DRC : sheria kuhusu uhuru wa vyombo vya habari inataraji kutangazwa
Waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari Patrick Muyaya alifanikisha azma yake jumanne hii mbele ya wabunge wa kitaifa. Mswada wake wa sheria kuhusu marekebisho ya sheria ya kiwaziri inayopanga utaratibu wa kutekeleza uhuru wa vyombo vya vyombo vya habari, uhuru katika kutoa habari na vipindi vya radio na televisheni, magazeti na njia zingine za mawasiliano nchini DRC uliidhinishwa na bunge la taifa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa waziri Muyaya, mswada huo wa sheria unaonyesha muono wa rais wa jamuhuri na madili ya kuwajibika kwa serikali na kuimarisha hadhi ya nchi.
Bwana Muyaya alizidi kufahamisha kuwa utafiti kuhusu hali ya uhuru wa kujieleza tayari ulifanyika.
” Tulianza zoezi hilo kwa ushirikiano na mashirika ya wandishi wa habari mbali mbali ili kuangalia hali halisi ya uhuru wa kujieleza upande mmoja na hali jumla ya vyombo vya habari katika nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha uhuru wa kujieleza”, alibaini waziri.
Licha ya upinzani wa baadhi ya wabunge wa nchi kuhusu utekelezwaji wa haraka wa sheria hiyo, waziri Muyaya alionyesha umuhimu wake ili kufikia hatua nyingine katika sekta ya vyombo vya habari nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
” Iwapo serikali imeamuru kutoa kipau mbele kwa sheria hiyo ni kwa sababu kuna dharura. Sheria hiyo itasaidia kumaliza idadi kubwa ya matatizo yanayosumbua kila siku katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na dosari na kwenda kinyume kwa baadhi ya vyombo vya habari hususan vyombo vya mitandaoni huku teknolojia ikiendelea kwa kasi kubwa”, alisisitiza waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari.
Na kuzidi kuwa : ” Ninawaambia kuwa radio zote hazienezi vigezo. Hakuna sheria inayozihusu. Kwa hiyo hatuwezi kuchelewesha kutekeleza sheria hiyo. Kuna haja ya haraka iki kurejesha mamlaka ya serikali “.
Ikumbukwe bunge la taifa lilifanya tathmini na uidhinishwaji wa miswada mingine saba ya sheria kuhusu kurekebisha sheria za kiwaziri zilizochukuliwa katika kutoa mamlaka kwa serikali .
You might also like
DRC: Ebola yapungua Bunia na Goma huku watu kadhaa wakipona, nchi jirani ziko katika tahadhari
SOS Médias Burundi Bunia/Goma, Juni 4, 2026 – Mapambano dhidi ya mlipuko mpya wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) yanaonyesha maendeleo ya kutia moyo na ahueni kadhaa
Ngozi: Mwanahabari Sandra Muhoza aendelea kushikiliwa licha ya kutolewa kwa wito wa kuachiliwa kwake
SOS Médias Burundi Ngozi, Oktoba 14, 2025 — Mahakama Kuu ya Ngozi iliamua Oktoba 14 kuendelea kumweka kizuizini mwandishi wa habari Sandra Muhoza, akisubiri mapitio ya kina ya kesi yake.
DRC: Mashambulio ya mabomu, mivutano ya kijeshi, na mashindano ya kikanda katika kiini cha mapigano ya muda mrefu mashariki mwa nchi.
SOS Médias Burundi Bukavu, Machi 22, 2026 – Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wimbi jipya la shutuma za milipuko ya mabomu inayolenga raia linazidisha hali ya wasiwasi katika
