Cibitoke : mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa katika msitu wa Kibira
Kundi la wachimba migodi wanaofanya kazi hiyo kwa kujificha walilengwa na wanajeshi usiku wa tarehe 8 kuamkia tarehe 9 aprili ndani ya msitu wa hifadhi wa Kibira. Tukio hilo lilijiri katika mlima wa Gafumbegeti, kijiji cha Butahana tarafa ya Mabayi katika mkoa wa Cibitoke (kaskazini magharibi mwa Burundi). Mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muhanga ni mwenye umri wa miaka 40, mjumbe wa moja kati ya vyama vya ushirika 17 vinavyojihusisha na kuchimba madini tarafani Mabayi ambavyo havijapata leseni.
” kwa jumla ya vyama vya ushirika 21, ni nne peke ambavyo vina idhini ya kuchimba dhahabu, na muhanga alikuwa akifanya kazi hiyo kwa kujificha”, chanzo cha polisi kilieleza.
Mchimba madini mwingine anayefanya kazi kwa kujificha pia alijeruhiwa vikali baada ya kupigwa risasi tatu kwenye mguu wake wa kulia, kwa mjibu la chanzo cha polisi.
Angalau wachimba migodi 13 waliangamia wiki iliyopita kutokana na mvua kubwa iliyowakuta baadhi yao katika migodi miwili ya dhahabu ndani ya tarafa hiyo ya kaskazini magharibi mwa Burundi.
Tukio hilo liliibua hisia kwa wananchi ambao wanadai ni jukumu la viongozi tawala kujali maisha ya wachimba madini kwa kuwarahisishia kupata vifaa vya kujilinda pamoja na bima”.
Akihojiwa kuhusiana na mkasa huo, gavana wa mkoa wa Cibitoke anawataka wachimba madini wanaojumuika katika vyama vya ushirika kuwa na uvumilivu wakisubiri hatua ya kuruhusu uchimbaji madini kuanza kutekelezwa katika migodi tofauti.
Kiongozi huyo anaomba vikosi vya ulinzi na usalama kuendelea kuheshimisha hatua ya kuzuia uchimbaji wa dhahabu katika migodi kadhaa
You might also like
Kabarore: wawili Imbonerakure walimuua kijana aliyejaribu kwenda Rwanda
Philippe Nsabimana, 22, aliuawa Ijumaa hii mwendo wa saa mbili usiku. Uhalifu huo ulifanyika katika mji wa Ryamukona unaotazamana na Mto Kanyaru unaotenganisha mataifa dada ya Maziwa Makuu ya Afrika.
Bubanza: Hasira na wasiwasi wa wakulima juu ya upungufu wa urea unaoendelea
SOS Médias Burundi Bubanza, Mei 18, 2026 — Wakulima katika tarafa ya Bubanza, katika mkoa wa Bujumbura, magharibi mwa Burundi, wanashutumu uhaba unaoendelea wa mbolea za kemikali zenye urea, licha
Mabayi : waziri mkuu wa serikali ya Burundi atishia kuwauwa watu wote wanaoshirikiana na waasi wa Rwanda waliopiga kambi ndani ya msitu wa Kibira
Tangazo lilitolewa jumanne hii kando na mkutano wa waziri mkuu Gervais Ndirakobuca na wawakilishi wa viongozi, maafisa wa usalama pamoja na waakazi wa tarafa ya Mabayi mkoa wa Cibitoke (kaskazini
