Bujumbura: watendaji watatu wa rais wahamishiwa katika gereza la Mpimba
Jean Baptiste Baribonekeza, mkuu wa zamani wa Tume Huru ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu, CNIDH, Cyrille Sibomana na Arcade Harerimana, waliwasili katika gereza la Bujumbura linalojulikana kwa jina la Mpimba mwendo wa saa 8:40 mchana.
HABARI SOS Médias Burundi
Wanaume hao watatu walikuwa wamezuiliwa katika seli za Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi (SNR) tangu siku ya kukamatwa kwao, Alhamisi iliyopita. Mashahidi waliiambia SOS Médias Burundi kwamba watendaji watatu wa ofisi ya rais wa Burundi waliwasili Mpimba mwendo wa saa 8:40 mchana.
https://www.sosmediasburundi.org/2025/01/09/bujumbura-trois-cadres-de-la-presidence-burundaise-detenus-par-les-renseignements/
“Wote watatu walifika hapa, wakiandamana na maafisa wa hati hawakuwa wamevaa mikanda,” shahidi aliyewaona wakiingia gerezani.
Shirika la Kupambana na Ukosefu wa Ajira na Mateso, ALUCHOTO, kilifuatilia kwa karibu oparesheni ya kuondoa msongamano wa magereza. Anaendelea kukashifu shughuli iliyojaa dosari nyingi.
“Tunadai kwamba wale wote waliohusika katika shambulizi lililozingira oparesheni ya kufungua magereza waadhibiwe vikali,” alitangaza Ijumaa iliyopita, Vianney Ndayisaba, mwakilishi wa shirika hili ya ndani, katika mkutano na waandishi wa habari ambao alisimamia katika mji mkuu wa kiuchumi, Bujumbura .
———
Sehemu ya gereza kuu la Bujumbura lijulikanalo kwa jina la Mpimba ambapo watendaji watatu wa ofisi ya rais wa Burundi wamekaa tangu jioni ya Januari 12, 2025, DR.
You might also like
Rumonge: Usafirishaji wa wasichana wadogo
Kigwena Angalau wasichana watano wamekuwa wahanga wa “usafirishaji haramu” huu tangu mwanzoni mwa mwaka huu katika ukanda wa Kigwena wa wilaya na mkoa wa Rumonge (kusini magharibi mwa Burundi).Wazazi wa
Cibitoke: utekaji nyara wa wanachama 4 wa chama cha siasa
Mkuu wa chama cha CDP (Conseil des Patriotes) katika mkoa mpya wa Bujumbura na wanachama wengine watatu wa chama hiki hawajapatikana tangu Jumapili Septemba 15. Chama kinashutumu Imbonerakure (wanachama wa
Goma: kijana mdogo uuwawa na askali polisi katika kituo cha kuandika wapiga kura
Dieudonné Bagenda, miaka 20 aliuwawa kwa kupigwa risasi. Risasi lilimpata kichwani akiwa katika kituo cha kuorodhesha wapiga kura cha Byahi alhamisi hii katika kata ya Bujovu ndani ya mji wa
