Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Ni muili wa mwanamke ambaye hakutambulika. Ulipatikana kwenye mstari wa kutenganisha eneo linalokaliwa na raia wa Kongo na lile wa raia wenye asili ya Burundi. Uchunguzi tayari imeanza ili kutambua aliyefariki. HABARI SOS Médias Burundi

Muili huo ni wa mwanamke wa kati ya miaka 25 na 30, kwa mujibu wa mashahidi. Muili huo uligunduliwa na wapita njia mapema jumatano hii asubuhi.

” Maiti ilikuwa imeanza kuharibika na kutoa harufu mbaya ambayo ilisababisha wapita njia kuangalia. Waliita mara moja polisi ambao walikuja kuchukuwa maiti hiyo. Polisi hiyo iliahidi pia kufanya uchunguzi kwa ajili ya kumutambua muhanga” , walisema wakimbizi.

Muili uliwekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika kijiji cha 3 eneo la raia wenye asili ya Kongo ili kusubiri kipindi cha siku tatu kwa ajili ya kijaribu kutambua muhanga kabla ya mazishi yake yanayotarajiwa wekendi ijayo, kwa mujibu wa viongozi wa kijamii.

Viongozi hao waliitisha mikutano ndani ya kila kijiji ili kuangalia iwapo kuma mtu ambaye atadai kutafuta mtu wake.

Taarifa za kwanza za polisi na viongozi tawala zinasema huenda muhanga ” alinyongwa ” sababu muili wake ulikuwa na majeraha.

Hadi sasa, jina la muhanga, na uraia wake bado kujulikana ikizingatiwa kuwa kambi ya Nyarugusu inawapa hifadhi raia kutoka Burundi pamoja na Kongo wanaokadiriwa kuwa wakimbizi laki moja na elfu 10.

Previous Burundi - Rwanda : mke wa rais wa Burundi afanya ziara katika nchi jirani ambayo hadi sasa mumeo apata tabu kutembelea
Next Burundi : ni budi kuwa makini katika kuwatuma wasichana nchini Saudi Arabia, alisema mke wa rais

You might also like

Wakimbizi

Dzaleka (Malawi): kutoweka kwa viongozi wawili wa jumuiya ya wakimbizi

SOS Médias Burundi Dzaleka, Mei 27, 2025 – Wanachama wawili mashuhuri wa jumuiya ya wakimbizi katika kambi ya Dzaleka, Malawi, wametoweka tangu Jumapili. Hao ni Daniel, chifu wa kijiji cha

Diplomasia

“Imekataliwa Kila mahali”: Wakimbizi wa Kongo watishiwa kurejea katika vituo vya usafiri nchini Burundi

SOS Médias Burundi Musenyi, Mei 5, 2026 — Nchini Burundi, hali ya baadhi ya wakimbizi wa Kongo wanaoishi katika eneo la Musenyi katika mkoa wa Burunga, kusini mashariki mwa taifa

Criminalité

Kirundo: Wakaazi wanashutumu michango ya kulazimishwa kwa ukumbusho wa Nkurunziza chini ya shinikizo kutoka kwa Imbonerakure

SOS Médias Burundi Kirundo, Mei 28, 2026 – Siku chache tu kabla ya sherehe rasmi zilizopangwa kufanyika Juni 8, 2026, huko Gitega, mji mkuu wa kisiasa wa Burundi ambako mkuu