Burundi : Chama cha CNL kimezuiliwa kuandaa siku maluum ya vijana
Chama kikuu cha upinzani cha CNL kilipanga kuandaa ijumapili hii siku ya kimataifa ya vijana wake. Wizara inayohusika na mambo ya ndani ilitupilia mbali ombi hilo na kudai kuwa siku maluum ya vijana wote tayari ilifanyika mwaka huu. Agathon Rwasa kiongozi wa chama cha CNL anasema hatua hii ni ya “udikteka uliozidi “. HABARI ya SOS Medias Burundi
Kulingana na barua ya katibu anayehusika mambo ya ndani na maendeleo ya ummaa, siku ya kimataifa ya vijana ya wafuasi wa chama cha CNL haingeweza kufanyika. Sababu ni moja : Siku ya kimataifa ya vijana iliadhimishwa tayari mkoani Ngozi kaskazini, sherehe zilifanyika tarehe 12 mwezi uliopita wa agosti.
Calinie Mbarushimana aliwasihi viongozi wa chama hicho cha upinzani nchini Burundi kuwahamasisha vijana wao kuitikia kwa wengi sherehe za siku kama hiyo mwaka ujao.
Agathon Rwasa kiongozi wa chama anasema kuwa hatua hiyo ni “ubaguzi mtupu”. anaona kuwa ni ” udikteka uliozidi”
“Ninaona kuwa ni njia nyingine ya kuonyesha udikteta unaozidi kuimarika katika nchi hii. Hoja zilizotolewa na viongozi wanaohusika haina msimamo. Ni maskitiko kuona wanafanya namna hiyo” analalamika bwana Rwasa.
na kuendelea “[….], chama cha CNDD-FDD ni chama kama vyama vingine, tunawaona wakifanya mandamano hapa na pale, kuhusu haya na yale. Kama una utawala, unaweza kuutumia gisi unavyotaka lakini ni muhimu kuzingatia kuwa kwa wakati mmoja madaraka yanaisha. Hakuna utawala wa milele, bora kuhudumia jamii iwapo uko kwenye utawala”.
Nchini Burundi, vyama vya kisiasa vyote vina matawi ya vijana wafuasi wao. CNDD-FDD na CNL vyote vilivyokuwa makundi ya waasi wa Hutu wako na matawi hayo kwa sehemu kubwa yakijumulisha waliokuwa wapiganaji wa zamani.Wamekuwa wakikabiliana mara kwa mara.Mwezi mei iliyopita, makabiliano kati yao eneo la Ruyumpu tarafani kiremba ( tarafa ya asili ya Agathon Rwasa) katika mkoa wa Ngozi kaskazini mwa Burundi, yalisababisha majeruhi kadhaa kwa pande zote mbili.
Takriban wapinzani saba wanatumikia kifungo cha miaka 15 katika gereza la mkoa. Walipatikana na kosa la ” jaribio la kufanya mauwaji”.
You might also like
Uchaguzi wa wakuu wa vilima Bubanza: Tuhuma za kudanganya na kuzuia matokeo
SOS Médias Burundi Bubanza, Agosti 27, 2025 — Uchaguzi wa kilele cha kilima uliofanyika Agosti 25 katika eneo la Bubanza, Mkoa wa Bujumbura (magharibi mwa Burundi), ulikumbwa na dosari kubwa,
Makamba Chini ya ulinzi : Jinsi CNDD-FDD ilivyozuia uchaguzi wa Juni 5
SOS Médias Burundi Makamba, Juni 7, 2025 – Wakati uchaguzi wa wabunge na manispaa umekamilika katika taifa hilo dogo la Afrika Mashariki, dosari kubwa zinatatiza mchakato wa uchaguzi katika wilaya
Bururi: Evangeline Manirakiza aliyechaguliwa kuwa msimamizi wa kike wa tarafa ya Vyanda, wa kwanza kwa tarafa hio
SOS Media Burundi Vyanda, Aprili 23, 2025 – Baraza la manispaa ya Vyanda, katika mkoa wa Bururi (kusini mwa Burundi), lilimchagua Evangeline Manirakiza Jumatano hii kwenye wadhifa wa msimamizi wa
