Rugombo : watu wawili, mke na mumeo wapatikana wakiwa maiti nyumbani kwao

Rugombo : watu wawili, mke na mumeo wapatikana wakiwa maiti nyumbani kwao

Tharcisse Nsanzamahoro (miaka 49) na mke wake Thérèse Nzohabonimama, miaka 52 walipatikana wakiwa maiti nyumbani kwao jumapili hii asubuhi kwenye transversale 3 tarafani Rugombo katika mkoa wa Cibitoke (kaskazini magharibi mwa Burundi). Familia ya wahanga hao inaomba waliohusika na mauwaji hayo watafutwe na wakamatwe. Mkuu wa tarafa anathibitisha habari hizo na kuzidi kuwa uchunguzi tayari umeanzishwa. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mujibu wa ushahidi iliyotolewa na jirani, wawili hao ambao walikuwa na watoto nane, walichangia vinywaji na marafiki siku moja kabla katika mgahawa.

Wapendanao hao waliotuhumiwa uchawi kwa kipindi kirefu, huenda walitumia kinywaji chenye sumu .

” Huenda kuna mtu aliyetaka kulipiza kisasi, sababu watu hao waliofariki walisotwa kidole mara nyingi na kuhusishwa katika visa vya uchawi ambavyo vilisababishwa vifo vingi”, alisisitiza jirani huyo.

Kulingana na chanzo cha usalama, uchunguzi unaoendelea umepelekea watu watatu kukamatwa. Kwa sasa wanahojiwa na kuzuiliwa katika gereza la tarafa ya Rugombo.

Watu wa karibu na wahanga wanalaani ” mauwaji hayo ya watu wawili wasiokuwa na hatia ” na kuomba vipimo vifanyike ili kutambua kilichosababisha vifo vya watu hao.

Mkuu wa tarafa ya Rugombo anathibitisha taarifa hizo na kuzidi kuwa uchunguzi wa kina unaendelea ili kukamata waliohusika.

Gilbert Manirakiza anaomba wananchi kushirikiana na polisi na vyombo vya sheria wakati huu wa uchunguzi na kujizuia na mwenendo wa kujichukulia sheria mikononi.

Previous Musigati : amri ya kung'oa heka 50 za mashamba ya miwa
Next DRC : siku chache baada ya muhula wake kumalizika, kikosi cha EAC chaomba kuongezewa muda

You might also like

Usalama

Gitega: mtu aliyekufa katika mazingira yasiyojulikana

Mwili wa Fabrice Nimpagaritse, 22, ulipatikana Jumatatu Julai 15 ukining’inia juu ya mti. Ugunduzi wa macabre ambao SOS Médias Burundi ilijifunza Alhamisi hii ulifanyika katika wilaya ya Yoba katika mji

Usalama

Kirundo: Wakaazi wanashutumu michango ya kulazimishwa kwa ukumbusho wa Nkurunziza chini ya shinikizo kutoka kwa Imbonerakure

SOS Médias Burundi Kirundo, Mei 28, 2026 – Siku chache tu kabla ya sherehe rasmi zilizopangwa kufanyika Juni 8, 2026, huko Gitega, mji mkuu wa kisiasa wa Burundi ambako mkuu

Diplomasia

Gitega: Nyuma ya matamshi, kashfa inayoendelea ya migogoro ya madini katika eneo la Maziwa Makuu barani Afrika.

SOS Médias Burundi Gitega, Aprili 21, 2026 – Wakiwa wamekusanyika Gitega, washikadau katika sekta ya madini katika eneo la Maziwa Makuu barani Afrika walielezea nia yao ya kuvuka migogoro ya