Burundi – Rwanda : mke wa rais wa Burundi afanya ziara katika nchi jirani ambayo hadi sasa mumeo apata tabu kutembelea
Nchi ya Rwanda inapokea tangu jumatatu kongamano la sita la kimataifa la ” Women Deliver ” kuhusu usawa wa kijinsia. Mmoja kati ya wageni maluum ni mke wa rais wa Burundi, nchi zamani adui. HABARI SOS Médias Burundi
Kongamano la kimataifa linalozungumzia afya ya akinama, haki na ustaawi wa wasichana na akinamama linafanyika tangu jumatatu ndani ya mji mkuu wa Kigali.
Zaidi ya watetezi wa usawa wa kijinsia elfu 6 wanahudhuria kongamano hilo. Mmoja kati ya wageni wa heshma ni marais kama rais wa Sénégal, Ethiopia na rais wa Hangari pamoja na wake wa ma rais wa nchi mbali mbali kama Burundi , nchi zamani aduwi wa nchi hiyo inayohifadhi kongamano hilo.
Angeline Ndayishimiye alipitia katika mpaka wa ardhini wa Gasenyi-Nemba ( Kaskazini) .
Alilakiwa na mshahuri wa kwanza katika ofisi ya mke wa rais wa Rwanda na badaye kupokelewa rasmi na mke wa rais wa Rwanda Jeannette Kagame mjini Kigali.
” Kuona wake hao wawili wa ma rais wa nchi zamani madui wakipeana zawadi , ni mabadiliko makubwa katika historia ya nchi hizo mbili. Lakini haieleweki pia kuona ni mke wa rais wa Burundi aliyeanza kufanya hatua hiyo kubwa mbele kabla ya mumeo ambaye amechagua kutuma ujumbe mwingi mjini Kigali kabla yake”, ametoa tathimini hiyo raia mmoja wa Burundi mjini Kigali kabla ya kutumai kuwa ” desturi ya ujumbe wa chuki na vita kati ya nchi hizo mbili zilizobadilika hautatolewa tena”.
Mwezi februari 2023, rais wa Rwanda Paul Kagame alitembelea mwenzake wa Burundi ndani ya mji mkuu wa Bujumbura ( mji wa kiuchumi) wakati wa kikao cha 20 cha wakuu wa nchi za EAC kuhusu mzozo mashariki mwa RDC.
” Kigali inasubiri ziara ya kurudishia “.
Nchi hizo mbili ziliamuru kufanya ujirani mwema tangu 2020, wakati Gitega ikiendelea kutuhumu ndugu yake wa Kaskazini kuwapa hifadhi waliofanya jaribio la mapinduzi la mei 2015.
Iwapo Kigali haijawafichua ” madui hao ambao wanatafutwa kwa udi na uvumba na sheria ya Burundi, kengele itasikika hivi karibuni ikizingatiwa ziara hiyo ya viongozi wakuu wa nchi hizo mbili”.
Waziri wa diplomasia wa Burundi hivi karibuni alifahamisha kuwa ” Kigali haitashindilia kwa muda mrefu juu ya kukataa ombi hilo ambalo si faida hata kidogo kwake”.
You might also like
Kayanza: Tani 1,600 za madini zilizosafirishwa nje ya nchi, wabunge wanahoji mwisho wa mapato
SOS Médias Burundi Kayanza, Juni 12, 2026 – Usimamizi wa mapato kutokana na shughuli za uchimbaji madini katika wilaya ya zamani ya Kabarore, ambayo sasa ni sehemu ya tarafa ya
Burundi : nchi imepata mwendeshamashtaka mkuu mpya
Ni Léonard Manirakiza, ameidhinishwa jumanne hii na baraza la seneti. Wanaharakati wanasema kuwa hawataraji mambo makubwa kutoka kwake lakini wameamuru kujizuia kueleza chochote. HABARI SOS Médias Burundi Léonard Manirakiza ameidhinishwa
Burundi: Uzalendo waadhimishwa Gitega huku kukiwa na mivutano ya kisiasa
Hotuba za Umoja wa Kitaifa na mijadala ya utawala tarehe 8 Juni SOS Médias Burundi Buhumuza, Juni 8, 2026 – Sherehe za kuadhimisha Siku ya Kitaifa ya Uzalendo ziliadhimishwa Jumatatu
