Gihanga : bibi kizee wa zaidi ya miaka sabini auwawa
Mwanamke mwenye wa miaka 75 alikatwa kichwa na watu wasiojulikana bado katika kijiji cha Rugunga tarafa ya Gihanga mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). Polisi tayari iliwakamata watuhumiwa watatu. HABARI SOS Medias Burundi
Janga hilo lilitokea usiku wa jumanne tarehe 12 kuamkia jumatano 13 septemba katika kijiji cha Rugunga. Jacqueline Nahishakiye mwenye umri wa miaka 75 aliuwawa akiwa nyumbani kwake.
” Maiti yake ilikuwa ikilala ndani ya damu huku kichwa kikiwa kilikatwa kwa kutumia panga”, alitoa ushahidi huo jirani.
Mkuu wa kijiji cha Rugunga, Célestin Rivugo akizungumzia na SOS Médias Burundi alithibitisha habari hizo na kuzidi kusema kuwa mauwaji hayo yalisababishwa na mizozo ya ardhi.
Kifo chake kilitokea siku moja baada ya kuzuru ardhi anazomiliki.
Uvumi mwingi unahusisha baadhi ya wajumbe wa familia yake kama watu walioandaa mauwaji hayo.
Ndugu wa muhanga ambaye walikuwa hawaelewani kwa muda mrefu kulingana na mashahidi katika kijiji cha Rugunga kwa sasa anazuiliwa katika gereza la tarafa ya Gihanga.
Watu wa karibu na muhanga wanaomba wapelekwe mahakama haraka waliohusika na mauwaji hayo.
You might also like
DRC (Beni) : watu zaidi ya kumi wauwaw a katika shambulio jingine la kundi la ADF eneo la Rwenzori
Watu 13 waliuwawa katika shambulio jingine ya waasi wa AFD (nguvu zilizoungana kwa ajili ya demokrasia) katika usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa . Shambulio hilo lilifanyika katika kitongoji cha Bukokoma
Tahadhari ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa: karibu watu 20 wang’atwa na mbwa waliopotea katika muda wa chini ya wiki moja katika wilaya za Gitanga, Mabanda na Rutana.
SOS Media Burundi Rutana-Makamba, Aprili 8, 2025 – Wiki iliyopita ilikumbwa na mfululizo wa mashambulizi ya mbwa kichaa katika wilaya za Gitanga, Mabanda na Rutana kusini mashariki mwa Burundi, ambapo
Burundi: kundi la waasi la Red-Tabara lashitakiwa kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu
Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma ya Jamhuri ya Burundi ilitangaza kuwa imefungua kesi mbili za jinai kwa mashambulizi ya Gatumba (Bujumbura) na Buringa (Bubanza) ambayo yaliua karibu watu thelathini,
