Bujumbura : kongamano lisilokuwa la kawaida la chama cha CNL lasimamishwa kwa kosa “la tahajia”

Bujumbura : kongamano lisilokuwa la kawaida la chama cha CNL lasimamishwa kwa kosa “la tahajia”

Kutokana na kosa katika kuandika barua inayotumwa kwa waziri wa mambo ya ndani, chama cha upinzani cha CNL kilizuiliwa kuandaa kongamano lake kuu lililokuwa limepangwa kufanyika mchana wa ijumaa tarehe 14 aprili. HABARI SOS Médias Burundi

Katibu mtendaji wa chama cha CNL anafahamisha kuwa ” tulipewa taarifa kupitia simu alhamisi usiku kuwa kongamano halitafanyika kwa sababu ya kosa la kimandishi ndani ya barua iliyotumwa kwa waziri wa mambo ya ndani”.

Tulivunjika moyo katika chama hiki cha upinzani ambacho mara nyingi hakiruhusiwi kutekeleza programu zake kama ilivyopangwa.

Simon Bizimungu katibu mtendaji wa chama hicho, anaomba waziri husika kushirikiana na vyama vya kisiasa na kutoa majibu kwa barua za vyama kwa wakati.

” Hali hiyo itasaidia kujiepusha na matatizo ya dakika ya mwisho” alieleza.

Tarehe 19 februari iliyopita, waziri wa Burundi wa mambo ya ndani Martin Niteretse alipiga marufuku sherehe za maadhimisho ya mwaka wa nne wa chama cha CNL akidai kuwa hali ya mvutano ndani ya chama hicho inaweza kuvuruga usalama katika mji mkuu wa kibiashara wa Bujumbura na kwenye barabara zinazounganisha mji huo na mikoa mbali mbali kabla ya badaye kuruhusu sherehe hizo kufanyika tarehe 12 machi.

Katika maeneo kadhaa, wafuasi wa CNL mara nyingi hunyanyaswa, kuuwawa na kuteswa lakini pia wanafungwa kinyume cha sheria. Wanaofanya vitendo hivyo, ni wafuasi wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD, wajumbe wa idara ya upelelezi, askali polisi pamoja pia na viongozi wa ndani na askali jeshi kwa kiwango kidogo kulingana na mashirika ya kutetea haki za binadamu na vyanzo vya SOS Médias Burundi.

Kwa mjibu wa Carina Tertsakian mtafiti mshirika wa IDHB ( Shirika la kutetea haki za binadamu nchini Burundi), kuna tofauti kubwa kati ya ahadi za rais Neva na vitendo kuhusu swala la kuheshimu haki za binadamu “.

Previous Kivu-Kaskazini : zaidi ya wananchi 200 waliuwawa katika kipindi cha mwezi mmoja eneo la Beni
Next RDC (Ituri) : angalau wananchi 40 waliuwawa na waasi wa CODECO

You might also like

Haki za binadamu

Gihanga: Mwanamume aliyetekwa nyara siku ya Jumanne bado hawezi kupatikana

Dieudonné Gahungu, baba mdogo wa mtoto mmoja, alitekwa nyara Jumanne saa sita mchana katika wilaya ya Gihanga katika mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi) na wanaume watatu, wawili kati yao

Utawala

Burundi: Waziri Mkuu atoa wito kwa matumizi ya ndani ili kuhifadhi fedha za kigeni

SOS Médias Burundi Bujumbura, Oktoba 8, 2025 — Ikikabiliwa na uhaba wa fedha za kigeni na kuendelea kushuka kwa thamani ya faranga ya Burundi, serikali ya Burundi inataka mabadiliko ya

Wakimbizi

Siku ya Kimataifa ya Wakimbizi: kati ya matumaini na kujiuzulu miongoni mwa wakimbizi wa Burundi

Tarehe 20 Juni kila mwaka, dunia huadhimisha Siku ya Wakimbizi. Fursa ya kuwafikiria na kutetea, kulinda na kuendeleza haki zao, kulingana na UNHCR. Kwa zaidi ya Warundi 300,000 ambao bado