Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Ni muili wa mwanamke ambaye hakutambulika. Ulipatikana kwenye mstari wa kutenganisha eneo linalokaliwa na raia wa Kongo na lile wa raia wenye asili ya Burundi. Uchunguzi tayari imeanza ili kutambua aliyefariki. HABARI SOS Médias Burundi

Muili huo ni wa mwanamke wa kati ya miaka 25 na 30, kwa mujibu wa mashahidi. Muili huo uligunduliwa na wapita njia mapema jumatano hii asubuhi.

” Maiti ilikuwa imeanza kuharibika na kutoa harufu mbaya ambayo ilisababisha wapita njia kuangalia. Waliita mara moja polisi ambao walikuja kuchukuwa maiti hiyo. Polisi hiyo iliahidi pia kufanya uchunguzi kwa ajili ya kumutambua muhanga” , walisema wakimbizi.

Muili uliwekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika kijiji cha 3 eneo la raia wenye asili ya Kongo ili kusubiri kipindi cha siku tatu kwa ajili ya kijaribu kutambua muhanga kabla ya mazishi yake yanayotarajiwa wekendi ijayo, kwa mujibu wa viongozi wa kijamii.

Viongozi hao waliitisha mikutano ndani ya kila kijiji ili kuangalia iwapo kuma mtu ambaye atadai kutafuta mtu wake.

Taarifa za kwanza za polisi na viongozi tawala zinasema huenda muhanga ” alinyongwa ” sababu muili wake ulikuwa na majeraha.

Hadi sasa, jina la muhanga, na uraia wake bado kujulikana ikizingatiwa kuwa kambi ya Nyarugusu inawapa hifadhi raia kutoka Burundi pamoja na Kongo wanaokadiriwa kuwa wakimbizi laki moja na elfu 10.

Previous Burundi - Rwanda : mke wa rais wa Burundi afanya ziara katika nchi jirani ambayo hadi sasa mumeo apata tabu kutembelea
Next Burundi : ni budi kuwa makini katika kuwatuma wasichana nchini Saudi Arabia, alisema mke wa rais

You might also like

Wakimbizi

Nyiragongo : hali ya kibinadamu kwenye kituo cha wakimbizi cha adventiste Kasenyi inatisha

Wakimbizi hao wa ndani hawapokei msaada wowote. Ni hali inayozidisha udhaifu wao na hivyo kuwasukuma katika mitaa kuomba omba. Ni tahadhari ya mkuu wa kituo cha adventiste Kasenyi ambaye anazidi

Wakimbizi

Kigoma: Msako wa kuwasaka wakimbizi wa Burundi waingiza kambi na familia katika hofu

SOS Médias Burundi Kigoma, Aprili 8, 2026 — Hali ya wasiwasi inaongezeka kaskazini-magharibi mwa Tanzania. Mamlaka katika mkoa wa Kigoma ambayo ni makazi ya kambi ya Nduta na Nyarugusu, imetangaza

Usalama

Kayogoro : hali ya wasi wasi yawakabili wananchi kutokana na mazoezi ya kijeshi ya Imbonerakure

Imbonerakure, wajumbe wa tawi la vijana wafuasi wa chama tawala, wanafanya mazoezi ya kijeshi hususan usiku. Mazoezi hayo yanafanyika katika vijijini vyote vya tarafa ya Kayogoro katika mkoa wa Makamba