Bururi : kiongozi wa gereza kuu ya Murembwe na wafanyakazi wenzake wawili wapewa adhabu ya kifungo cha miaka 7 na miezi 6 jela
Kanali wa polisi Patrice Nkurikiye kiongozi wa gereza kuu la Murembwe mkoani Rumonge (kusini magharibi mwa Burundi) na washirika wake wawili wahudumu katika idara ya sheria ndani ya gereza hilo, Florence Nimbona na Pélagie Nindamutsa wote walikatiwa kifungo cha miaka 7 na miezi 6 jela. Watatakiwa pia kulipa faini ya franka za Burundi milioni moja kila mmoja. Hukumu hiyo ilitolewa na mahakama ya rufaa ya Bururi (kusini ) jumanne hii. Walipatikana na kosa la kuchangia katika ” kuvuruga usalama wa ndani ya nchi”. HABARI SOS Médias Burundi
Katika kesi ya mafumanio iliyofanyika wiki moja iliyopita, korti ya mkoa wa Bururi ilitoa hukumu kama hiyo ambayo iliendelezwa badaye na mahakama ya rufaa ya mkoa .
Watuhumiwa walipinga tuhuma zote dhidi yao. Tuhuma hizo zilihusu kuachiliwa huru kwa wafungwa waliokuwa wakifuatiliwa katika kesi ya mauwaji kwa kutumia mapanga. Mauwaji hayo yalitekelezwa kwenye makao makuu ya mkoa wa Bururi na viunga vyake katika mwezi mei iliyopita.
Siku moja baada ya kuwaachilia huru kwa muda wafungwa saba kati ya wale nane walikamatwa kwa mara nyingine.
Majaji watatu wa mahakama ya mkoa wa Bururi walikamatwa mwanzoni mwa wiki iliyopita.
Majaji hao Antoine Ndendakumana, Léonard Nizigiyimana na Irène Mukeshimana wanazuiliwa katika gereza la Bururi. Wanafuatiliwa kwa kuwaachilia huru kwa muda wafungwa wanaohusishwa katika faili ya mauwaji kwa kutumia mapanga mkoani Bururi kwa mujibu wa mwendeshamashtaka wa jamuhuri.
You might also like
Kampeni za uchaguzi Kiremba: CNDD-FDD inaonyesha nguvu zake katika hali ya wasiwasi
SOS Médias Burundi Ngozi, Mei 13, 2025 – Taifa dogo la Afrika Mashariki linaingia katika awamu ya kampeni yenye mvutano, inayoadhimishwa na hamasa kubwa, uwepo mkubwa wa umoja wa vijana
Burundi: vyama vinne vya siasa vya upinzani vinaunda muungano wa kwanza kabisa kwa chaguzi zijazo
Hivi ni vyama vya FRODEBU, CODEBU, FEDES-SANGIRA na CNDD. Marais wao waliwasilisha faili inayohusiana na muungano wao Ijumaa iliyopita, Desemba 13. Alipokelewa na wizara inayohusika na mambo ya ndani inayosimamia
Burunga: Wapinzani 50 wameondolewa kwenye orodha ya wagombea udiwani wa manispaa
Wagombea hao hamsini walipendekezwa na muungano mpya wa kisiasa “Burundi Bwa Bose”. Tume ya Uchaguzi ya Mkoa inatoa sababu kuu mbili: kukosekana kwa saini kwenye CV na kutokuwepo kwa utambulisho
