Burundi : serikali iliamuru kusamehe ushuru kwa baadhi ya bidhaa za vyakula kutoka nje ya nchi

Burundi : serikali iliamuru kusamehe ushuru kwa baadhi ya bidhaa za vyakula kutoka nje ya nchi

Serikali ilichukuwa uamzi wa kusamehe ushuru kwa baadhi ya bidhaa mahitajio muhimu kama mchele, maharagwe, mbegu za mahindi, sukari ,…. kupitia tangazo la 30 machi 2023. Wizara ya fedha ilifahamisha kuwa bidhaa hizo za vyakula zilisamehewa ushuru wa hadi asilimia 1.5 ya ushuru wa forodhani. Hatua hiyo ilipokelewa vizuri na wafanyabiashara waliohojiwa. Hata hivyo wanahofia kuwa haitakuwa na athari kubwa kwenye soko. HABARI SOS Médias Burundi

Sheria hiyo ya kiwaziri ya tarehe 30 machi ilikuja kama suluhu kwa ajili ya kustawisha bei ya bidhaa hizo kwa mjibu wa wizara ya fedha.

Wafanyabiashara walipokea vizuri hatua hiyo. Kwa mjibu wao, bidhaa hizo sasa zinapatikana zaidi katika soko. Wanaomba serikali kuhakikisha hatua hiyo inachukuliwa kwa bidhaa zingine.

Lakini watumiaji upande wao wanasalia na wasi wasi. Hawaamini kuwa mabadiliko makubwa yatatokea.

Baadhi ya watalaam wa uchumi waliohojiwa upande wao wanadai kuwa hatua ya kusamehe ushuru wa baadhi ya bidhaa za vyakula inaweza kubadili hali lakini hapana hadi kupunguza bei kama inavyotarajiwa. ” Hatua hiyo itasaidia kuongeza kiwango cha bidhaa ndani ya nchi”, walizidi kusema baadhi.

Watalaam wa maswala ya uchumi wengine wanadai kuwa ni budi iwepo sera ya kitaifa ya kuongeza uzalishaji wa ndani ili bei ya bidhaa masokoni iweze kupunguka . Hata hivyo watalaam hao wanapendekeza ziwepo hatua za ziada ili hatua hiyo ya serikali iweze kuwa na athari inayodhihirika .

Previous Nakivale-Mahama : zoezi la kuhesabu upya wakimbizi na kuhakiki tena hadhi zao za ukimbizi lasababisha wasi wasi kwa wahusika
Next Cibitoke : waasi wa Rwanda wa kundi la FLN waripotiwa katika maeneo kadhaa ya umaa tarafani Mabayi, viongozi wachukuwa hatua ya kuwafungiana

You might also like

Jamii

Kayanza: mji umetumia zaidi ya miezi miwili bila umeme

Wakaaji wa mtaa wa Gasenyi katika wilaya ya Rango katika mkoa wa Kayanza (kaskazini mwa Burundi) wametumia zaidi ya miezi miwili bila umeme. Wafanyabiashara wanasema wanafanya kazi kwa hasara wakati

Jamii

Bururi: kusikiliza vyombo vya habari uhamishoni bado ni kosa

Mkurugenzi wa Shule ya Upili ya Jumuiya ya Murehe katika jimbo la Bururi (kusini mwa Burundi), Germain Ntakarutimana, alikaa kizuizini kwa usiku kucha kwa kusikiliza matangazo ya Humura ya RPA

Jamii

Burundi: Shirika la Kimataifa la Wanawake (UN Women) latoa kinu kidogo cha mafuta kwa chama cha ushirika cha wanawake walio katika mazingira magumu huko Rumonge

SOS Médias Burundi Rumonge, Mei 6, 2025 – Ishara kali ya kuunga mkono uwezeshaji wa kiuchumi wa wanawake wa vijijini. Mnamo Aprili 29, UN Women ilikabidhi rasmi kinu cha mafuta