Burundi : tatizo la uhaba wa mafuta, majibu yake bado kupatikana
Baada ya miezi 18 ya uhaba wa mafuta ya gari, viongozi wa Burundi hawawapi moyo wananchi. Wanachukuwa hatua zisizodumu. Wanaharakati upande wao, wanaomba mkutano mkuu ufanyike kuhusiana na tatizo hilo. HABARI SOS Médias Burundi
Nchini Burundi, linapokuja swala la uhaba wa mafuta ya gari, watu wamekata tamaa wengine wamezoea . Wananchi wanatakiwa kuzowea uhaba wa mafuta ya gari na hasa uongo na majibu ya kukwepa yanayotolewa na viongozi ambao wanazidi kuhakikisha kuwa ” ghala za Burundi zimejaa ” mjini Dar Es Salam ( Tanzania).
Ukweli huo ulikaririwa alhamisi hii na msemaji wa rais Ndayishimiye.
” Kuna waagizaji wa mafuta wasiopenda nchi ambao wanaegesha lori zao nyumbani na kukataa kwenda kuleta mafuta nchini Tanzania. Hawako juu ya sheria na sio watu wasioweza kuguswa. Idara zinazohusika zinawajibika na watu hao watapelekwa mbele ya sheria wakati wowote”, alifahamisha msemaji wa rais Evariste Ndayishimiye, Rosine Guilene Gatoni katika kipindi cha wasemaji wa taasisi za umma kilichofanyika mkoani Muramvya kati kati mwa Burundi.
Kwa mujibu wake, serikali itaangalia uwezekano wa kununua lori zake na kujiandaa kujenga ghala katika ardhi ya Burundi . Na hapa hakuna maelezo yaliyotolewa.
Kwa mujibu wa watalaamu, swala la uhaba wa mafuta ya gari ni ngumu na linaomba kujadiliwa katika mkutano mkuu.
” Ni tatizo linalodumu. Limekuwa na kawaida. Warundi wanatakiwa kuona mafuta hapa, na sio katika ghala mjini Dar Es Salam. Hata Kongo ambayo inakabiliwa na mzozo na ambayo tunasaidia katika maswala ya usalama, haina matatizo ya kuagiza mafuta ya gari”, anasema Faustin Ndikumana, kiongozi wa Parcem , shirika linalopambana kwa ajili ya utawala bora.
Wadadisi wengi wanadai kuwa tatizo la uhaba wa mafuta ya gari husababishwa na uhaba wa pesa ya kigeni, na urasibu mbaya.
You might also like
Burundi: Serikali inakabiliwa na mgogoro wa kushtua wa majengo
SOS Médias Burundi Bujumbura, Novemba 17, 2025 – Serikali ya Burundi inakabiliwa na mzozo wa kuhuzunisha wa mali isiyohamishika. Kulingana na data iliyowasilishwa katika mkutano wa serikali wiki iliyopita, nchi
Bubanza: wakazi walazimika kukaribisha mwenge wa amani, shule na biashara kufungwa
Biashara, shule, utawala, wakazi… Kila mtu alilazimika kwenda kuukaribisha mwenge wa amani Jumanne hii katika wilaya ya Bubanza. Iko katika jimbo la Bubanza (magharibi mwa Burundi). Msafara huo uliozinduliwa na
Burundi: Mishahara midogo, uhaba, na wimbi la kuondoka—je, serikali inaruhusu utumishi wa umma kufa?
SOS Médias Burundi Bujumbura, Agosti 11, 2026—Kila wiki, matangazo ya watu waliopotea yanayorushwa na Shirika la Taifa la Redio na Televisheni la Burundi (RTNB) yanaangazia hali ya kutia wasiwasi: watumishi
