Gihanga : bibi kizee wa zaidi ya miaka sabini auwawa
Mwanamke mwenye wa miaka 75 alikatwa kichwa na watu wasiojulikana bado katika kijiji cha Rugunga tarafa ya Gihanga mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). Polisi tayari iliwakamata watuhumiwa watatu. HABARI SOS Medias Burundi
Janga hilo lilitokea usiku wa jumanne tarehe 12 kuamkia jumatano 13 septemba katika kijiji cha Rugunga. Jacqueline Nahishakiye mwenye umri wa miaka 75 aliuwawa akiwa nyumbani kwake.
” Maiti yake ilikuwa ikilala ndani ya damu huku kichwa kikiwa kilikatwa kwa kutumia panga”, alitoa ushahidi huo jirani.
Mkuu wa kijiji cha Rugunga, Célestin Rivugo akizungumzia na SOS Médias Burundi alithibitisha habari hizo na kuzidi kusema kuwa mauwaji hayo yalisababishwa na mizozo ya ardhi.
Kifo chake kilitokea siku moja baada ya kuzuru ardhi anazomiliki.
Uvumi mwingi unahusisha baadhi ya wajumbe wa familia yake kama watu walioandaa mauwaji hayo.
Ndugu wa muhanga ambaye walikuwa hawaelewani kwa muda mrefu kulingana na mashahidi katika kijiji cha Rugunga kwa sasa anazuiliwa katika gereza la tarafa ya Gihanga.
Watu wa karibu na muhanga wanaomba wapelekwe mahakama haraka waliohusika na mauwaji hayo.
You might also like
Bujumbura Inakabiliwa na mgogoro wa vyoo vya umma: Wakazi washutumu faini inayoonekana si ya haki
SOS Médias Burundi Bujumbura, Novemba 12, 2025 – Hatua mpya ya serikali imezua hasira miongoni mwa wakazi wa mji mkuu wa kiuchumi. Tangu kuchapishwa kwa agizo la pamoja la Mawaziri
Bujumbura: Kashfa katika wodi ya wazazi ya hospitali ya Roi Khaled baada ya watoto wawili waliozaliwa kubadilishwa
SOS Médias Burundi Bujumbura, Oktoba 30, 2025 – Tukio la kusikitisha lilitokea Jumanne hii, Oktoba 28, katika Hospitali ya Roi Khaled mjini Bujumbura, mji mkuu wa kiuchumi wa Burundi. Wanawake
Burundi: Nyuma ya FRAD, hofu ya kuundwa upya kwa busara kwa jeshi
Bujumbura, Mei 7, 2026 – Mabadiliko ya kituo cha mbegu cha umma cha Kigarika, katika tarafa ya Ruyigi ya mkoa wa Buhumuza, mashariki mwa taifa hilo dogo la Afrika Mashariki,
