Burundi : bei ya tiketi ya usafiri yapanda

Burundi : bei ya tiketi ya usafiri yapanda

Waziri wa biashara alitangaza jumatano hii bei mpya na nauli ya usafiri ndani ya mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura na katika ya mikoa. Bei ya tiketi ndani basi mjini Bujumbura popote pale unapotoka na kuelekea kati kati mwa mji ilipandishwa franka 50 sarafu za Burundi. Kati kati mwa nchi nauli itapanda kwa franka 500. HABARI SOS Médias Burundi

Waziri Marie Chantal Nijimbere alifahamisha kupitia tangazo kuwa bei ya nauli za usafiri ilipandishwa kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta ya gari tangu jumatatu hii.

Wakaazi wa jiji la Bujumbura walibaini kuwa walitaraji ongezeko hilo la bei ya tiketi litatokea.

” Bila shaka na bei ya vyakula na bidhaa zingine mahitajio muhimu zitapanda”. wanalaani wakaazi wengine ambao wanazidi kuwa walitupiliwa “.

Wengine wanasema kuwa hawaelewi malengo ya serikali. Wafanyakazi wa umma wanasema kuwa serikali inalenga kukusanya pesa iliyotumia katika kutekeleza sera ya kusawazisha mishahara iliyoanza kutelelezwa tangu julai iliyopita”.

” Bei ya bidhaa muhimu itapanda pia kwa mkondo huo”, wanalaani wafanyakazi wa serikali.

Bei ya tiketi ya usafiri ilipanda mara ya mwisho katika mwezi julai iliyopita.

Hatua hiyo ilisababisha bei ya bidhaa zingine kama sukari, simenti na vinywaji kupanda licha ya kuendelea kuadimika kwenye soko nchini Burundi.

Previous DRC (Uvira) wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi wakamatwa kwa jaribio la mauwaji
Next Gihanga : bibi kizee wa zaidi ya miaka sabini auwawa

You might also like

DRC Sw

Uvira: Burundi na DRC wanataka kurahisisha taratibu kwa wafanyabiashara wanaovuka mpaka

Majirani hao wawili katika eneo la Maziwa Makuu barani Afrika wamezindua mpango unaolenga kupunguza taratibu zilizowekwa kwa wafanyabiashara wa mipakani. Ni programu inayoungwa mkono na Soko la Pamoja la Mashariki

Uchumi

Bujumbura: kukamatwa na kufuatiwa na kuwekwa kizuizini kwa maafisa wa kampuni ya kibiashara na utengenezaji

Meneja mkuu wa kampuni ya biashara na utengenezaji bidhaa iliyoko Bujumbura, jiji la kibiashara la Burundi, na msaidizi wake wamekuwa wapangaji wa gereza kuu la Bujumbura linalojulikana kwa jina la

Uchumi

Gitega: bei imekuwa ngumu kumudu

Familia kadhaa katika mji wa Gitega (mji mkuu wa kisiasa) haziwezi kuhudhuria soko la Krismasi na Mwaka Mpya. Bidhaa zote zimeona ongezeko la bei kupita kiasi, na kuwaacha wakaazi wasiweze