DRC : sheria kuhusu uhuru wa vyombo vya habari inataraji kutangazwa
Waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari Patrick Muyaya alifanikisha azma yake jumanne hii mbele ya wabunge wa kitaifa. Mswada wake wa sheria kuhusu marekebisho ya sheria ya kiwaziri inayopanga utaratibu wa kutekeleza uhuru wa vyombo vya vyombo vya habari, uhuru katika kutoa habari na vipindi vya radio na televisheni, magazeti na njia zingine za mawasiliano nchini DRC uliidhinishwa na bunge la taifa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa waziri Muyaya, mswada huo wa sheria unaonyesha muono wa rais wa jamuhuri na madili ya kuwajibika kwa serikali na kuimarisha hadhi ya nchi.
Bwana Muyaya alizidi kufahamisha kuwa utafiti kuhusu hali ya uhuru wa kujieleza tayari ulifanyika.
” Tulianza zoezi hilo kwa ushirikiano na mashirika ya wandishi wa habari mbali mbali ili kuangalia hali halisi ya uhuru wa kujieleza upande mmoja na hali jumla ya vyombo vya habari katika nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha uhuru wa kujieleza”, alibaini waziri.
Licha ya upinzani wa baadhi ya wabunge wa nchi kuhusu utekelezwaji wa haraka wa sheria hiyo, waziri Muyaya alionyesha umuhimu wake ili kufikia hatua nyingine katika sekta ya vyombo vya habari nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
” Iwapo serikali imeamuru kutoa kipau mbele kwa sheria hiyo ni kwa sababu kuna dharura. Sheria hiyo itasaidia kumaliza idadi kubwa ya matatizo yanayosumbua kila siku katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na dosari na kwenda kinyume kwa baadhi ya vyombo vya habari hususan vyombo vya mitandaoni huku teknolojia ikiendelea kwa kasi kubwa”, alisisitiza waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari.
Na kuzidi kuwa : ” Ninawaambia kuwa radio zote hazienezi vigezo. Hakuna sheria inayozihusu. Kwa hiyo hatuwezi kuchelewesha kutekeleza sheria hiyo. Kuna haja ya haraka iki kurejesha mamlaka ya serikali “.
Ikumbukwe bunge la taifa lilifanya tathmini na uidhinishwaji wa miswada mingine saba ya sheria kuhusu kurekebisha sheria za kiwaziri zilizochukuliwa katika kutoa mamlaka kwa serikali .
You might also like
Uvira: Wanachama wa Wazalendo wanaotuhumiwa kwa unyanyasaji dhidi ya jamii ya Banyamulenge
Jamii ya Banyamulenge, wanaoishi katika mji wa Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), inaendelea kukumbwa na dhuluma zinazofanywa na baadhi ya wapiganaji kutoka vikundi vya wapiganaji wa
Kivu Kusini: Raia wauawa na kutekwa nyara huko Mikalati – Jeshi la Burundi lashtakiwa tena
SOS Médias Burundi Bukavu, Desemba 7, 2025 – Hali ya usalama ilizorota sana wikendi hii huko Kivu Kusini, ambapo shambulio lililohusishwa na wanajeshi wa Burundi liliwalenga raia waliokuwa wakirejea kutoka
Uholanzi inafunga ubalozi wake mjini Bujumbura: uamuzi wenye athari kubwa kwa ushirikiano wa nchi mbili
SOS Media Burundi – Bujumbura, Aprili 19, 2025 – Serikali ya Uholanzi imetangaza kufungwa kwa mawasilisho yake kadhaa ya kidiplomasia, ikiwa ni pamoja na ubalozi wa Bujumbura, mji mkuu wa
