Burundi : shirikisho la vyama viwili vya kutetea haki za wafanyakazi vinaomba CNDS kuingilia kati katika mzozo dhidi ya serikali
Mashirikisho ya vyama vya wafanyakazi COSYBU na CSB vinapaza sauti dhidi ya kusimamishwa kwa tozo za michango ya wajumbe wao. Serikali iliweka hatua ya kupiga marufuku michango ya wajumbe wa vyama vya wafanyakazi kuchukuliwa moja kwa moja kwenye mishahara yao. Mashirika hayo mawili yanaomba upatanishi wa kamati ya kitaifa ya mjadala wa kijamii (CNDS) ufanyike kuhusu swala hilo. HABARI SOS Médias Burundi
Kupitia malalamiko dhidi ya serikali ya Burundi yaliyowasilishwa kwa mkuu wa kamati ya kitaifa ya mjadala wa kijamii, shirikisho la vyama vya wafanyakazi COSYBU na CSB vinatoa wito, kwa niaba ya vyama vyote vya kutetea haki za wafanyakazi nchini i Burundi kwa CNDS kuunganisha pande mbili kuhusu swala la hatua ya serikali ya kusimamisha michango kuwa ilitolewa moja kwa moja kwenye mishahara ya wajumbe wa vyama hivyo.
Mashirikisho hayo mawili yanathibitisha kuwa hatua hiyo inazorotesha urasibu mzuri wa ofisi zao.
Mashirika hayo mawili yanatuhumu serikali kukiuka sheria kuhusiana na utekelezwaji wa makubaliano 87 ya OIT ( shirika la kimataifa kuhusu kazi) kuhusu uhuru wa kuunda chama cha wafanyakazi na kulinda haki ya kuunda chama cha wafanyakazi pamoja pia na makubaliano nambari 135 kuhusu kuwalinda wawakilishi wa wafanyakazi na kuwarahisishia.
Katika ziara za wajumbe wa serikali zilizofanyika kati ya januari na februari mwaka huu, waziri mkuu Gervais Ndirakobuca akiwa mkoani Makamba, alifahamisha kuwa hatua ya kutoa tozo ya michango moja kwa moja kwenye mishahara kwa ajili ya vyama vya wafanyakazi imesimamishwa.
Baadhi ya wafanyakazi walilaani kuona kuna kiwango cha pesa kilichokatwa kwenye mishahara kufadhili vyama vya ushirika ambapo sio wajumbe.
Kupitia mashtaka hayo yaliyowasilishwa tarehe 4 aprili 2023, shirikisho la vyama vya ushirika la COSYBU na CSB, hawajapinga kuwepo kwa visa vya aina hiyo lakini wanaitumu serikali kuharakisha kuchukuwa hatua ya kusitisha tozo hilo badala ya kujadili na wawakilishi wa vyama vya ushirika ili kuonyesha majukumu ya kila upande.
Mashirika hayo yanaomba mazungumzo yafanyike kumaliza mara mwisho swala kuhusu haki ya kujiunga na chama cha ushirika utekelezwaje.
You might also like
Kielezo cha RSF 2026: Burundi yafanya maendeleo katikati ya kurudi nyuma kwa uhuru wa kihistoria wa vyombo vya habari
SOS Médias Burundi Bujumbura, Mei 1, 2026 – Burundi inashika nafasi ya 119 kati ya nchi 180 katika Fahirisi ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ya 2026 iliyochapishwa Alhamisi
Burundi: utawala wa rais Ndayishimiye unafanya mauwaji kama ule wa mtangulizi wake Nkurunziza
Shirika la kutetea haki za binadamu la Iteka linatoa tahadhari . Katika ripoti yake ya mwisho, shirika hilo la zamani kabisa la kutetea haki za binadamu nchini Burundi limetoa orodha
Rwanda: wakimbizi wa Kitutsi wa Kongo waandamana kupinga mauaji ya kimbari yanayowalenga nchini DRC
Walikuwa ni wakimbizi kutoka kambi za Kiziba na Nkamira zilizoko katika wilaya za Karongi na Rubavu za Mkoa wa Magharibi ambao waliandamana siku ya Jumatatu. Wanashutumu “mauaji ya halaiki” yaliyofanywa
