Bujumbura : wakaazi wasumbuka kupata maji safi
Maji safi yamekuwa adimu katika kata za kaskazini na kusini mwa jiji kuu la kiuchumi. Katika baadhi ya kata, wakaazi wanaweza kumaliza wiki moja bila kupata huduma hiyo. Wananchi wanahofia kuambukizwa maradhi yanayosababishwa na uchavu hususan wakikumbuka katika akili za karibu lilivyokuwa janga la kipindupindu. HABARI SOS Médias Burundi
Wakaazi wa kata mbali mbali za jiji la Bujumbura waliohojiwa, wanahakikisha kuwa sasa ni zaidi ya siku tatu bila kupata hata tonya la maji kwenye ma bomba yao.
” Limekuwa ni jambo la kawaida. Ninatembea kila siku na jerikani ndani ya gari langu, ili wakati wa kurejea nyumbani niangalie wapi ninaweza kuchota maji”, alilaani mkaazi wa kata ya Gasekebuye ( kusini mwa jiji).
” Jambo la kushangaza ni kwamba sehemu ya kata hiyo inapata maji safi, wakati sehemu nyingine haina huduma hiyo. Hali hiyo imedumu kwa siku nyingi. Jambo la kusikitisha ni kuwa Regideso haina uwezo la kutoa suluhu kwa tatizo hilo ” amelalamika mkaazi wa kusini mwa jiji la Bujumbura.
Wakaazi wa kata zingine zinazokabiliwa na uhaba wa maji safi wanasema kuwa wanalazimika kulipa ili kupata baadhi ya jerikani ama dumu katika maeneo jirani.
” Jerikani moja hununiliwa franka mia mbili lakini bei inaweza kufikia elfu moja”, alibaini mkaazi mmoja.
Wakaazi wao wanasema kuwa hawana la kufanya. Wanaomba Regideso ( mamlaka ya maji ya umeme ) kutafuta suluhu la haraka na la kudumu. Wanahofia kuambukizwa maradhi yanayosababishwa na usanifishaji mdogo. Uhaba huo unakuwa tishio kubwa kwao hasusan wa wakikumbuka janga la kipindupindu.
” Hakika, janga hilo lilidhibitiwa haraka, lakini hatuwezi kukosa woga”, alieleza mkaazi mmoja wa kata ya Mutanga-Nord kaskazini mwa jiji la kibiashara.
Wanaomba ugavi wa maji ufanyike kwa usawa katika kata zote.
Upande wa Regideso, wanasema sababu kuu ya uhaba huo wa maji , ni mji unaoendelea kuwa mkubwa pamoja pia na kuzeheka kwa mitaro ya maji.
Kuhusu sababu ya kwanza Regideso haina suhulu , lakini inahakikisha kuwa wanaweka mitaro mipya katika nafasi ya ili iliyozeheka.
You might also like
Bujumbura: kaskazini mwa jiji la kibiashara, kitovu cha tumbili walioathiriwa na ukosefu wa maji ya kunywa
Tangu Oktoba 18, wakaazi wa maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu wa kiuchumi Bujumbura wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa maji ya kunywa. Kwa sababu nzuri, bomba kubwa ambalo hutoa sehemu
Burundi: Usambazaji wa vyandarua vilivyotiwa viua wadudu Umevurugwa na muunganisho mbaya
SOS Médias Burundi Bujumbura, Novemba 28, 2025 – Kampeni ya kitaifa ya kusambaza vyandarua vilivyotiwa dawa, iliyozinduliwa Novemba 26 na kupangwa kukamilika Desemba 1, kwa sasa inaendelea katika maeneo ya
Kayanza: Wanaume wanne walikufa baada ya kunywa bia iliyopigwa marufuku
Wanaume hawa wanne walikufa wakati wa usiku kutoka Alhamisi hadi Ijumaa. Wahasiriwa walikuwa na watu wengine watatu ambao wamelazwa hospitalini kwa sasa. Mkasa huo ulitokea katika mji mkuu wa jimbo
