Uvira : zaidi ya watu wengine 300 kutoka Burundi wakimbilia nchini DRC

Wanapewa hifadhi katika kambi ya muda ya Sange ndani ya wilaya ya Uvira mkoa wa kivu-kusini (mashariki mwa DRC) tangu siku chache zilizopita. Wahusika ni kutoka hususan katika mikoa ya Cibitoke na Bubanza (kaskazini magharibi mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi

Warundi hao wanadai kuwa walifukuzwa ndani ya ardhi zao na serikali.

” Serikali yetu ilitunyanganya ardhi zetu. Hakuna haki ya kwenda katika mashamba yetu. Kilichosalia kwetu ni kukimbia” walilaani wajumbe wa kundi kundi hilo waliozungumza na SOS Médias Burundi.

Ardhi hizo zinazozungumziwa zinapatikana eneo la Mabayi, Nyarure, Rugombo, Mbazamiduha katika mkoa wa Cibitoke pamoja na Kibira-Rukoko mkoani Bubanza.

Mmoja kati ya viongozi wa kambi hiyo ya muda ya Sange anafahamisha kuwa takriban waomba hifadhi hao wote, wanakutania katika hoja moja : Kunyanganywa ardhi zao”.

Kuhusu swala hilo, gavana wa mkoa wa Cibitoke anapinga madai hayo. Carême Bizoza anafahamisha kuwa serikali ilirejesha ardhi ambazo zilikuwa miliki yake. Anatoa mifano ya ardhi za Nyarure na Mbazamiguha.

Mkoani Bubanza, gavana anasema ni eneo ambako kunafanyika mazoezi ya kijeshi.

Lakini waomba hifadhi hao kutoka Burundi ” wanadai ni ukiukwaji wa haki zao”.

Katika miaka ya hivi karibuni, walishuhudiwa warundi wanaokimbilia nchini RDC kutokana na njaa mbali na wale waliokimbia kutokana na unyanyasaji dhidi ya wapinzani lakini hii imekuwa mara ya kwanza kwa nchi hiyo kubwa ya Afrika ya kati kuwapokea watu wenye asili ya Burundi kwa idadi kubwa wanaotoroka kwa sababu ya Kunyanganywa ardhi za kilimo.

Previous Tanzania : viongozi tawala wawahamasisha wakimbizi kuhusu kuheshimu sheria ambazo wao wanazikiuka kila mara
Next Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo

You might also like

Siasa

Burundi: Bunge la kitaifa la 2025-2030 limetawaliwa kabisa na CNDD-FDD

SOS Médias Burundi Bujumbura, Juni 11, 2025 – Burundi inaingia katika muhula wa kisheria ambao haujawahi kushuhudiwa. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (CENI) ilitangaza Jumatano hii kwamba manaibu wote

Siasa

Usambazaji wa kadi za uchaguzi: wakazi walio katika matatizo kaskazini-magharibi, kuongezwa kwa tarehe ya mwisho iliyoombwa

SOS Media Burundi Cibitoke, Mei 14, 2025 – Mwishoni mwa usambazaji wa kadi za uchaguzi, wananchi wa mikoa ya Cibitoke, Bubanza na Bujumbura, kaskazini-magharibi mwa Burundi, wanakashifu utendakazi katika mchakato

Criminalité

Ndayishimiye na CNDD-FDD wanaweka utaratibu wao na vitisho huko Gitega

SOS Médias Burundi Gitega, Agosti 30, 2025 – Katika mji mkuu uliozuiliwa chini ya ulinzi mkali, serikali ya Burundi iliadhimisha Siku ya 9 ya Imbonerakure, pamoja na maadhimisho ya miaka