Bujumbura : kongamano lisilokuwa la kawaida la chama cha CNL lasimamishwa kwa kosa “la tahajia”
Kutokana na kosa katika kuandika barua inayotumwa kwa waziri wa mambo ya ndani, chama cha upinzani cha CNL kilizuiliwa kuandaa kongamano lake kuu lililokuwa limepangwa kufanyika mchana wa ijumaa tarehe 14 aprili. HABARI SOS Médias Burundi
Katibu mtendaji wa chama cha CNL anafahamisha kuwa ” tulipewa taarifa kupitia simu alhamisi usiku kuwa kongamano halitafanyika kwa sababu ya kosa la kimandishi ndani ya barua iliyotumwa kwa waziri wa mambo ya ndani”.
Tulivunjika moyo katika chama hiki cha upinzani ambacho mara nyingi hakiruhusiwi kutekeleza programu zake kama ilivyopangwa.
Simon Bizimungu katibu mtendaji wa chama hicho, anaomba waziri husika kushirikiana na vyama vya kisiasa na kutoa majibu kwa barua za vyama kwa wakati.
” Hali hiyo itasaidia kujiepusha na matatizo ya dakika ya mwisho” alieleza.
Tarehe 19 februari iliyopita, waziri wa Burundi wa mambo ya ndani Martin Niteretse alipiga marufuku sherehe za maadhimisho ya mwaka wa nne wa chama cha CNL akidai kuwa hali ya mvutano ndani ya chama hicho inaweza kuvuruga usalama katika mji mkuu wa kibiashara wa Bujumbura na kwenye barabara zinazounganisha mji huo na mikoa mbali mbali kabla ya badaye kuruhusu sherehe hizo kufanyika tarehe 12 machi.
Katika maeneo kadhaa, wafuasi wa CNL mara nyingi hunyanyaswa, kuuwawa na kuteswa lakini pia wanafungwa kinyume cha sheria. Wanaofanya vitendo hivyo, ni wafuasi wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD, wajumbe wa idara ya upelelezi, askali polisi pamoja pia na viongozi wa ndani na askali jeshi kwa kiwango kidogo kulingana na mashirika ya kutetea haki za binadamu na vyanzo vya SOS Médias Burundi.
Kwa mjibu wa Carina Tertsakian mtafiti mshirika wa IDHB ( Shirika la kutetea haki za binadamu nchini Burundi), kuna tofauti kubwa kati ya ahadi za rais Neva na vitendo kuhusu swala la kuheshimu haki za binadamu “.
You might also like
Gitega: Uhaba wa mbolea ya FOMI wazua hofu ya njaa katika Msimu wa Kilimo wa C
SOS Médias Burundi Gitega, Julai 28, 2026 – Wakulima katika mkoa wa Gitega, katikati mwa Burundi, wanatoa tahadhari kuhusu ukosefu wa mbolea ya FOMI (mbolea mchanganyiko wa kikaboni na madini
Burundi: Faustin Ndikumana alia njama baada ya silaha kupatikana katika kituo chake
SOS Médias Burundi Ngozi, Juni 5, 2026 – Ugunduzi wa silaha na zana za kijeshi katika taasisi ya mtetezi wa haki za binadamu Faustin Ndikumana unaendelea kuibua hisia kali nchini
Bujumbura: Mafua isiyo ya kawaida yanawasumbua Idadi ya watu
SOS Médias Burundi Bujumbura, Januari 19, 2026 – Kwa karibu mwezi mmoja, ugonjwa wenye dalili zisizo za kawaida umekuwa ukienea katika vitongoji kadhaa vya Bujumbura, na kusababisha wasiwasi na kuzua
