wito wa kufanyiwa tathmini tena ya mazoezi ya ukimbizi.
Geneva, Mei 27, 2026 — Mashirika ya kiraia, yakiungwa mkono na wataalam wa sheria na wataalam wa haki za binadamu, yalifanya mkutano na waandishi wa habari Jumatano hii kushutumu Uswizi
Goma: kijana mdogo uuwawa na askali polisi katika kituo cha kuandika wapiga kura
Dieudonné Bagenda, miaka 20 aliuwawa kwa kupigwa risasi. Risasi lilimpata kichwani akiwa katika kituo cha kuorodhesha wapiga kura cha Byahi alhamisi hii katika kata ya Bujovu ndani ya mji wa
Burundi: wanaharakati kadhaa waliojitolea wanataka kuachiliwa kwa Mwanahabari Sandra Muhoza
Takriban mashirika ishirini yenye asili ya Burundi yalitoa taarifa mnamo Ijumaa Februari 28, 2025, kutaka Mwanahabari Sandra Muhoza aachiliwe bila masharti. Akiwa kizuizini kwa takriban mwaka mzima, anashutumiwa, miongoni mwa
