Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri
Tangu disemba 2022, angalau watoto 60 waliuwawa katika vurugu za makundi ya silaha mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Takwimu hizo zilitolewa na ujumbe wa shirika la umoja wa mataifa kwa ajili ya amani nchini Kongo (MONUSCO) ofisi ya mkoa. HABARI SOS Médias Burundi
Takwimu hizo za kusikitisha zilitolewa wakati wa uzinduzi wa mazungumzo ya jamii ya Hema yanayofanyika eneo la Bunia tangu siku chache zilizopita.
Karna Soro, mkuu wa MONUSCO mkoani Ituri, anaeleza kuwa watoto hao ni kati ya wananchi 310 waliouwawa na vikundi vinavyotajwa kuwa vibaya tangu mwishoni mwa mwaka jana mkoani Ituri.
” Kati ya tarehe mosi disemba 2022 na 21 machi 2023, tumeorodhesha watu 310 waliuwawa wakiwemo watoto 60. Nadhani katika lugha zetu za Afrika, hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kutoa maana ya hali hiyo. Ituri, Kongo ni ikulu yenu ya dhahabu. Licha ya matatizo na changamoto, tuungane. Damu ni nyingi, mateso ni mengi, hali hiyo inatakiwa kusimama”, alibaini.
Baadhi ya mashirika ya kutetea haki za watoto yanaomba ulinzi kwa watoto upewe kipau mbele na viongozi na pia makundi ya silaha.
About author
You might also like
DR Congo: Waasi wa M23 waliuteka Goma
Mji wa Goma uliangukia mikononi mwa waasi wa M23 Jumatatu hii, Januari 27. Rais wa Kenya William Ruto, ambaye anaongoza jumuiya ya kiuchumi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ameitisha mkutano
Burundi:Hata kama imekosolewa, mamlaka ya mwandishi maalum wa Umoja wa Mataifa yaongezwa
Ilikuwa ni kikao cha Alhamisi hii ambacho kilipiga kura ya kuongezwa kwa mwaka mmoja kwa mamlaka ya Burkinabè Fortune Gaétan Zongo. Mwandishi Maalum kuhusu Burundi anakosolewa ndani na serikali na
Burundi: hali ya kutisha ya shule kwa wakimbizi katika Kambi ya Kavumba
Kambi ya wakimbizi ya Kavumu iliyoko katika wilaya na jimbo la Cankuzo mashariki mwa Burundi na inahifadhi zaidi ya wakimbizi 18,000, inaona elimu ya watoto inatatizika sana. Wazazi hao wanaomba