DRC (Uvira) wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi wakamatwa kwa jaribio la mauwaji
Wakimbizi wenye asili ya Burundi katika kambi ya muda ya Kavimvira mjini Uvira katika mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa DRC walikamatwa kwa tuhuma za jaribio la mauwaji. Mmoja anafuatiliwa kwa jaribio la kumuuwa mvuvi mmoja wakati wa pili akiwa alijaribu kumumalizia maisha mlinzi wa kambi. Wawili hao raia wa Burundi wanazuiliwa ndani ya gereza la polisi mjini Uvira. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na Kiza Tiniko, kiongozi wa vijana eneo la Kavimvira, wakimbizi hao wawili walikamatwa jumatatu tarehe 11 septemba 2023.
” Kijana mkimbizi mwenye uraia wa Burundi kwa jina la Mugisha Justin mkaazi wa kambi ya Kavimvira alijaribu kumumalizia maisha kijana mvuvi mwenye uraia wa Kongo kwa jina la Matabishi Saleh ilikuwa majira ya saa 6 na dakika 15 katika kata ya Kavimvira barabara ya Lac. Vijana wakaazi wa kata hiyo waliingilia kati [….], alisema.
Kwa mjibu wake, kisu ambacho mkimbizi huyo wa Burundi alitaka kutumia kilikamatwa .
Mkimbizi mwingine anazuiliwa jela kwa tuhuma za jaribio ya kumuuwa mlinzi wa kambi ya muda ya Kavimvira.
Habari hizo zinathibishwa na mfanyakazi wa tume ya kitaifa kwa ajili ya wakimbizi mjini Uvira. Anahakikisha kuwa uchunguzi ulianzishwa na polisi eneo hilo.
Kambi ya muda ya Kavimvira inawapa hifadhi zaidi ya watu 3000 wenye asili ya Burundi.
You might also like
Cibitoke: wimbi kubwa la wakimbizi wa Kongo, zaidi ya watu 47,000 walipokea haraka
Katika muda wa chini ya wiki mbili, mkoa wa Cibitoke lilishuhudia ongezeko la wakimbizi wa Kongo 50,000 waliokimbia ghasia nchini mwao. Uhamisho huu mkubwa, unaojumuisha hasa wanawake na watoto, unaleta
Rutana: shida ya kiafya inayotia wasiwasi katika eneo la wakimbizi la Giharo
Eneo la wakimbizi la Giharo, lililo katika jimbo la Rutana, kusini mashariki mwa Burundi, liko katika hali ngumu ya kiafya. Kituo cha afya cha eneo hilo, muhimu kwa idadi hii
Nyarugusu (Tanzania): wakimbizi watatu wa Burundi walikufa katika ajali ya barabarani
Mkasa huo umetokea Ijumaa hii.Wakimbizi wanadai udhibiti mkali wa polisi katika utoaji wa leseni za kuendesha gari, haswa kwa waendesha pikipiki. HABARI SOS Media Burundi Ajali hiyo ilitokea katika eneo
