Kayogoro : wafuasi wa vyama vya upinzani watiwa wasi wasi na sensa inayofanyika

Kayogoro : wafuasi wa vyama vya upinzani watiwa wasi wasi na sensa inayofanyika

Wafuasi wa vyama vya upinzani wanasema kuwa wanahofia mabaya kutokea kufuatia sensa iliyoanza jumatano tarehe 7 juni katika kijiji vyote vya tarafa ya Kayogoro mkoa wa Makamba (kusini mwa Burundi) . Sensa hiyo ya wananchi kuhusu vyama vyao inaendeshwa na wafuasi wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD Imbonerakure. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa vyanzo katika tarafa ya Kayogoro, sensa hiyo ilianza jumatano tarehe 7 katika vijiji vyote vya tarafa hiyo.

Sensa hiyo inatofautisha wafuasi wa chama cha CNDD-FDD na wale wa upinzani, jinsia na miaka yao .

Vyanzo vyetu vinathibitisha kuwa Imbonerakure wanaofanya sensa hiyo hupita nyumba hadi nyingine katika vijiji vyote na vitongoji.

Kulingana na vyanzo katika baadhi ya Imbonerakure wanaoendesha sensa hiyo, zoezi hilo linalenga kuwatishia wafuasi wa vyama vya upinzani ili wasithubutu kuonyesha uwanachama wao katika vyama vya upinzani.

” Hiyo itatusaidia kupotosha matokeo ya uchaguzi ujao”, walihakikisha Imbonerakure waliozungumza na SOS Médias Burundi.

” Hiyo itatuwezesha kuhakikisha kuwa hakuna hata mfuasi mmoja wa chama cha upinzani katika vijiji mbali mbali na kwa hiyo chama cha upinzani hakitakuwa na haki ya kupinga matokeo” alifahamisha Imbonerakure mmoja wa eneo hilo kwa sharti ya kubana jina lake.

Upande wa upinzani, wafuasi wanasema kuwa wanaishi katika hali ya wasi wasi kwa sababu ” hali hiyo inaweza kusababisha mauwaji ya wafuasi wa upinzani”.

Wanaomba viongozi wa nchi kusimamisha mara moja aina hiyo ya sensa. Viongozi wa tarafa na wakuu wa chama tawala hawakupatikana ili kujibu maswali yetu.

Previous DRC (Beni) : watu zaidi ya kumi wauwaw a katika shambulio jingine la kundi la ADF eneo la Rwenzori
Next DRC : raia wa Kongo waelekea kupata kadi ya uraia

You might also like

Usalama

Moto Katika Shule ya upili ya Nyabigina: bweni lapungua na kuwa Majivu, Wanafunzi wafadhaika

SOS Médias Burundi Makamba, Oktoba 11, 2025 – Moto ulizuka Jumamosi hii asubuhi mwendo wa saa 8:30 a.m. katika Shule ya Upili ya Nyabigina, katika wilaya ya Makamba, jimbo la

Usalama

Cibitoke : watu watano wenye asili ya Rwanda wanaobebelea silaha waliuwawa katika mapigano na jeshi la Burundi ndani ya msitu wa Kibira

Milio ya silaha nzito ilisikika tangu ijumaa iliyopita ndani ya msitu wa hifadhi wa Kibira kwenye milima ya Gasenyi na Gafumbegeti tarafani Mabayi mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Kwa

Utawala

Burunga: Msako katika Nyumba ya polisi kanali Moïse Arakaza, almaarufu Nyeganyega

SOS Médias Burundi Burunga, Agosti 18, 2025 – Kipindi kipya kimeongezwa kwenye kesi ya Kanali Moïse Arakaza wa polisi, kwa jina la utani Nyeganyega, ambaye anashitakiwa kwa kuhujumu uchumi wa