Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Nyarugusu (Tanzania) : maiti ya mwanamke mmoja yapatikana ndani ya shamba

Ni muili wa mwanamke ambaye hakutambulika. Ulipatikana kwenye mstari wa kutenganisha eneo linalokaliwa na raia wa Kongo na lile wa raia wenye asili ya Burundi. Uchunguzi tayari imeanza ili kutambua aliyefariki. HABARI SOS Médias Burundi

Muili huo ni wa mwanamke wa kati ya miaka 25 na 30, kwa mujibu wa mashahidi. Muili huo uligunduliwa na wapita njia mapema jumatano hii asubuhi.

” Maiti ilikuwa imeanza kuharibika na kutoa harufu mbaya ambayo ilisababisha wapita njia kuangalia. Waliita mara moja polisi ambao walikuja kuchukuwa maiti hiyo. Polisi hiyo iliahidi pia kufanya uchunguzi kwa ajili ya kumutambua muhanga” , walisema wakimbizi.

Muili uliwekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika kijiji cha 3 eneo la raia wenye asili ya Kongo ili kusubiri kipindi cha siku tatu kwa ajili ya kijaribu kutambua muhanga kabla ya mazishi yake yanayotarajiwa wekendi ijayo, kwa mujibu wa viongozi wa kijamii.

Viongozi hao waliitisha mikutano ndani ya kila kijiji ili kuangalia iwapo kuma mtu ambaye atadai kutafuta mtu wake.

Taarifa za kwanza za polisi na viongozi tawala zinasema huenda muhanga ” alinyongwa ” sababu muili wake ulikuwa na majeraha.

Hadi sasa, jina la muhanga, na uraia wake bado kujulikana ikizingatiwa kuwa kambi ya Nyarugusu inawapa hifadhi raia kutoka Burundi pamoja na Kongo wanaokadiriwa kuwa wakimbizi laki moja na elfu 10.

Previous Burundi - Rwanda : mke wa rais wa Burundi afanya ziara katika nchi jirani ambayo hadi sasa mumeo apata tabu kutembelea
Next Burundi : ni budi kuwa makini katika kuwatuma wasichana nchini Saudi Arabia, alisema mke wa rais

You might also like

Usalama

Kivu-Kaskazini: sehemu ya kikundi cha Busanza kilichochukuliwa na Uganda?

Wakazi wa kundi la Busanza katika eneo la Rutshuru katika jimbo la Kivu Kaskazini (mashariki mwa DRC) wanasema kuwa Uganda imehamisha alama za mpaka zinazoashiria mpaka kati ya nchi hii

Wakimbizi

Mahama (Rwanda): zaidi ya wakimbizi wapya 2,000 wa Kongo wakaribishwa

Kambi ya Mahama ilipokea zaidi ya wakimbizi 2,000 wapya wa Kongo Jumanne hii kutoka kambi ya usafiri ya Nkamira. Wote wanazungumza Kinyarwanda na wanatoka sehemu ya mashariki ya Kongo. HABARI

Wakimbizi

Tanzania: mamia ya warundi wakamatwa, watoto kumi na watatu wafungwa kwa kudai ujira wao

SOS Médias Burundi Nyamisivya, Juni 9, 2025 — Tangu Februari 28, vijana kumi na watatu wa Burundi wamekuwa wakiteseka katika gereza la Nyamisivya, kaskazini-magharibi mwa Tanzania. “Uhalifu” wao: baada ya