Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Muili wa Gilbert Ndacayisaba mwenye umri wa miaka 47 ulipatikana katika shamba la miti ya mikaratusi alhamisi mchana. Mkaazi huyo wa kijiji cha Karungura tarafani Mwumba mkoa wa Ngozi (Kaskazini mwa Burundi), alikuwa mmoja kati ya viongozi wa chama hicho cha upinzani katika eneo hilo. Watu wake wa karibu wanadai kuwa huenda aliuwawa na Imbonerakure (wajumbe wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD). Wawili kati ya Imbonerakure wanne wanaotuhumiwa mauwaji hayo walikamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muili wake ulikuwa ndani ya mfuko wakati ulipogunduliwa na watoto waliokuwa wakitafuta kuuni za kupikia.
” Tuliona mfuko ambao ndani yake kulikuwa kitu. Tuliangalia na tukagundua kuwa ndani kuna maiti. Tulipata woga, tukatoa taarifa kwa wakaazi”, alieleza shahidi mmoja katika wale waliofanya ugunduzi huo wa kutisha.
Kwa mjibu wa mfuasi wa chama cha CNL katika kijiji hicho cha Karungura, marehemu alikuwa miongoni mwa viongozi wa chama hicho cha upinzani eneo hilo. Huenda aliuwawa kutokana na msimamo wake wa kisiasa.
” Mara nyingi alifanyiwa vitisho na Imbonerakure wa kijiji cha Karungura ambao nia yao walitaka ajiunge na chama tawala cha CNDD-FDD lakini bila kufanikiwa. Waliahidi hata kumupa adhabu. Hatukuamini kuwa wangefikia hata kumumalizia maisha”, walieleza wafuasi wa chama hicho.
Imbonerakure wawili walikamatwa, wawili wengine walikimbia. Wanatuhumiwa kuhusika na mauwaji hayo.
Waliokamatwa, wanazuiliwa katika kamishena ya polisi ya Mwumba.
Polisi inahakikisha kuwa uchunguzi unafanyika.
Gilbert Ndacayisaba alitoweka jumatano tarehe 6 aprili jioni wakati akielekea nyumbani kwake kwa mjibu wa watu wa karibu yake. Wanaomba ufanyike uchunguzi huru.
About author
You might also like
Kuhusu-Bunyoni : kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia abadilishwa
Ni wizara ya mambo ya ndani na usalama iliyochukuwa uamzi huo. Kanali wa polisi Désiré Uwamahoro aliyekuwa kiongozi wa kikosi kinachokosolewa cha kutuliza ghasia (BAE) alirejelewa na kanali mwingine. Jonathan
Bujumbura: Maafisa wawili wa polisi wahukumiwa kulipa faini kwa kumpiga kiongozi wa chama cha siasa
Ilikuwa ni mahakama ya Ntahangwa kaskazini mwa jiji la kibiashara la Bujumbura ambayo iliwahukumu maajenti hao wawili siku ya Jumanne. Gabriel Banzawitonde, rais wa chama cha wahanga wa APDR, anasema
Tanzania-Burundi: Polisi wa Tanzania wawasafirisha zaidi ya Warundi 60, wengi wao wakiwa ni watoto wadogo
Polisi wa Tanzania wamewakabidhi takriban watoto arobaini wa Burundi kwa mamlaka ya Burundi katika kituo cha mpaka cha Mugina katika wilaya ya Mabanda katika jimbo la Makamba (kusini mwa Burundi)