Cibitoke : waasi wa Rwanda wa kundi la FLN waripotiwa katika maeneo kadhaa ya umaa tarafani Mabayi, viongozi wachukuwa hatua ya kuwafungiana
Hatua ya kufunga shughuli zote kwenye kituo cha Kivogero kinachotembelewa na waasi wanaozungumza Kinyarwanda waliopiga kambi katika msitu wa Kibira ilichukuliwa na mkuu wa tarafa ya Mabayi katika mkoa wa Cibitoke ( kaskazini magharibi mwa Burundi) .
Hatua hiyo ilipokelewa vibaya na wafanyabiashara. Mkuu wa tarafa hiyo alifahamisha kuwa alichukuwa hatua hiyo kwa ajili ya kulinda usalama. HABARI SOS Médias Burundi
Hatua hiyo ilichukuliwa mkuu wa tarafa ya Mabayi katika mkoa wa Cibitoke tangu wiki moja iliyopita.
Mahali yaliyolengwa ni pamoja na migahawa ya pombe na vyakula , maduka, pamoja na soko linalopatikana katika mlima wa Kivogero kwenye umbali wa kilometa mbili ya makao makuu ya tarafa hiyo.
Chanzo katika jeshi kinafahamisha kuwa waasi wa kundi la FLN wanaopigana dhidi ya serikali ya Kigali kutoka msitu wa Kibira siku ya ijumaa walihemea katika soko hilo.
” Wanaume hao wanaoficha sura zao na kuongea Kinyarwanda walipeleka bidhaa za vyakula kama unga wa mihogo, mahindi, maharagwe na viatu. Walirejea katika msitu huo kwenye mpaka na Rwanda ” chanzo chetu kilifahamisha.
Daima kulingana na chanzo hicho, kundi hilo linapata usaidizi kutoka Imbonerakure (wafuasi wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD) na kutoka kwa baadhi ya wanajeshi wa FDNB ( jeshi la Burundi) ambao wanawasaidia kupata usafiri wa bidhaa walizonunua.
Viongozi tawala wanasema kukasirikishwa na mwenendo huo wakati huu wa kufufuka kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Gitega na Kigali”.
Wakaazi waliohojiwa wanaridhishwa na hatua hiyo ya mkuu wa tarafa na kuomba waasi hao wapigwe vita.
” Haikubaliki kuona watu hao wenye silaha wakijinufaisha na kutembea katika tarafa yetu kila mtu akiwaona bila kuguswa” alilaani mkaazi mmoja eneo hilo.
Shahidi huyo alihakikisha kuwa mbali ya waasi hao kupiga kambi ndani ya msitu wa Kibira kwa kipindi kirefu, wamekuwa wakionekana pia karibu na msitu huo mkubwa ndani ya tarafa za Mabayi na Bukinanyana.
Kamanda wa operesheni za kijeshi wa wakati huu ndani ya msitu wa Kibira alithibitisha habari hizo na kuzidi kuwa mashambulizi yanaandaliwa dhidi ya kundi hilo la silaha la watu wanaozungumza Kinyarwanda.
Machi iliyopita, katika mkutano kati ya gavana wa mkoa wa Cibitoke na mkoa wa magharibi mwa Rwanda, mkuu wa mkoa wa magharibi mwa Rwanda François Habitegeko aliwaomba viongozi wa Burundi kuwaambia wananchi waanze kuwafichuwa waasi wao wanaotoka nchini DRC katika mkoa wa Kivu ya kusini ambapo waasi wengi na makundi ya kigaidi yalipiga kambi na kupita katika tarafa za Mabayi na Bukinanyana hususan ili kurudi kuvuruga usalama kwenye ardhi ya Rwanda na kuwauwa wananchi wasiokuwa na hatia “.
” Ni budi kupeana habari na waasi waliokamatwa, wanatakiwa kuonyeshwa wananchi ili kulaani ushirikiano wao kabla ya kuhukumiwa kwa mjibu wa sheria” , alisisitiza bwana Habitegeko .
You might also like
Burundi: kwanini viongozi wa Burundi wanataka kuweka taarifa za wanajeshi waliopewa dhamana ya DRC?
Waziri wa Burundi anayehusika na ulinzi Alain Tribert Mutabazi alikataa Ijumaa iliyopita kutoa maelezo kuhusu ujumbe wa FDNB (Jeshi la Ulinzi la Kitaifa la Burundi) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Gihanga: askari alimuua kijana na kumjeruhi kijana wa miaka sitini
Mauaji hayo yalifanyika katika eneo la Gihungwe katika wilaya ya Gihanga mkoani Bubanza (magharibi). Askari mmoja aliwapiga risasi watu wawili. Mashahidi wanazungumza juu ya mabishano kati ya askari na raia
Cibitoke: mafunzo ya kijeshi kwa Imbonerakure kabla ya kutumwa kwao DRC
Kwa muda wa wiki tatu, wanachama wa ligi ya vijana ya chama cha CNDD-FDD wamekuwa wakipokea mafunzo ya kijeshi katika jimbo la Cibitoke (kaskazini magharibi mwa Burundi). Vyanzo vya ndani
