DRC : raia wa Kongo waelekea kupata kadi ya uraia
Mkataba ulitiwa saini alhamisi hii tarehe 8 juni kati ya tume ya kitaifa ya uchaguzi (CENI), ofisi ya kitaifa ya utambulisho na wananchi (ONIP) pamoja na idara ya kitaifa ya takwimu (INS) kwa lengo la kuwapatia wananchi wa Kongo kadi ya uraia. Itakuwa ni mara ya kwanza kwa raia wa Kongo kupewa kadi ya uraia. Waziri mkuu aliyehudhuria sherehe hizo za kutia saini aliwasihi kuteleleza kikamilifu misheni hiyo ” kwa mantiki ya kuweka vitendoni muongozo wa rais wa jamuhuri Félix Tshisekedi”. HABARI SOS Médias Burundi
Mkataba huo unaamuru kwanza tume huru ya kitaifa ya uchaguzi kuzikabidhi ofisi za ONIP na INS data na vifaa ya kukusanyisha maelezo pamoja pia sheria za uandikishaji. Ofisi hizo mbili zinatakiwa kuendelea na operesheni ya utambulisho na sensa ya wananchi na hivyo kufungua njia ya kutoa kadi ya uraia.
Sherehe hizo zilifuatiwa na kukabidhi ofisi ya ONIP alama za baadhi ya vifaa vilivyotumiwa katika zoezi la kuandikisha wapiga kura ili kuruhusu ofisi hiyo kuanzisha rasmi zoezi la kuorodhesha wananchi kwa kuanzia katika mji- mkoa wa Kinshasa kama mkoa wa mfano mnamo siku zijazo.
Mbali na vifaa hivyo, tume huru ya kitaifa ya uchaguzi ilikabidhi kwa muda wafanyakazi wake ofisi hiyo ya kitaifa ya utambulisho wa wananchi ili kuunga mkono zoezi hilo.
Akieleza kuwa kitendo hicho ni kwa lengo la kutumia vizuri uwezo wa kifedha ambao serikali ingetumia ili kutekeleza operesheni hiyo, waziri mkuu Sama Lukonde alitoa wito kwa wadau kuongeza juhudi ili kufikia malengo waliojipa.
Katika nchi hiyo kubwa ya Afrika ya kati, ni kadi ya wapiga kura ambayo hutumiwa kama kadi ya uraia hadi sasa. Kwa sababu hiyo, hata wafungwa wanaorodheshwa wakati wa kipindi cha uchaguzi ili kuepusha wafungwa wa zamani kujikuta wakiwa hawana kadi ya utambulisho.
You might also like
Ituri: Raia 25 wauawa katika shambulizi la ADF huko irumu
SOS Médias Burundi Irumu, Januari 26, 2026 – Wanamgambo kutoka Allied Democratic Forces (ADF) walishambulia tena kijiji cha Apakolu, katika eneo la chifu la Walese Vonkutu eneo la Irumu katika
“Imekataliwa Kila mahali”: Wakimbizi wa Kongo watishiwa kurejea katika vituo vya usafiri nchini Burundi
SOS Médias Burundi Musenyi, Mei 5, 2026 — Nchini Burundi, hali ya baadhi ya wakimbizi wa Kongo wanaoishi katika eneo la Musenyi katika mkoa wa Burunga, kusini mashariki mwa taifa
Burundi : nchi imepata mwendeshamashtaka mkuu mpya
Ni Léonard Manirakiza, ameidhinishwa jumanne hii na baraza la seneti. Wanaharakati wanasema kuwa hawataraji mambo makubwa kutoka kwake lakini wameamuru kujizuia kueleza chochote. HABARI SOS Médias Burundi Léonard Manirakiza ameidhinishwa
