DRC (Beni) : watu zaidi ya kumi wauwaw a katika shambulio jingine la kundi la ADF eneo la Rwenzori
Watu 13 waliuwawa katika shambulio jingine ya waasi wa AFD (nguvu zilizoungana kwa ajili ya demokrasia) katika usiku wa alhamisi kuamkia ijumaa . Shambulio hilo lilifanyika katika kitongoji cha Bukokoma karibu ya eneo la Nzenga kwenye umbali wa kilometa takriban tano kutoka kijiji cha Mutwanga makao makuu ya Rwenzori ndani ya wilaya ya Beni mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC. HABARI SOS Médias Burundi
Hayo yanaripotiwa na baraza la vijana wa eneo la Rwenzori ambao wanazidi kuhakikisha kuwa mbali na watu waliouwawa, wengine wengi hawajulikani walipo. Mifungo mingi pia iliibiwa .
Kulingana na Bernard Muke, kiongozi wa baraza hilo, waasi waliingia kwa kujificha ndani ya kijiji hicho. Waliuwawa wananchi wa kawaida kwa kutumia silaha zisizokuwa za moto kama wanavyoripoti mashahidi.
” ilikuwa majira ya saa tatu za usiku ambapo adui aliingia katika vijiji vya Bukokoma kuelekea magharibi mwa kijiji cha Mutwanga ambapo walianza kuwauwa wananchi. Majira ya saa saba za usiku katika siku ya ijumaa tarehe 9 juni, tulianza kupata ujumbe kuwa miili ya watu zaidi ya kumi imefikishwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali kuu ya Mutwanga. Tukiangalia namna walivyotenda, bila shaka ni waasi wa kundi la ADF waliotekeleza shambulio hilo. Waasi hao walikuwa wakijaribu kuingia katika eneo hilo kwa muda mrefu pasina kufanikiwa. Walibadili mbinu kwa kuingia katika majumba bila kupiga risasi”, alifahamisha.
Baraza la vijana wa eneo hilo la Rwenzori linasema kuwa wananchi wengine wa kawaida huenda walitekwa na waasi lakini pia mali za wananchi ziliibiwa wakati wa uvamizi huo.
Bernard Muke inatoa wito kwa wananchi kuwa wangalifu. Hata hivyo analaani uzembe unaoshuhudiwa tangu siku chache zilizopita upande wa taasisi ya usalama katika eneo hilo. Alizidi kusema kuwa hali hiyo inatoa nafasi kubwa kwa kundi la ADF kuvamia wananchi waliotulia.
You might also like
Gihanga: Mwanamume aliyetekwa nyara siku ya Jumanne bado hawezi kupatikana
Dieudonné Gahungu, baba mdogo wa mtoto mmoja, alitekwa nyara Jumanne saa sita mchana katika wilaya ya Gihanga katika mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi) na wanaume watatu, wawili kati yao
Mbuye (Muramvya): Familia ya Oscar Mbonihankuye, aliyeuawa na Imbonerakure kwa kutoshiriki kazi za jamii, inadai mwili wake
Oscar Mbonihankuye, mwenye umri wa miaka 60, alikamatwa, kuteswa na kisha kutupwa kwenye Mto Mubarazi na Imbonerakure zaidi ya wiki mbili zilizopita. Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, matukio
Kivu Kusini: Wanajeshi wa Burundi kwa wingi Fizi kupunguza mwendo wa Twirwaneho na kuwadhibiti M23
SOS Media Burundi Bukavu, Mei 22, 2025 – Harakati kubwa za kijeshi zimezingatiwa katika siku za hivi majuzi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Tangu Jumatano, wanajeshi wapya wa
