Gihanga : bibi kizee wa zaidi ya miaka sabini auwawa
Mwanamke mwenye wa miaka 75 alikatwa kichwa na watu wasiojulikana bado katika kijiji cha Rugunga tarafa ya Gihanga mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). Polisi tayari iliwakamata watuhumiwa watatu. HABARI SOS Medias Burundi
Janga hilo lilitokea usiku wa jumanne tarehe 12 kuamkia jumatano 13 septemba katika kijiji cha Rugunga. Jacqueline Nahishakiye mwenye umri wa miaka 75 aliuwawa akiwa nyumbani kwake.
” Maiti yake ilikuwa ikilala ndani ya damu huku kichwa kikiwa kilikatwa kwa kutumia panga”, alitoa ushahidi huo jirani.
Mkuu wa kijiji cha Rugunga, Célestin Rivugo akizungumzia na SOS Médias Burundi alithibitisha habari hizo na kuzidi kusema kuwa mauwaji hayo yalisababishwa na mizozo ya ardhi.
Kifo chake kilitokea siku moja baada ya kuzuru ardhi anazomiliki.
Uvumi mwingi unahusisha baadhi ya wajumbe wa familia yake kama watu walioandaa mauwaji hayo.
Ndugu wa muhanga ambaye walikuwa hawaelewani kwa muda mrefu kulingana na mashahidi katika kijiji cha Rugunga kwa sasa anazuiliwa katika gereza la tarafa ya Gihanga.
Watu wa karibu na muhanga wanaomba wapelekwe mahakama haraka waliohusika na mauwaji hayo.
You might also like
Goma : miili ya watu zaidi ya arobaini yazikwa kwa amri ya serikali licha ya upinzani wa familia na mashirika ya kirai
Angalau miili ya watu 40 ilizikwa jumatatu hii tarehe 18 septemba 2023 kwa amri ya gavana wa mkoa wa kivu kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo licha ya
Cibitoke: Wanawake wanakemea kasi ndogo ya utoaji haki katika migogoro ya ardhi
SOS Médias Burundi Cibitoke, Julai 9, 2025 – Katika eneo hili la kaskazini-magharibi mwa Burundi, wanawake wanazungumza dhidi ya kile wanachoelezea kama “ucheleweshaji usio na sababu” katika kushughulikia kesi za
Giheta: msichana mdogo mjamzito auawa
Esther Irakoze (umri wa miaka 20) aliuawa Alhamisi iliyopita kwenye kilima cha Rutegama katika wilaya ya Giheta, mkoa wa Gitega, katikati mwa Burundi. Washukiwa watatu walikamatwa kama sehemu ya uchunguzi
