Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Tangu disemba 2022, angalau watoto 60 waliuwawa katika vurugu za makundi ya silaha mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Takwimu hizo zilitolewa na ujumbe wa shirika la umoja wa mataifa kwa ajili ya amani nchini Kongo (MONUSCO) ofisi ya mkoa. HABARI SOS Médias Burundi

Takwimu hizo za kusikitisha zilitolewa wakati wa uzinduzi wa mazungumzo ya jamii ya Hema yanayofanyika eneo la Bunia tangu siku chache zilizopita.

Karna Soro, mkuu wa MONUSCO mkoani Ituri, anaeleza kuwa watoto hao ni kati ya wananchi 310 waliouwawa na vikundi vinavyotajwa kuwa vibaya tangu mwishoni mwa mwaka jana mkoani Ituri.

” Kati ya tarehe mosi disemba 2022 na 21 machi 2023, tumeorodhesha watu 310 waliuwawa wakiwemo watoto 60. Nadhani katika lugha zetu za Afrika, hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kutoa maana ya hali hiyo. Ituri, Kongo ni ikulu yenu ya dhahabu. Licha ya matatizo na changamoto, tuungane. Damu ni nyingi, mateso ni mengi, hali hiyo inatakiwa kusimama”, alibaini.

Baadhi ya mashirika ya kutetea haki za watoto yanaomba ulinzi kwa watoto upewe kipau mbele na viongozi na pia makundi ya silaha.

Previous Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Next Cibitoke : mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa katika msitu wa Kibira

You might also like

Diplomasia

Bukavu: Mkutano wa kimkakati kati ya viongozi wa jeshi la Kongo na Burundi

SOS Médias Burundi Bukavu, Mei 15, 2025 — Mkutano wa ngazi ya juu ulifanyika Jumatano hii katika jiji la Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kati ya wakuu

DRC Sw

Kinshasa: Mamlaka ya Kongo yatangaza kuzuia mapinduzi

Jeshi la DRC linadai “kuzuia mapinduzi” Jumapili asubuhi. Watu watatu waliokuwa na silaha waliuawa baada ya kupigwa risasi karibu na ikulu ya rais. HABARI SOS Media Burundi Jeshi la Kongo

DRC Sw

Kivu Kusini: FDNB Yaimarisha nafasi yake dhidi ya M23 na washirika wake wa Twirwaneho

SOS Médias Burundi Bukavu, Oktoba 16, 2025 – Licha ya kutiwa saini kwa makubaliano ya kusitisha mapigano mnamo Oktoba 14 huko Doha kati ya serikali ya Kongo na waasi wa