Kayogoro : wafuasi wa vyama vya upinzani watiwa wasi wasi na sensa inayofanyika

Kayogoro : wafuasi wa vyama vya upinzani watiwa wasi wasi na sensa inayofanyika

Wafuasi wa vyama vya upinzani wanasema kuwa wanahofia mabaya kutokea kufuatia sensa iliyoanza jumatano tarehe 7 juni katika kijiji vyote vya tarafa ya Kayogoro mkoa wa Makamba (kusini mwa Burundi) . Sensa hiyo ya wananchi kuhusu vyama vyao inaendeshwa na wafuasi wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD Imbonerakure. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa vyanzo katika tarafa ya Kayogoro, sensa hiyo ilianza jumatano tarehe 7 katika vijiji vyote vya tarafa hiyo.

Sensa hiyo inatofautisha wafuasi wa chama cha CNDD-FDD na wale wa upinzani, jinsia na miaka yao .

Vyanzo vyetu vinathibitisha kuwa Imbonerakure wanaofanya sensa hiyo hupita nyumba hadi nyingine katika vijiji vyote na vitongoji.

Kulingana na vyanzo katika baadhi ya Imbonerakure wanaoendesha sensa hiyo, zoezi hilo linalenga kuwatishia wafuasi wa vyama vya upinzani ili wasithubutu kuonyesha uwanachama wao katika vyama vya upinzani.

” Hiyo itatusaidia kupotosha matokeo ya uchaguzi ujao”, walihakikisha Imbonerakure waliozungumza na SOS Médias Burundi.

” Hiyo itatuwezesha kuhakikisha kuwa hakuna hata mfuasi mmoja wa chama cha upinzani katika vijiji mbali mbali na kwa hiyo chama cha upinzani hakitakuwa na haki ya kupinga matokeo” alifahamisha Imbonerakure mmoja wa eneo hilo kwa sharti ya kubana jina lake.

Upande wa upinzani, wafuasi wanasema kuwa wanaishi katika hali ya wasi wasi kwa sababu ” hali hiyo inaweza kusababisha mauwaji ya wafuasi wa upinzani”.

Wanaomba viongozi wa nchi kusimamisha mara moja aina hiyo ya sensa. Viongozi wa tarafa na wakuu wa chama tawala hawakupatikana ili kujibu maswali yetu.

Previous DRC (Beni) : watu zaidi ya kumi wauwaw a katika shambulio jingine la kundi la ADF eneo la Rwenzori
Next DRC : raia wa Kongo waelekea kupata kadi ya uraia

You might also like

Criminalité

Bujumbura: Madawa ya kulevya yazua madhara Miongoni mwa vijana Musaga na Kanyosha

SOS Médias Burundi Bujumbura, Oktoba 30, 2025 — Matumizi ya dawa za kulevya na pombe yanaongezeka miongoni mwa vijana, hasa wavulana, katika maeneo ya Musaga na Kanyosha katika tarafa ya

Jamii

Kayanza: Watu 19 wang’atwa na mbwa waliozurura huko Gahombo, chanjo ya kichaa cha mbwa imeisha

Hali ya kutisha inatikisa wilaya ya Gahombo, katika jimbo la Kayanza kaskazini mwa Burundi. Tangu Februari, wakazi 19 wameng’atwa na mbwa waliozurura, lakini bado hawawezi kupata matibabu ya kutosha kutokana

Siasa

Burundi: “Miaka mitano ya ahadi, miaka mitano ya ugumu” – Huko Bujumbura, wakazi wa Jiji wachora tathmini ya kufisha juu ya utawala wa Ndayishimiye

SOS Médias Burundi Bujumbura, Juni 19, 2025 Miaka mitano baada ya kuchukua madaraka nchini Burundi, Rais Évariste Ndayishimiye anajikuta akikabiliana na watu waliokatishwa tamaa. Huko Bujumbura – mji mkuu wa