Nyiragongo : hali ya kibinadamu kwenye kituo cha wakimbizi cha adventiste Kasenyi inatisha
Wakimbizi hao wa ndani hawapokei msaada wowote. Ni hali inayozidisha udhaifu wao na hivyo kuwasukuma katika mitaa kuomba omba. Ni tahadhari ya mkuu wa kituo cha adventiste Kasenyi ambaye anazidi kuwa hali yao ya kibinadamu ni mbaya. Viongozi wa kituo hicho wanaomba misaada. Kituo hicho kunapatikana karibu ya mji wa Goma makao makuu ya mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mujibu wa Jean-Claude Nguriye, miezi mingi imemalizika wakimbizi hao wa ndani wakiwa hawana msaada wowote.
Wanalazimika kuingia katika mitaa ili kuomba misaada na hivyo kujiweka katika hatari ya kukumbwa na matatizo mengi zikiwemo ajari za barabarani, mateso na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya akinamama na wasichana wadogo.
” Tuko hapa tangu tarehe 27 oktoba 2022. Hatujapewa msaada wowote. Tunaishi maisha mabaya . Tunaomba omba ili tuweze kupata cha kutafuna. Watu wa roho nzuri wanatupatia chakula lakini wengine wanatutesa. Wakimbizi wengine wanapata ajari za barabarani na wanawake wanabakwa. Wale waliokosa chakula, wanarudi nyuma na kulala tumbo ikiwa haina kitu”, anaeleza mkuu wa kituo hicho.
Ili kujiepusha na mabaya zaidi, kiongozi wa kituo cha adventiste cha Kasenyi anaomba misaada kutoka kwa mashariki ya kiutu na serikali na kurejea kwa amani ndani ya eneo hilo.
Kituo cha wakimbizi cha adventiste Kasenyi tayari kiliorodhesa vifo vya watu wanne kutokana na njaa pamoja na matatizo mengine kama uhaba wa maji na kujaa kwa vyoo.
Zaidi ya watu 100000 walitoroka makaazi yao na ma kumi ya wengine kuuwawa katika mashambulizi ya vikundi vya silaha ndani ya mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo ( DRC) kwa mjibu wa ripoti ya shirika la umoja wa mataifa UN mwanzoni mwa mwezi machi.
You might also like
Kigali: Wakfu wa Maggy Barankitse sasa unafanya kazi nchini Rwanda
Baada ya Marekani na Ubelgiji, Taasisi ya Maggy Barankitse sasa itaanza kufanya kazi nchini Rwanda. Tangazo hilo lilitolewa Jumatatu Machi 24 wakati wa jioni ya kirafiki iliyoandaliwa katika makao makuu
Picha ya wiki:ukosefu mkubwa wa maji ya kunywa katika kambi la wakimbizi wa warundi ya Nduta
Kuna ongezeko la uhaba wa maji ya kunywa katika kambi ya Nduta nchini Tanzania. Wakimbizi wanaogopa magonjwa kutoka kwa mikono michafu. HABARI SOS Médias Burundi Maeneo yaliyoathirika zaidi ni yale
Burundi: hakuna fedha zaidi za kufadhili masomo ya chuo kikuu ya wanafunzi wakimbizi na wanaorejea
Wakimbizi vijana na waliorejea walio na digrii nchini Burundi wanakabiliwa na kutopatikana kwa fedha za ufadhili wa masomo wa DAFI. Hii inahusu mwaka wa masomo wa 2024-2025. Matumaini ya vijana
