Burundi : bei ya tiketi ya usafiri yapanda

Burundi : bei ya tiketi ya usafiri yapanda

Waziri wa biashara alitangaza jumatano hii bei mpya na nauli ya usafiri ndani ya mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura na katika ya mikoa. Bei ya tiketi ndani basi mjini Bujumbura popote pale unapotoka na kuelekea kati kati mwa mji ilipandishwa franka 50 sarafu za Burundi. Kati kati mwa nchi nauli itapanda kwa franka 500. HABARI SOS Médias Burundi

Waziri Marie Chantal Nijimbere alifahamisha kupitia tangazo kuwa bei ya nauli za usafiri ilipandishwa kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta ya gari tangu jumatatu hii.

Wakaazi wa jiji la Bujumbura walibaini kuwa walitaraji ongezeko hilo la bei ya tiketi litatokea.

” Bila shaka na bei ya vyakula na bidhaa zingine mahitajio muhimu zitapanda”. wanalaani wakaazi wengine ambao wanazidi kuwa walitupiliwa “.

Wengine wanasema kuwa hawaelewi malengo ya serikali. Wafanyakazi wa umma wanasema kuwa serikali inalenga kukusanya pesa iliyotumia katika kutekeleza sera ya kusawazisha mishahara iliyoanza kutelelezwa tangu julai iliyopita”.

” Bei ya bidhaa muhimu itapanda pia kwa mkondo huo”, wanalaani wafanyakazi wa serikali.

Bei ya tiketi ya usafiri ilipanda mara ya mwisho katika mwezi julai iliyopita.

Hatua hiyo ilisababisha bei ya bidhaa zingine kama sukari, simenti na vinywaji kupanda licha ya kuendelea kuadimika kwenye soko nchini Burundi.

Previous DRC (Uvira) wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi wakamatwa kwa jaribio la mauwaji
Next Gihanga : bibi kizee wa zaidi ya miaka sabini auwawa

You might also like

Uchumi

Burundi: Uhaba wa mafuta na faini za rekodi zalemaza mtandao mzima wa usafirishaji

SOS Médias Burundi Bujumbura, Julai 29, 2025 – Kupooza kabisa kwa usafiri wa umma kumekumba taifa hilo dogo la Afrika Mashariki. Tangu Jumapili na Jumatatu nzima, maeneo ya kuegesha magari

Uchumi

Burundi: mtandao wa mafuta bila mafuta

Raia wa Burundi wanalazimika kununua mafuta mtandaoni. Ombi hilo lilitekelezwa na Société Pétrolière du Burundi (SOPEBU) tangu mwisho wa Septemba iliyopita. Lakini, cha kushangaza, mafuta haya bado hayapatikani kwenye soko

Utawala

Bujumbura: tatizo la usafiri bado halijatatulika

Wakazi wa wilaya tofauti za mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura wanazoea kuzunguka kwa miguu na kwa sababu nzuri, usafiri wa umma unazidi kuwaumiza kichwa. Hali inazidi kuwa mbaya siku