Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Tangu disemba 2022, angalau watoto 60 waliuwawa katika vurugu za makundi ya silaha mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Takwimu hizo zilitolewa na ujumbe wa shirika la umoja wa mataifa kwa ajili ya amani nchini Kongo (MONUSCO) ofisi ya mkoa. HABARI SOS Médias Burundi

Takwimu hizo za kusikitisha zilitolewa wakati wa uzinduzi wa mazungumzo ya jamii ya Hema yanayofanyika eneo la Bunia tangu siku chache zilizopita.

Karna Soro, mkuu wa MONUSCO mkoani Ituri, anaeleza kuwa watoto hao ni kati ya wananchi 310 waliouwawa na vikundi vinavyotajwa kuwa vibaya tangu mwishoni mwa mwaka jana mkoani Ituri.

” Kati ya tarehe mosi disemba 2022 na 21 machi 2023, tumeorodhesha watu 310 waliuwawa wakiwemo watoto 60. Nadhani katika lugha zetu za Afrika, hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kutoa maana ya hali hiyo. Ituri, Kongo ni ikulu yenu ya dhahabu. Licha ya matatizo na changamoto, tuungane. Damu ni nyingi, mateso ni mengi, hali hiyo inatakiwa kusimama”, alibaini.

Baadhi ya mashirika ya kutetea haki za watoto yanaomba ulinzi kwa watoto upewe kipau mbele na viongozi na pia makundi ya silaha.

Previous Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Next Cibitoke : mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa katika msitu wa Kibira

You might also like

DRC Sw

Masisi: Zaidi ya watu 200 wamekufa kutokana na maporomoko ya udongo kwenye mgodi wa ufundi huko Rubaya

Goma, Januari 31, 2026 – Msiba umekumba eneo la uchimbaji madini la Rubaya katika eneo la Masisi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Zaidi ya wachimba migodi 200 walipoteza

Wakimbizi

Busuma: Kunusurika vitani tu kufa kwa kutojali

SOS Médias Burundi Ruyigi, Machi 2, 2026 – Mkimbizi wa Kongo alipatikana amefariki kilomita chache kutoka kambi ya Busuma mashariki mwa Burundi Jumapili, Machi 1, baada ya kutoweka kwa siku

DRC Sw

Goma: Kurudi kwa Joseph Kabila kunazua hisia tofauti kwa maoni ya umma

SOS Médias Burundi Goma, Aprili 19, 2025 – Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila Kabange, alirejea kwa njia ya kushangaza Ijumaa hii, Aprili 18, huko Goma,