Nakivale-Mahama : zoezi la kuhesabu upya wakimbizi na kuhakiki tena hadhi zao za ukimbizi lasababisha wasi wasi kwa wahusika
Katika kambi za wakimbizi za Nakivale nchini Uganda na Mahama nchini Rwanda wakati huu ni wa kuhesabu upya na kuhakiki hadhi za wakimbizi. Programu hiyo inatelezwa na HCR na inataraji kumalizika tarehe 23 aprili 2023 nchini Rwanda. Wahusika wanahofia hatua zinazoweza kuchukuliwa baada ya zoezi hilo. HABARI SOS Médias Burundi
Shughuli ya kukusanya takwimu mpya inafanyika katika kambi ambako wakimbizi walirejea makwao kwa hiari. Nchini Uganda, shughuli hiyo ilifanyika hususan katika kambi ya Nakivale na nchini Rwanda kambi ya Mahama ndio iliyolengwa.
” Ni zoezi la kuweka sawa mfumo wa kuorodhesha wakimbizi. HCR inafanya kazi hiyo ili kuimarisha mfumo huo na kuongeza uwajibikaji wake”, linaeleza tangazo la HCR kuhusu shughuli hiyo.
Wajumbe wa shirika hilo la umoja wa mataifa walifahamisha wakimbizi wa kambi ya Nakivale kuwa wanatakiwa kujiandaa kwa mabadiliko kuhusu namna wanavyopewa misaada baada ya zoezi hilo kumalizika.
” Mgawo wa chakula unaweza kupungua ikizingatiwa pia kuwa wakimbizi nao walipunguka kwa kiwango wa kutosha. Mfumo wa kuwasaidia kwa kuwapa pesa nao pia utashuhudia mabadiliko” walibaini.
Katika kambi ya wakimbizi ya Mahama, wakaazi wanasema pia kuwa wanajiandaa kupata baadhi ya habari mbaya. Lakini HCR inawatuliza.
” Munaweza kutaraji ucheleweshaji wa baadhi ya huduma, lakini hilo halitakuwa na madhara kwa programu ya misaada. Wanaopata msaada wa chakula na msaada mwingine hawataathiriwa na mchakato huo na wataendelea kupata misaada yao katika kipindi hicho kama kawaida”, HCR-Rwanda inatuliza na kuzidi kuwa mchakato wa kukusanya takwimu mpya utaendelea hadi 23 aprili 2023.
Wakimbizi wanataraji kuwa baada ya sensa hiyo, HCR badala yake itaongeza kuwango cha pesa ya matumizi inayotolewa ikizingatiwa kuwa bei zilipanda katika masoko ya ndani.
Nakivale inaorodhesha zaidi ya wakimbizi 140.000 wakiwemo elfu 33 kutoka Burundi wakati Mahama upande wake ikitoa hifadhi kwa wakimbizi elfu 45 idadi kubwa wakiwa kutoka Burundi.
You might also like
Nakivale (Uganda): Takriban madereva wanne wa pikipiki waliuawa katika muda wa mwezi mmoja, jambo lililozua wasiwasi katika kambi ya wakimbizi.
SOS Médias Burundi Nakivale, Septemba 3, 2025 – Kambi ya wakimbizi ya Nakivale, iliyoko katika wilaya ya Isingiro, kusini-magharibi mwa Uganda, imekumbwa na mfululizo wa mauaji yanayolenga waendesha pikipiki. Takriban
Tanzania: ‘Wanataka kutulazimisha kurudi’ – Wakimbizi wa Burundi wanashutumu mahojiano yaliyoshinikizwa
SOS Médias Burundi Nduta, Mei 22, 2025 – Katika kambi za wakimbizi za Burundi za Nduta na Nyarugusu, “mahojiano ya kabla ya uchaguzi” yaliyofanywa na UNHCR na mamlaka ya Tanzania
Burundi: Uhamisho wa kulazimishwa kutoka uswizi, kurudi kwa mvutano, na mashtaka ya mateso yanakanushwa na wataalam
SOS Médias Burundi Burundi, Mei 24, 2026 – Kurejea Burundi kwa vijana kadhaa waliofukuzwa kutoka Uswizi kunazua wasiwasi na maswali miongoni mwa familia zao, katika muktadha ambao tayari umekumbwa na
