Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo

Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo

Janga la kibinadamu linaendelea kutokea katika mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC, lilitahadharisha shirika la MSF la waganga wasiokuwa na mipaka. Shirika hilo la waganga la kimataifa linatoa mwito kwa jamii ya kimataifa na viongozi wa Kongo kuongeza juhudi katika kukidhi mahitaji ya wananchi walioathiriwa na mapigano ya silaha. HABARI SOS Médias Burundi

Takriban watu milioni moja walikimbia mapigano baada ya kuibuka kwa kundi la silaha la M23 eneo la Kivu kaskazini katika kipindi cha mwaka ulioyopita. Misaada hadi sasa haitoshi kulingana na MSF.

Watu madhaifu wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi yakiwemo maradhi ya kipindupindu, ukomaa , utapia mloo na kunyanyaswa kijinsia.

” Mzozo wa Kivu kaskazini umekuwa na madhara makubwa kutokana na ukubwa wake lakini pia misaada imekuwa ikichelewa katika maeneo mengi”, alifahamisha Avril Benoît, kiongozi mtendaji wa MSF-USA ambaye kwa sasa yuko mjini Goma.

” Kuna uhaba mkubwa wa misaada ili kukidhi mahitaji ya msingi ya wananchi kuhusiana na makaazi, madawa, vyakula na maji safi. Tunashuhudia kuwa madhara katika afya yao ni makubwa na yanaendelea kuongezeka, alizidi kusema.

Katika miezi ya hivi karibuni, ma mia ya ma elfu ya wananchi walitoroka makaazi yao na vijiji vyao na kwenda kuishi katika familia zilizowapokea na ndani ya vituo visivyokuwa rasmi. Pembeni ya Goma makaazi yaliyotengenezwa kwa kutumia hema za plastiki au vyandarua yamejaa huku watu wengine wakihifadhiwa ndani ya majengo ya kanisa na shule.

Wajumbe wa MSF wanahudumu katika vituo vya wakimbizi pembeni ya mji wa Goma tangu 2022 kwa kuwapa madawa bila kuwalipisha, gari za shirika hilo liliwapelekea maji safi na kuwajengea vyoo na baafu.

Mapigano yanaendelea kuripotiwa katika maeneo tofauti ya Kivu kaskazini na kuzidi kusababisha idadi kubwa ya wananchi kutimka

Previous Uvira : zaidi ya watu wengine 300 kutoka Burundi wakimbilia nchini DRC
Next Gatumba : mafuriko yalazimisha familia nyingi kukimbia

You might also like

DRC Sw

Busuma: Majaribio ya kurejea Kongo, wakimbizi wa Kongo wakamatwa na kurejeshwa kwa nguvu kambini

SOS Médias Burundi Ruyigi, Januari 28, 2026 — Katika siku za hivi majuzi, wakimbizi kadhaa Wakongo kutoka kambi ya Busuma, iliyoko katika wilaya ya Ruyigi, jimbo la Buhumuza, mashariki mwa

Wakimbizi

Burundi-Tanzania: Wakimbizi walazimishwa kurejeshwa makwao kwa shinikizo, Dola Milioni 82 bado hazijapatikana

SOS Médias Burundi Bujumbura, Machi 5, 2026 — Burundi imewasilisha mpango kabambe wa kuwezesha kurejea na kuunganishwa tena kwa wakimbizi, hasa kutoka Tanzania. Tangu mgogoro wa 2015, zaidi ya wakimbizi

Justice En

Jenerali Alain Guillaume Bunyoni kati ya maisha na kifo huko Gitega

SOS Médias Burundi Gitega, Oktoba 13, 2025 — Amelazwa hospitalini tangu Alhamisi, Oktoba 9, 2025, katika Hospitali ya Mkoa ya Gitega katika mji mkuu wa kisiasa wa Burundi, Waziri Mkuu