Burundi : bei ya tiketi ya usafiri yapanda
Waziri wa biashara alitangaza jumatano hii bei mpya na nauli ya usafiri ndani ya mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura na katika ya mikoa. Bei ya tiketi ndani basi mjini Bujumbura popote pale unapotoka na kuelekea kati kati mwa mji ilipandishwa franka 50 sarafu za Burundi. Kati kati mwa nchi nauli itapanda kwa franka 500. HABARI SOS Médias Burundi
Waziri Marie Chantal Nijimbere alifahamisha kupitia tangazo kuwa bei ya nauli za usafiri ilipandishwa kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta ya gari tangu jumatatu hii.
Wakaazi wa jiji la Bujumbura walibaini kuwa walitaraji ongezeko hilo la bei ya tiketi litatokea.
” Bila shaka na bei ya vyakula na bidhaa zingine mahitajio muhimu zitapanda”. wanalaani wakaazi wengine ambao wanazidi kuwa walitupiliwa “.
Wengine wanasema kuwa hawaelewi malengo ya serikali. Wafanyakazi wa umma wanasema kuwa serikali inalenga kukusanya pesa iliyotumia katika kutekeleza sera ya kusawazisha mishahara iliyoanza kutelelezwa tangu julai iliyopita”.
” Bei ya bidhaa muhimu itapanda pia kwa mkondo huo”, wanalaani wafanyakazi wa serikali.
Bei ya tiketi ya usafiri ilipanda mara ya mwisho katika mwezi julai iliyopita.
Hatua hiyo ilisababisha bei ya bidhaa zingine kama sukari, simenti na vinywaji kupanda licha ya kuendelea kuadimika kwenye soko nchini Burundi.
You might also like
Kashfa ya mbolea nchini Burundi: mabilioni yadaiwa, wajibu wasio wazi, na wakulima washikiliwa mateka
SOS Médias Burundi Bujumbura, Januari 2, 2026 – Tangu mwisho wa Desemba 2025, kashfa yenye athari kubwa za kifedha na kisiasa imetikisa sekta ya kilimo ya Burundi. Mgogoro wa kuwania
Kodi ya angani katika miji mikuu ya Burundi: mgogoro wa kimya kimya unaozinyonga kaya
SOS Médias Burundi Bujumbura, Aprili 29, 2025 – Tangu mwaka jana, ukodishaji wa nyumba katika miji mikuu ya Burundi, ikiwa ni pamoja na Bujumbura, Gitega, na Ngozi, umeongezeka, wakati mwingine
Bujumbura: Faustin Ndikumana atoa wito wa uhuru wa Benki ya Jamhuri ya Burundi
SOS Médias Burundi Bujumbura, Julai 27, 2025 – Mkuu wa shirika la Paroles et Actions pour le Réveil de la Conscience et des Mentalités (PARCEM), Faustin Ndikumana, alizindua rufaa ya
