Burundi : ni mapema kubainika wazi madhambi ya Bunyoni
Mahakama kuu ya Burundi alhamisi hii ilifahamisha kuwa mwendeshamashtaka mkuu wa jamuhuri anaendelea kutafuta mashtaka mapya dhidi ya Bunyoni. Msemaji wa mahakama kuu na ofisi ya mwendeshamashtaka mkuu aliyefahamisha hayo, alizidi kusema kuwa mwendeshamashtaka yuko na taarifa mpya zinazoweza kumuelekeza kwenye njia ya maovu mengine katika faili dhidi ya waziri mkuu wa zamani Allain Guillaume Bunyoni. HABARI SOS Médias Burundi
Ni katika kipindi cha wasemaji wa taasisi za umma ambapo msemaji wa mwendeshamashtaka mkuu alifahamisha hayo. Alikuwa akijibu swali la mwandishi wa habari wa ndani ya nchi.
“Katika awamu wa mwanzo, Bunyoni alifuatiliwa kwa kuvuruga usalama wa ndani ya nchi, kuhujumu uchumi na kutumia cheo chake kutafuta maslahi yake binafsi na kumiliki silaha kinyume cha sheria pamoja na kumutukana rais wa nchi”, alifahamisha Agnès Bangiricenge.
Alisema kuwa “mwendeshamashtaka alikataa rufaa baada ya wakili wake kupinga hatua ya kumushikilia jela kwa muda. Mwendeshamashtaka alipata habari mpya zinazoweza kumufungulia mashtaka mapya”, alisisitiza.
Mmoja kati ya waendeshaji wa kipindi alitaka kujuwa maelezo zaidi kuhusu madai ya kumiliki silaha kinyume cha sheria wakati Bunyoni akiwa askali polisi wa cheo cha jemedali.
“Ni wewe unaoona hivyo na kusema hivyo hivyo. Iwapo wamesema anamiliki silaha kinyume cha sheria, inamaanisha kuwa waligundua nyumbani kwake silaha zingine mbali na zile anazoruhusiwa kumiliki”, alijibu hivyo kwa hasira.
Mwanzoni mwa mwezi mei mwaka huu, Alain Guillaume Bunyoni alipelekwa katika gereza kuu ya Ngozi (Kaskazini mwa Burundi) baada ya kumaliza siku nyingi katika gereza la SNR (idara ya kitaifa ya ujasusi) ndani ya mji wa kibiashara wa Bujumbura.
Shirika la Human Right Watch linaomba viongozi wa Burundi kuhakikisha kesi dhidi yake inaendeshwa kwa haki na uwepo wa waangalizi wa kimataifa ili haki ya Bunyoni iweze kuheshimiwa”.
Muasi huyo wa zamani wa kihutu chini ya vikwazo vya serikali ya marekani, alifutwa kwenye wadhifa wake na rais wa jamuhuri Evariste Ndayishimiye mwanzoni mwa mwezi septemba 2022 katika mazingira ya giza.
You might also like
Matana: Mamilioni yamefujwa, ofisi za Ghost – kashfa ya maeneo yaliyotelekezwa ya ujenzi
SOS Médias Burundi Burundi, Machi 29, 2026 – Katika tarafa ya Matana, katika mkoa wa Burunga, kusini mwa taifa hili dogo la Afrika Mashariki, ujenzi ambao haujakamilika wa ofisi kadhaa
Giharo: vyama vya ushirika vya kilimo vilivyopokonywa ardhi yao vinashutumu ufisadi uliochanganyikana na nia za kisiasa
Wakulima na vyama vya ushirika vya kilimo kutoka Giharo commune, mkoa wa Rutana (kusini-mashariki mwa Burundi) wanamshutumu mkurugenzi wa ofisi ya mkoa ya mazingira, kilimo na mifugo (BPEAE) kwa kusambaza
Kirundo: Utawala Unataka Kuidhinisha Wanawake Peke Yake katika Vilabu vya Usiku
SOS Media Burundi Kirundo, Februari 9, 2026 – Uamuzi uliotangazwa Jumanne iliyopita umezua mabishano makali katika eneo la Kirundo, katika eneo la jina moja katika mkoa Butanyerera, kaskazini mwa Burundi.
