Goma: kijana mdogo uuwawa na askali polisi katika kituo cha kuandika wapiga kura
Dieudonné Bagenda, miaka 20 aliuwawa kwa kupigwa risasi. Risasi lilimpata kichwani akiwa katika kituo cha kuorodhesha wapiga kura cha Byahi alhamisi hii katika kata ya Bujovu ndani ya mji wa Goma makao makuu ya mkoa wa Kivu kaskazini. Kulingana na ushahuda ulipatikana eneo hilo, chanzo cha mgogoro ni kitita cha pesa walichokubaliana kati ya muhanga na askali polisi anayelinda kituo hicho. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa ushuhuda, makubaliano ni kwamba Dieudonné Bagenda angetakiwa kumpa pesa askali polisi huyo baada ya kujiorodhesha. Baada ya kukosa kadi yake, muhanga alikataa kuheshimu makubaliano na yote yakaanzia hapo.
” Walikubaliana kuwa baada ya kupewa kadi, kijana huyo angemupa franka 5000 sarafu za Kongo askali polisi huyo. Baada ya kujichakaza, kijana alijikuta hana pesa hiyo waliokubaliana, hali ambayo haikumufurahisha polisi huyo. Aliamuru kumpiga risasi kichwani “, alieleza shahidi mmoja kwa hasira.
Mtu mwingine alifahamisha kuwa muhanga hakupata kadi yake ya mpiga kura, na alikuwa akifuatilia mchakato wote kupitia dirisha.
” Alikuwa bado hajapata kadi yake. Iwapo angemufuatilia baada ya kupata kadi yake, hapo tungeelewa lakini alikuwa alifuatilia kupitia dirisha. Kuliko kumuambia aondoke, askali polisi huyo alimufuatilia hadi ndani ya kata na kumumalizia maisha”, alitoa ushuhuda mkaazi wa Goma machozi yakitiririka.
Muili wa muhanga ulibaki kwa dakika chache katika kituo cha kuorodhesha wapiga kura wakisubiri wananchi waliokuwa na hasira watulie.
Badaye muili ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti kwa kusubiri matokeo ya uchunguzi.
Kituo hicho cha kuorodhesha wapiga kura kilivamiwa na kusambuliwa na vijana kabla ya polisi kuwasili eneo la tukio.
Hivi karibuni, askali polisi mwingine aliwasha moto ndani ya kituo cha kuandikisha wapiga kura kaskazini mwa mji wa Goma bila hata hivo kusababisha hasara.
Mashirika ya kiraia yanaomba viongozi wa usalama kuwaelekeza askali polisi wanaohudumu kwenye vituo vya kuandikisha wapiga kura.
You might also like
Geneva: Mamlaka ya Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi yafanywa upya
Kura hiyo imefanyika Alhamisi hii. Kati ya nchi 47 zinazounda Baraza, 22 zilipiga kura kuunga mkono kuteuliwa tena kwa Fortune Gaétan Zongo. Mamlaka ya Burundi bado haijaguswa na uamuzi huu.
Burundi: Mahakama ya Rufaa ya Mukaza yatangaza mamlaka yake yameisha – Sandra Muhoza aendelea kuzuiliwa licha ya kumalizika kwa hatia
SOS Médias Burundi Bujumbura, Julai 1, 2025 — SOS Media Burundi imefahamu kwamba Mahakama ya Rufaa ya Mukaza, iliyoko katika jiji la kibiashara la Bujumbura, ilitoa uamuzi wake Juni 13,
Wito wa kutisha: Kesi ya Kenny Claude Nduwimana inaelekea wapi?
SOS Médias Burundi Bujumbura, Desemba 4, 2025 – Alhamisi hii, mwanahabari Kenny Claude Nduwimana aliitwa bila taarifa mapema kwa ofisi ya mwendesha mashtaka wa Mukaza katika jiji la kibiashara la
