Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo
Janga la kibinadamu linaendelea kutokea katika mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC, lilitahadharisha shirika la MSF la waganga wasiokuwa na mipaka. Shirika hilo la waganga la kimataifa linatoa mwito kwa jamii ya kimataifa na viongozi wa Kongo kuongeza juhudi katika kukidhi mahitaji ya wananchi walioathiriwa na mapigano ya silaha. HABARI SOS Médias Burundi
Takriban watu milioni moja walikimbia mapigano baada ya kuibuka kwa kundi la silaha la M23 eneo la Kivu kaskazini katika kipindi cha mwaka ulioyopita. Misaada hadi sasa haitoshi kulingana na MSF.
Watu madhaifu wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi yakiwemo maradhi ya kipindupindu, ukomaa , utapia mloo na kunyanyaswa kijinsia.
” Mzozo wa Kivu kaskazini umekuwa na madhara makubwa kutokana na ukubwa wake lakini pia misaada imekuwa ikichelewa katika maeneo mengi”, alifahamisha Avril Benoît, kiongozi mtendaji wa MSF-USA ambaye kwa sasa yuko mjini Goma.
” Kuna uhaba mkubwa wa misaada ili kukidhi mahitaji ya msingi ya wananchi kuhusiana na makaazi, madawa, vyakula na maji safi. Tunashuhudia kuwa madhara katika afya yao ni makubwa na yanaendelea kuongezeka, alizidi kusema.
Katika miezi ya hivi karibuni, ma mia ya ma elfu ya wananchi walitoroka makaazi yao na vijiji vyao na kwenda kuishi katika familia zilizowapokea na ndani ya vituo visivyokuwa rasmi. Pembeni ya Goma makaazi yaliyotengenezwa kwa kutumia hema za plastiki au vyandarua yamejaa huku watu wengine wakihifadhiwa ndani ya majengo ya kanisa na shule.
Wajumbe wa MSF wanahudumu katika vituo vya wakimbizi pembeni ya mji wa Goma tangu 2022 kwa kuwapa madawa bila kuwalipisha, gari za shirika hilo liliwapelekea maji safi na kuwajengea vyoo na baafu.
Mapigano yanaendelea kuripotiwa katika maeneo tofauti ya Kivu kaskazini na kuzidi kusababisha idadi kubwa ya wananchi kutimka
You might also like
Buhumuza: Zaidi ya wakimbizi 67,000 katika kambi ya Busuma wakabiliwa na mgogoro wa maji na usafi wa mazingira
SOS Médias Burundi Ruyigi, Januari 12, 2026 – Kwa kuzidiwa na msongamano mkubwa wa watu, kambi ya wakimbizi ya Busuma, iliyoko katika tarafa ya Ruyigi, mkoa wa Buhumuza, mashariki mwa
Musenyi: Mshikamano wa mpaka – Angéline Ndayishimiye na Denise Nyakeru Tshisekedi wanakutana na wakimbizi wa Kongo
SOS Médias Burundi Musenyi, Aprili 30, 2025 – Marais wa Marais wa Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo walifanya ziara ya pamoja katika eneo la wakimbizi la Musenyi, kusini-mashariki
Goma: zaidi ya wakazi 17,000 wapya waliohama makazi yao kutokana na vita kati ya jeshi la kawaida na waasi wa M23
Zaidi ya watu 17,000 waliokimbia makazi yao wamesajiliwa katika kambi mpya iliyoundwa katika mji wa Goma katika jimbo la Kivu Kaskazini (mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo). Kulingana na
