Burundi : shirikisho la vyama viwili vya kutetea haki za wafanyakazi vinaomba CNDS kuingilia kati katika mzozo dhidi ya serikali

Burundi : shirikisho la vyama viwili vya kutetea haki za wafanyakazi vinaomba CNDS kuingilia kati katika mzozo dhidi ya serikali

Mashirikisho ya vyama vya wafanyakazi COSYBU na CSB vinapaza sauti dhidi ya kusimamishwa kwa tozo za michango ya wajumbe wao. Serikali iliweka hatua ya kupiga marufuku michango ya wajumbe wa vyama vya wafanyakazi kuchukuliwa moja kwa moja kwenye mishahara yao. Mashirika hayo mawili yanaomba upatanishi wa kamati ya kitaifa ya mjadala wa kijamii (CNDS) ufanyike kuhusu swala hilo. HABARI SOS Médias Burundi

Kupitia malalamiko dhidi ya serikali ya Burundi yaliyowasilishwa kwa mkuu wa kamati ya kitaifa ya mjadala wa kijamii, shirikisho la vyama vya wafanyakazi COSYBU na CSB vinatoa wito, kwa niaba ya vyama vyote vya kutetea haki za wafanyakazi nchini i Burundi kwa CNDS kuunganisha pande mbili kuhusu swala la hatua ya serikali ya kusimamisha michango kuwa ilitolewa moja kwa moja kwenye mishahara ya wajumbe wa vyama hivyo.

Mashirikisho hayo mawili yanathibitisha kuwa hatua hiyo inazorotesha urasibu mzuri wa ofisi zao.

Mashirika hayo mawili yanatuhumu serikali kukiuka sheria kuhusiana na utekelezwaji wa makubaliano 87 ya OIT ( shirika la kimataifa kuhusu kazi) kuhusu uhuru wa kuunda chama cha wafanyakazi na kulinda haki ya kuunda chama cha wafanyakazi pamoja pia na makubaliano nambari 135 kuhusu kuwalinda wawakilishi wa wafanyakazi na kuwarahisishia.

Katika ziara za wajumbe wa serikali zilizofanyika kati ya januari na februari mwaka huu, waziri mkuu Gervais Ndirakobuca akiwa mkoani Makamba, alifahamisha kuwa hatua ya kutoa tozo ya michango moja kwa moja kwenye mishahara kwa ajili ya vyama vya wafanyakazi imesimamishwa.

Baadhi ya wafanyakazi walilaani kuona kuna kiwango cha pesa kilichokatwa kwenye mishahara kufadhili vyama vya ushirika ambapo sio wajumbe.

Kupitia mashtaka hayo yaliyowasilishwa tarehe 4 aprili 2023, shirikisho la vyama vya ushirika la COSYBU na CSB, hawajapinga kuwepo kwa visa vya aina hiyo lakini wanaitumu serikali kuharakisha kuchukuwa hatua ya kusitisha tozo hilo badala ya kujadili na wawakilishi wa vyama vya ushirika ili kuonyesha majukumu ya kila upande.

Mashirika hayo yanaomba mazungumzo yafanyike kumaliza mara mwisho swala kuhusu haki ya kujiunga na chama cha ushirika utekelezwaje.

Previous Goma: mahakama ya kijeshi yaahirisha kesi ya kigogo wa Lucha
Next DRC : sheria kuhusu uhuru wa vyombo vya habari inataraji kutangazwa

About author

You might also like

Jamii

Burundi: wafanyakazi hawawezi kukidhi mahitaji yao ya kimsingi kulingana na mashirikisho mawili ya vyama vya ndani

CSB (Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi wa Burundi) na COSYBU (Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi vya Burundi) wanasikitishwa na hali ya sasa ya kiuchumi na mapato ya kutosha miongoni

DRC Sw

DRC : sheria kuhusu uhuru wa vyombo vya habari inataraji kutangazwa

Waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari Patrick Muyaya alifanikisha azma yake jumanne hii mbele ya wabunge wa kitaifa. Mswada wake wa sheria kuhusu marekebisho ya sheria ya kiwaziri inayopanga

Utawala

Goma: mahakama ya kijeshi yaahirisha kesi ya kigogo wa Lucha

Kesi dhidi ya Mwamisyo Ndungo mwanaharakati ya vuguvugu la LUCHA ndani ya mkoa wa Kivu kaskazini iliotaraji kusikilizwa jumatano saa nne, iliahirishwa katika siku nyingine, korti ya kijeshi mkoani humo