Bururi : kiongozi wa gereza kuu ya Murembwe na wafanyakazi wenzake wawili wapewa adhabu ya kifungo cha miaka 7 na miezi 6 jela

Bururi : kiongozi wa gereza kuu ya Murembwe na wafanyakazi wenzake wawili wapewa adhabu ya kifungo cha miaka 7 na miezi 6 jela

Kanali wa polisi Patrice Nkurikiye kiongozi wa gereza kuu la Murembwe mkoani Rumonge (kusini magharibi mwa Burundi) na washirika wake wawili wahudumu katika idara ya sheria ndani ya gereza hilo, Florence Nimbona na Pélagie Nindamutsa wote walikatiwa kifungo cha miaka 7 na miezi 6 jela. Watatakiwa pia kulipa faini ya franka za Burundi milioni moja kila mmoja. Hukumu hiyo ilitolewa na mahakama ya rufaa ya Bururi (kusini ) jumanne hii. Walipatikana na kosa la kuchangia katika ” kuvuruga usalama wa ndani ya nchi”. HABARI SOS Médias Burundi

Katika kesi ya mafumanio iliyofanyika wiki moja iliyopita, korti ya mkoa wa Bururi ilitoa hukumu kama hiyo ambayo iliendelezwa badaye na mahakama ya rufaa ya mkoa .

Watuhumiwa walipinga tuhuma zote dhidi yao. Tuhuma hizo zilihusu kuachiliwa huru kwa wafungwa waliokuwa wakifuatiliwa katika kesi ya mauwaji kwa kutumia mapanga. Mauwaji hayo yalitekelezwa kwenye makao makuu ya mkoa wa Bururi na viunga vyake katika mwezi mei iliyopita.

Siku moja baada ya kuwaachilia huru kwa muda wafungwa saba kati ya wale nane walikamatwa kwa mara nyingine.

Majaji watatu wa mahakama ya mkoa wa Bururi walikamatwa mwanzoni mwa wiki iliyopita.

Majaji hao Antoine Ndendakumana, Léonard Nizigiyimana na Irène Mukeshimana wanazuiliwa katika gereza la Bururi. Wanafuatiliwa kwa kuwaachilia huru kwa muda wafungwa wanaohusishwa katika faili ya mauwaji kwa kutumia mapanga mkoani Bururi kwa mujibu wa mwendeshamashtaka wa jamuhuri.

Previous Mabayi : waziri mkuu wa serikali ya Burundi atishia kuwauwa watu wote wanaoshirikiana na waasi wa Rwanda waliopiga kambi ndani ya msitu wa Kibira
Next DRC (Kalehe) : watoto saba wafariki dunia kwa kuteketezwa na moto ulioibuka katika kambi ya wahanga wa mafuriko

You might also like

Siasa

Uchaguzi wa Buhumuza: Wapinzani Walia Kukosa Taarifa na Vitisho

SOS Médias Burundi Buhumuza, Juni 6, 2025 – Masanduku ya kura yalifungwa kwa shida kabla ya mvutano kuongezeka Buhumuza. Katika mkoa huo ambalo bado ni tete kisiasa, vyama kadhaa vya

Siasa

Burunga: Uzinduzi wa kampeni ya CNDD-FDD, kati ya matokeo ya shangwe na mashaka ya wengi

SOS Media Burundi Burunga, Mei 19, 2025 – Chama cha CNDD-FDD kilizindua rasmi kampeni yake ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa wabunge na manispaa katika mkoa wa Burunga (kusini-mashariki),

Siasa

Rumonge: Rais Ndayishimiye awashambulia wale wanaobeza maono ya 2040-2060

Wakati wa ufunguzi wa jengo jipya la ofisi ya mkoa katika jimbo la Rumonge kusini magharibi mwa nchi, Rais Évariste Ndayishimiye aliwashambulia kwa nguvu watu “ambao huvuruga umakini wa watu