DRC : siku chache baada ya muhula wake kumalizika, kikosi cha EAC chaomba kuongezewa muda

DRC : siku chache baada ya muhula wake kumalizika, kikosi cha EAC chaomba kuongezewa muda

Kikosi cha kanda ya jumuiya ya Afrika mashariki EAC kilichotumwa katika mkoa wa kivu kaskazini (mashariki mwa DRC) kutokana na waasi wa M23 kudhibiti maeneo kadhaa, kinaomba kupewa muda wa ziada, hadi tarehe 8 septemba ijayo. HABARI SOS Médias Burundi

Ombi hilo lilitolewa na Aden Duale, katibu katika wizara ya ulinzi nchini Kenya.

” Tuliomba serikali ya DRC kujipanga kwa ajili ya kuongeza muhula wa kikosi cha kanda ya EAC hadi baada ya tarehe 8 septemba ili kudumisha matunda ya kikosi hicho cha kikanda “, alifahamisha mwishoni mwa wiki iliyopita.

Nchi wanachama wa EAC ziliamuru jumatano tarehe 31 mai wakati wa mkutano wa kilele wa 21 wa ma rais wa nchi za EAC kuongeza muhula wa kikosi cha EAC nchini DRC hadi 8 septemba 2023. Muhula huo ungemalizika alhamisi tarehe mosi juni.

Marais wawili, William Ruto wa Kenya na Evariste Ndayishimiye wa Burundi ambaye pia ni mwenyekiti wa jumuiya ya Afrika mashariki walihudhuria mkutano huo uliofanyika mjini Bujumbura, mji mkuu wa kiuchumi wa Burundi.

Kwa kipindi cha siku tatu, washiriki walifanya tathmini ya uwendeshaji wa operesheni za kikosi cha kanda ya EAC katika mkoa wa Kivu kaskazini.

” Mkutano huo uliamuru wakusanywe pamoja waasi wa kundi la M23 eneo la Rumangabo (Kivu kaskazini) chini ya uangalizi wa mjumbe wa kikosi cha kikanda na FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo). Mbali na hayo, uamzi wa kuondoka kwa kikosi cha EAC unaweza kuchukuliwa katika kikao cha makadirio ki nachopangwa kufanyika juni 15 ” yalisomeka katika tamko la kuhitimisha mkutano wa Bujumbura.

Wananchi wakaazi wa mkoa wa Kivu kaskazini na mashirika ya kiraia, wanaendelea kutofautiana kuhusu matokeo ya harakati za kikosi cha kanda ya EAC nchini DRC, mbali na kikosi cha wanajeshi wa Burundi kilichowekwa katika wilaya ya Masisi.

Previous Rugombo : watu wawili, mke na mumeo wapatikana wakiwa maiti nyumbani kwao
Next Gitega : watu saba wapewa adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja na miwili jela kwa kuhusika na ushoga

You might also like

Wakimbizi

Dzaleka (Malawi): ukosefu wa usalama, wasiwasi kwa kila mtu

Ripoti kutoka kwa uchunguzi wa UNHCR kuhusu sababu za kuongezeka kwa uhalifu katika kambi ya Dzaleka imetangazwa hadharani ndani ya kambi hiyo. Hati hiyo inapendekeza kwamba wahalifu lazima wapatikane na

Usalama

Rumonge – Mvua kubwa: Mto Kirasa unafurika, uharibifu mkubwa umerekodiwa kwenye kilima cha Gabirano

SOS Médias Burundi Rumonge, Aprili 17, 2025 – Mvua kubwa ilisababisha Mto Kirasa kufurika Jumatano hii mchana katika tarafa ya Muhuta, katika mkoa wa Rumonge (kusini-magharibi mwa Burundi). Maafa hayo

Usalama

Bujumbura: Wakongo wakamatwa kwa wingi, hofu yatanda katika mji mkuu

SOS Médias Burundi Bujumbura, Oktoba 4, 2025 – Hali ya hofu na kutokuwa na uhakika imetanda miongoni mwa jamii ya Wakongo wanaoishi Bujumbura, mji mkuu wa kiuchumi wa Burundi. Chanzo: