Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Tangu disemba 2022, angalau watoto 60 waliuwawa katika vurugu za makundi ya silaha mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Takwimu hizo zilitolewa na ujumbe wa shirika la umoja wa mataifa kwa ajili ya amani nchini Kongo (MONUSCO) ofisi ya mkoa. HABARI SOS Médias Burundi

Takwimu hizo za kusikitisha zilitolewa wakati wa uzinduzi wa mazungumzo ya jamii ya Hema yanayofanyika eneo la Bunia tangu siku chache zilizopita.

Karna Soro, mkuu wa MONUSCO mkoani Ituri, anaeleza kuwa watoto hao ni kati ya wananchi 310 waliouwawa na vikundi vinavyotajwa kuwa vibaya tangu mwishoni mwa mwaka jana mkoani Ituri.

” Kati ya tarehe mosi disemba 2022 na 21 machi 2023, tumeorodhesha watu 310 waliuwawa wakiwemo watoto 60. Nadhani katika lugha zetu za Afrika, hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kutoa maana ya hali hiyo. Ituri, Kongo ni ikulu yenu ya dhahabu. Licha ya matatizo na changamoto, tuungane. Damu ni nyingi, mateso ni mengi, hali hiyo inatakiwa kusimama”, alibaini.

Baadhi ya mashirika ya kutetea haki za watoto yanaomba ulinzi kwa watoto upewe kipau mbele na viongozi na pia makundi ya silaha.

Previous Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Next Cibitoke : mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa katika msitu wa Kibira

You might also like

Criminalité

Kivu Kusini: Wanajeshi wa Burundi kwa wingi Fizi kupunguza mwendo wa Twirwaneho na kuwadhibiti M23

SOS Media Burundi Bukavu, Mei 22, 2025 – Harakati kubwa za kijeshi zimezingatiwa katika siku za hivi majuzi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Tangu Jumatano, wanajeshi wapya wa

DRC Sw

Ituri: kuonekana kwa kikundi kipya cha silaha kunasisitiza ukosefu wa usalama

Mkoa wa Ituri ulioko mashariki mwa Kongo unaendelea kuwa eneo la machafuko ya muda mrefu, yanayochangiwa na kuzuka upya kwa makundi yenye silaha. Baada ya CRP (Mkataba wa Mapinduzi Mashuhuri)

DRC Sw

Uvira: madarasa yarejea katika shule za umma baada ya zaidi ya miezi miwili ya mgomo

Wiki iliyopita, baadhi ya walimu katika jimbo la Kivu Kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) walianza kufundisha tena madarasa. Walikuwa wamegoma kwa zaidi ya miezi miwili. Ingawa