DRC : sheria kuhusu uhuru wa vyombo vya habari inataraji kutangazwa
Waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari Patrick Muyaya alifanikisha azma yake jumanne hii mbele ya wabunge wa kitaifa. Mswada wake wa sheria kuhusu marekebisho ya sheria ya kiwaziri inayopanga utaratibu wa kutekeleza uhuru wa vyombo vya vyombo vya habari, uhuru katika kutoa habari na vipindi vya radio na televisheni, magazeti na njia zingine za mawasiliano nchini DRC uliidhinishwa na bunge la taifa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa waziri Muyaya, mswada huo wa sheria unaonyesha muono wa rais wa jamuhuri na madili ya kuwajibika kwa serikali na kuimarisha hadhi ya nchi.
Bwana Muyaya alizidi kufahamisha kuwa utafiti kuhusu hali ya uhuru wa kujieleza tayari ulifanyika.
” Tulianza zoezi hilo kwa ushirikiano na mashirika ya wandishi wa habari mbali mbali ili kuangalia hali halisi ya uhuru wa kujieleza upande mmoja na hali jumla ya vyombo vya habari katika nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha uhuru wa kujieleza”, alibaini waziri.
Licha ya upinzani wa baadhi ya wabunge wa nchi kuhusu utekelezwaji wa haraka wa sheria hiyo, waziri Muyaya alionyesha umuhimu wake ili kufikia hatua nyingine katika sekta ya vyombo vya habari nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
” Iwapo serikali imeamuru kutoa kipau mbele kwa sheria hiyo ni kwa sababu kuna dharura. Sheria hiyo itasaidia kumaliza idadi kubwa ya matatizo yanayosumbua kila siku katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na dosari na kwenda kinyume kwa baadhi ya vyombo vya habari hususan vyombo vya mitandaoni huku teknolojia ikiendelea kwa kasi kubwa”, alisisitiza waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari.
Na kuzidi kuwa : ” Ninawaambia kuwa radio zote hazienezi vigezo. Hakuna sheria inayozihusu. Kwa hiyo hatuwezi kuchelewesha kutekeleza sheria hiyo. Kuna haja ya haraka iki kurejesha mamlaka ya serikali “.
Ikumbukwe bunge la taifa lilifanya tathmini na uidhinishwaji wa miswada mingine saba ya sheria kuhusu kurekebisha sheria za kiwaziri zilizochukuliwa katika kutoa mamlaka kwa serikali .
You might also like
Kielezo cha RSF 2026: Burundi yafanya maendeleo katikati ya kurudi nyuma kwa uhuru wa kihistoria wa vyombo vya habari
SOS Médias Burundi Bujumbura, Mei 1, 2026 – Burundi inashika nafasi ya 119 kati ya nchi 180 katika Fahirisi ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ya 2026 iliyochapishwa Alhamisi
Kivu-Kaskazini : zaidi ya wananchi 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja eneo la Beni
Katika kitongoji cha Ruwenzori wilaya ya Beni mkoa wa Kivu-kaskazini (mashariki mwa DRC) , zaidi ya watu 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja. Takwimu hizo zinatolewa na ofisi ya
Kaburantwa – DRC: Misafara ya wanajeshi wa Burundi wakielekea Kivu Kusini, huku kukiwa na mvutano wa kikanda na kimya rasmi
SOS Médias Burundi Bujumbura, Septemba 2, 2025 — Kwa muda wa siku tatu, misafara mizito ya wanajeshi wa Burundi imekuwa ikipitia mji wa Kaburantwa, katika eneo la Cibitoke mkoani Bujumbura,
