Masisi: mapigano makali kati ya kikosi cha Burundi na kundi la M23
Mapigano makali ya kundi la M23 dhidi ya wanajeshi wa Burundi wa kikosi cha jumuiya ya Afrika mashariki yalifanyika siku ya ijumaa. Jeshi la Kongo linahakikisha kuwa zaidi ya wapiganaji 10 wa kundi la M23 waliuwawa na wengine kukamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Ni mchana wa ijumaa ambapo mapigano hayo yaliibuka. Yalifanyika eneo la Jérusalem katika kitongoji cha Malehe katika wilaya ya Masisi. Msemaji wa kikosi cha kikanda cha EAC alifahamisha katika tangazo siku ya ijumamosi kuwa mapigano yaliendelea hadi usiku na jumamosi asubuhi.
” Mapigano yaliibuka wakati wapiganaji wa M23 walitaka kudhibiti tena baadhi ya ngome walizoacha wiki kadhaa zilizopita. Wanajeshi wa Burundi wajumbe wa kikosi cha kikanda wanaohudumu eneo hilo, walipinga hilo”, yanaeleza mashirika ya kiraia eneo hilo.
Habari hizo zimethibitishwa na jeshi la Kongo katika mkoa wa Kivu kaskazini. Jeshi hilo linahakikisha kuwa angalau wapiganaji 10 waliuwawa, wengine walikamatwa pamoja na zana za kijeshi.
” Tunapongeza ushujaa wa wanajeshi wa Burundi walifungua moto kwa ajili ya kuwalinda wananchi dhidi ya uvamizi wa M23. Wananchi wanahitaji amani” , alibaini luteni kanali Guillaume Ndjike Kaiko msemaji wa gavana mwanajeshi wa mkoa wa Kivu kaskazini.
Mashirika ya kiraia ya ndani yanaripoti kuwa yaliona gari za kubeba wagonjwa sikifanya nenda rudi kwa ajili ya kuchukuwa maiti na majeruhi waliokuwa wamevalia sare za kijeshi , wengine nguo za kawaida ambao idadi yao na uraia bado kujulikana.
Hii ni mara ya kwanza kwa wanajeshi wa kikosi cha EAC kilichotumwa nchini DRC kupigana dhidi ya M23.
Upande wake, kundi la M23 halijasema chochote kuhusu mapigano hayo ya waasi wake dhidi ya wanajeshi wa Burundi.
Kulingana na makubaliano ya Luanda ( Angola) na Nairobi (Kenya) , kundi la M23 liliahidi kuacha ngome zake za zamani na kuzikabidhi kikosi cha EAC tangu disemba 2022.
Lakini katika baadhi ya maeneo, vyanzo vyetu vinasema kuwa kuna uvunjaji wa amri hiyo ya kusitisha vita inayoendelea. Burundi ina kikosi vitatu vilivyotumwa kwenye ardhi ya nchi hiyo kubwa jirani wa magharibi. Walitumwa katika mkoa wa Kivu ya kusini na Kivu kaskazini katika jukwa la ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili na chini ya mwamvuli wa jumuiya ya Afrika mashariki.
You might also like
DRC: Mamilioni ya raia wamenaswa, UN yatoa wito kwa AFC/M23
SOS Médias Burundi Goma, Machi 18, 2026 Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliwa na janga la kibinadamu linaloendelea, ambalo linaadhimishwa na vurugu za kutumia silaha, kuhama kwa watu
Cibitoke: wachimbaji dhahabu wawili wamekufa katika maporomoko ya ardhi
Wachimbaji wawili wa dhahabu walisombwa na maporomoko ya ardhi mnamo Jumatatu, Mei 13, kwenye kilima cha Myave katika eneo la Ndora katika wilaya ya Bukinanyana, mkoa wa Cibitoke, kaskazini-magharibi mwa
Kivu Kusini: Makubaliano ya Doha tayari Yamevunjwa na kurejeshwa haraka kwa uhasama
SOS Médias Burundi Bukavu, Novemba 17, 2025 – Chini ya siku mbili baada ya kutiwa saini huko Doha kwa makubaliano ya amani yaliyokusudiwa kufungua njia ya kuzuka mashariki mwa DRC,
