Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo

Kivu-kaskazini : MSF yatahadharisha kuhusu janga la kibinadamu kutokea eneo la mashariki mwa DRC kutokana na usalama mdogo

Janga la kibinadamu linaendelea kutokea katika mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC, lilitahadharisha shirika la MSF la waganga wasiokuwa na mipaka. Shirika hilo la waganga la kimataifa linatoa mwito kwa jamii ya kimataifa na viongozi wa Kongo kuongeza juhudi katika kukidhi mahitaji ya wananchi walioathiriwa na mapigano ya silaha. HABARI SOS Médias Burundi

Takriban watu milioni moja walikimbia mapigano baada ya kuibuka kwa kundi la silaha la M23 eneo la Kivu kaskazini katika kipindi cha mwaka ulioyopita. Misaada hadi sasa haitoshi kulingana na MSF.

Watu madhaifu wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi yakiwemo maradhi ya kipindupindu, ukomaa , utapia mloo na kunyanyaswa kijinsia.

” Mzozo wa Kivu kaskazini umekuwa na madhara makubwa kutokana na ukubwa wake lakini pia misaada imekuwa ikichelewa katika maeneo mengi”, alifahamisha Avril Benoît, kiongozi mtendaji wa MSF-USA ambaye kwa sasa yuko mjini Goma.

” Kuna uhaba mkubwa wa misaada ili kukidhi mahitaji ya msingi ya wananchi kuhusiana na makaazi, madawa, vyakula na maji safi. Tunashuhudia kuwa madhara katika afya yao ni makubwa na yanaendelea kuongezeka, alizidi kusema.

Katika miezi ya hivi karibuni, ma mia ya ma elfu ya wananchi walitoroka makaazi yao na vijiji vyao na kwenda kuishi katika familia zilizowapokea na ndani ya vituo visivyokuwa rasmi. Pembeni ya Goma makaazi yaliyotengenezwa kwa kutumia hema za plastiki au vyandarua yamejaa huku watu wengine wakihifadhiwa ndani ya majengo ya kanisa na shule.

Wajumbe wa MSF wanahudumu katika vituo vya wakimbizi pembeni ya mji wa Goma tangu 2022 kwa kuwapa madawa bila kuwalipisha, gari za shirika hilo liliwapelekea maji safi na kuwajengea vyoo na baafu.

Mapigano yanaendelea kuripotiwa katika maeneo tofauti ya Kivu kaskazini na kuzidi kusababisha idadi kubwa ya wananchi kutimka

Previous Uvira : zaidi ya watu wengine 300 kutoka Burundi wakimbilia nchini DRC
Next Gatumba : mafuriko yalazimisha familia nyingi kukimbia

You might also like

Wakimbizi

Nduta (Tanzania) : uhaba mkubwa wa damu wakati wa mripuko wa malaria

Damu zimekosekana katika vituo vya afya ndani ya kambi ya Nduta nchini Tanzania. Sababu kuu ya hali hiyo ni watoa damu kuacha kutoa damu kutokana na ukosefu wa chakula kuzuri.

Jamii

Cibitoke: Wasichana 15 walio na umri wa chini ya miaka 10 walibakwa katika muda wa chini ya miezi mitatu, jambo ambalo ni la aibu

Cibitoke, Aprili 7, 2025 – Mkoa la Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi) limetikiswa na wimbi la kutisha la unyanyasaji wa kingono dhidi ya watoto. Katika muda wa chini ya miezi mitatu,

Wakimbizi

Siku ya Wakimbizi Duniani 2026: Kati ya Kukata tamaa, shinikizo la kurejea, na mgogoro wa muda mrefu wa kibinadamu katika kambi.

Kutoka Nyarugusu hadi Kakuma, kupitia Mahama, Nakivale, Meheba, Lusenda, na maeneo ya mapokezi nchini Burundi, wakimbizi wa Burundi na Kongo wanapitia Siku ya Wakimbizi Duniani inayoadhimishwa na kupungua kwa usaidizi