DRC (Uvira) wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi wakamatwa kwa jaribio la mauwaji
Wakimbizi wenye asili ya Burundi katika kambi ya muda ya Kavimvira mjini Uvira katika mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa DRC walikamatwa kwa tuhuma za jaribio la mauwaji. Mmoja anafuatiliwa kwa jaribio la kumuuwa mvuvi mmoja wakati wa pili akiwa alijaribu kumumalizia maisha mlinzi wa kambi. Wawili hao raia wa Burundi wanazuiliwa ndani ya gereza la polisi mjini Uvira. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na Kiza Tiniko, kiongozi wa vijana eneo la Kavimvira, wakimbizi hao wawili walikamatwa jumatatu tarehe 11 septemba 2023.
” Kijana mkimbizi mwenye uraia wa Burundi kwa jina la Mugisha Justin mkaazi wa kambi ya Kavimvira alijaribu kumumalizia maisha kijana mvuvi mwenye uraia wa Kongo kwa jina la Matabishi Saleh ilikuwa majira ya saa 6 na dakika 15 katika kata ya Kavimvira barabara ya Lac. Vijana wakaazi wa kata hiyo waliingilia kati [….], alisema.
Kwa mjibu wake, kisu ambacho mkimbizi huyo wa Burundi alitaka kutumia kilikamatwa .
Mkimbizi mwingine anazuiliwa jela kwa tuhuma za jaribio ya kumuuwa mlinzi wa kambi ya muda ya Kavimvira.
Habari hizo zinathibishwa na mfanyakazi wa tume ya kitaifa kwa ajili ya wakimbizi mjini Uvira. Anahakikisha kuwa uchunguzi ulianzishwa na polisi eneo hilo.
Kambi ya muda ya Kavimvira inawapa hifadhi zaidi ya watu 3000 wenye asili ya Burundi.
You might also like
Mahama (Rwanda): jamii ya Kongo iliadhimisha “mauaji ya halaiki” yaliyofanywa dhidi ya “Watutsi”
Wakimbizi wa Kongo nchini Rwanda walikumbuka Alhamisi hii mauaji ambayo yamefanywa dhidi ya jamii yao ya “Watutsi” kwa zaidi ya miaka 20. Wanazungumzia “mauaji ya kimbari” yaliyofanywa dhidi ya “Banyamulenge”
Giharo: Mvua kubwa husababisha uharibifu mkubwa katika eneo la wakimbizi wa Kongo huko Musenyi
SOS Médias Burundi Giharo, Aprili 13, 2025 – Mvua kubwa ilinyesha Jumapili hii asubuhi kwenye eneo la wakimbizi la Musenyi, katika tarafa ya Giharo (mkoa wa Rutana – kusini mashariki
Musenyi: Wakimbizi wa Kongo wakiwa katika dhiki huku kukiwa na wimbi la wizi wa usiku
Musenyi, Septemba 1, 2025 – Kusini mwa Burundi, katika kambi ya wakimbizi ya Musenyi, ukosefu wa usalama unazidi kuwa mbaya. Wakimbizi wa Kongo, waliokimbia ghasia mashariki mwa DRC, sasa wanakabiliwa
