Musigati : amri ya kung’oa heka 50 za mashamba ya miwa

Musigati : amri ya kung’oa heka 50 za mashamba ya miwa

Mkuu wa tarafa alichukuwa uamzi wa kupiga marufuku miwa katika bonde la tarafa ya Musigati mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). Zao hilo litatoa nafasi kwa mazao mengine ya vyakula, kwa mujibu wa viongozi wa mkoa. Wamiliki wa mashamba ya miwa wanasema kuwa wamevunjika moyo. HABARI SOS Médias Burundi

Mkuu wa tarafa anaeleza kuwa anataka kukabiliana na njaa ambayo inakabili familia mkoani Bubanza.

” Ni kuondoa mashamba yote ya miwa ndani ya bonde la Musigati na kupanda eneo hilo mahindi, maharagwe, na mimea mingine ya mabondeni “, alibaini gavana wa mkoa wa Bubanza katika mkutano tarafani Musigati.

Hakika ni heka 50 za mashamba ya miwa zinazohusishwa. Na hatua hiyo ilianza kutekelezwa tangu ilipotangazwa, kwa mujibu wa wakaazi.

” Uongozi wa tarafa uliwaalika Imbonerakure ( wajumbe wa tawi la vijana wafuasi wa chama cha CNDD-FDD) kutekeleza uamzi huo. Walilata , kung’oa na kuharibu mashamba ya miwa katika mto wa Nyamugerera , waliripoti mashahidi.

Na katibu wa chama cha CNDD-FDD alishindilia.

” Hawaelewi kuwa muwa unaleta mavuno mara moja kwa mwaka. Mazao mengine yanaleta mavuno angalau mara mbili. Kwanza pesa inayotokana na zao hilo huchangia katika kitendo cha kuparika. Uamzi huu hawutabadilika ” alibaini Alexandre Ngoragoze.

Fundi wa kilimo tarafani Musigati anasema zao hilo lililopewa jina moja na tarafa hiyo katika lugha ya taifa ( Umusigati =muwa ) litapelekwa katika maeneo mengine na ambako kuna maji.

Wakaazi wanadai kuwa ni hatua ambayo hawakufikiria. Wanasema zao la miwa lilikuwa na faida : Shamba la miwa la ukubwa wa mita mraba 20 , linaweza kuingiza kitita cha 350.000 zikiwa ndogo. Kitita hicho kinatocha ili kuanzisha biashara ndogo yenye faida kwa familia na katika uchumi wa tarafa “, wanadai wakulima.

Previous Burundi : Imbonerakure zapewa sifa na kuhitajiwa
Next Rugombo : watu wawili, mke na mumeo wapatikana wakiwa maiti nyumbani kwao

You might also like

Uchumi

Gitega: bei imekuwa ngumu kumudu

Familia kadhaa katika mji wa Gitega (mji mkuu wa kisiasa) haziwezi kuhudhuria soko la Krismasi na Mwaka Mpya. Bidhaa zote zimeona ongezeko la bei kupita kiasi, na kuwaacha wakaazi wasiweze

Jamii

Burunga: kampeni ya uvunaji wa mahindi Inakabiliwa na kutokuamini kwa mkulima

SOS Médias Burundi Burunga, Julai 22, 2025 – Katikati ya kampeni ya mavuno ya mahindi, Wakala wa Kitaifa wa Kusimamia Hifadhi ya Kimkakati ya Chakula (ANAGESSA) inakabiliwa na upinzani mkali

Uchumi

Bujumbura: bei ya tikiti ya basi imeongezeka mara tatu kaskazini mwa ukumbi wa jiji

Wasafirishaji wanaendelea kukisia bei ya tikiti za usafiri katika sehemu ya kaskazini ya mji mkuu wa kiuchumi Bujumbura. Kwa kawaida, bei ya tikiti ya usafiri kwenye sehemu ya katikati ya