Kivu-Kaskazini : zaidi ya wananchi 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja eneo la Beni

Kivu-Kaskazini : zaidi ya wananchi 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja eneo la Beni

Katika kitongoji cha Ruwenzori wilaya ya Beni mkoa wa Kivu-kaskazini (mashariki mwa DRC) , zaidi ya watu 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja. Takwimu hizo zinatolewa na ofisi ya uratibu wa mashirika ya kiraia ya Kongo. Idadi kubwa ya wahanga waliuwawa kwa mapanga na kundi la ADF (nguvu zilizoungana kwa ajili ya demokrasia). HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa Jade Vutsapu, muhudumu katika ofisi ya uratibu wa mashirika ya kiraia nchini Kongo, tangu usiku wa tarehe 9 machi hadi 09 aprili, ” waasi wa ADF waliwauwa watu 200 katika wilaya moja ya Beni huku kitongoji cha Bashi kikiorodhesha idadi kubwa “.

” Katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia usiku wa tarehe 8 kuamkia tarehe 09 aprili , tulihesabu zaidi ya watu 200 waliouwawa kwa mapanga na waasi wa ADF. Idadi kubwa waliuwawa katika kitongoji cha Bashu, ambapo idadi iliyoorodheshwa ni zaidi ya vifo 38 waliouwawa eneo la Mukondi na 8 walikufa eneo Mwasa katika kipindi cha siku moja, lakini pia eneo la Kirindera usiku wa tarehe 11 kuamkia 12 machi watu 20 waliuwawa. Eneo la Masabanda kuelekea Oicha waliuwawa watu 21 na kuna maeneo mengine ambapo mauwaji hayo yalifanyika. Tunakasirika kuona mauwaji hayo yakitekelezwa katika maeneo ambako kuna idadi kubwa ya wanajeshi “, alibaini mwanaharakati huyo.

Jade Vutsapu anatumai kuwa mauwaji hayo yanatekelezwa katika mpango wa mauwaji ya halaiki yanayolenga wananchi wa wilaya ya Beni.

Anaomba serikali kutathimini upya mkakati wake wa amani na usalama katika eneo hilo.

Previous Nyarugusu (Tanzania) : wakimbizi wawili kutoka Burundi wakufa kutokana na na maji ya mvua
Next Bujumbura : kongamano lisilokuwa la kawaida la chama cha CNL lasimamishwa kwa kosa "la tahajia"

About author

You might also like

DRC Sw

Minembwe: kukamatwa kwa kijana wa miaka sitini kufuatia kutoweka kwa ndege isiyo na rubani ya FARDC

Zachée Runezerwa (umri wa miaka 65) anazuiliwa katika kontena la jeshi la Kongo. Alikamatwa Oktoba 22 katika mtaa wa Runundu-Minembwe katika eneo la Fizi, katika jimbo la Kivu Kusini mashariki

DRC Sw

DRC: uasi mpya wa ndani ungeungana na M23

Jamii ya Walombi katika jimbo la Tshopo imetuma risala kwa gavana wa mkoa, ikielezea wasiwasi kuhusu uwezekano wa muungano kati ya kundi la waasi wa eneo hilo na March 23

Haki za binadamu

RDC (Ituri) : angalau wananchi 40 waliuwawa na waasi wa CODECO

Vijiji vitatu vya eneo la Banyali Kilo, wilayani Djugu katika mkoa wa Ituri mashariki mwa DRC vililengwa na mashambulizi ya wakati mmoja ya waasi wa CODECO (shirikisho kwa ajili ya