Kakuma (Kenya) : maradhi ya usafi mdogo yatishia waomba hifadhi
Maradhi ya usanifishaji mdogo yanashuhudiwa kwenye kituo cha mapokezi ya waomba hifadhi ndani ya kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya . Kituo kicho kimeathirika zaidi kutokana na msongamano wa watu na udogo wa eneo hilo. Msimu wa mvua ulikuja kuhatarisha mazingira. HABARI SOS Médias Burundi
Kituo cha mapokezi katika kambi ya Kakuma kaskazini magharibi mwa Kenya kimezidiwa na idadi kubwa ya waomba hifadhi. Maradhi yanayotokana na usafi mdogo yanaanza kushuhudiwa.
” Kituo kicho kinachopatikana katika maeneo ya viillage ya Kakuma III kimeathiriwa pakubwa sababu kinahifadhi zaidi ya watu elfu tatu katika maeneo madogo yaliyoandaliwa ili kupokea watu. Kufuatia mvua nyingi inayonyesha katika kanda ya Turkana mnamo siku hizi, vyoo viliharibika”, alisikitika mfanyakazi wa kujitolea wa HCR.
Katika eneo la Kalobeyei ambako kuna kituo cha kupanua kambi ya Turkana, vituo vitatu vipya vilifunguliwa.
” Eneo hilo pia ni hali kadhalika na mazingira ya maisha yanafanana. Kadiri watu wanakuwa wengi, ndivyo wanavyokosa maji safi, na hivyo maradhi ya usanifishaji mdogo huingia na kushambulia hasa watoto “, walisisitiza wadau eneo hilo.
Waomba hifadhi wapya katika kambi ya Kakuma kwa sehemu kubwa ni wenye asili ya nchi ya DRC, Somalia na Sudan kusini. Kwa hao, wanajumulika pia wale kutoka Burundi walitoroka kambi za wakimbizi nchini Tanzania na Uganda wakitafuta mazingira mazuri ya maisha kwa mjibu wao.
Wanaomba HCR kuharakisha mchakato wa kuwapa hadhi ya ukimbizi ili waweze kuingia katika village na Blocs za kambi.
Wakimbizi wengine upande wao waliomba HCR kuweka pembeni wagonjwa ambao tayari walipatikana na ugonjwa wa kuharisha ili kuthibiti mambukizi ndani ya kambi hiyo inayowapa hifadhi watu zaidi ya laki mbili wakiwemo warundi elfu 25.
You might also like
Nakivale (Uganda): mapambano dhidi ya ujenzi wa ghasia uliochafuliwa na ufisadi
Afisa mkuu kutoka wizara ya Uganda inayosimamia wakimbizi anashutumiwa nao kwa kuharibu nyumba zinazoendelea kujengwa katika kambi ya Nakivale, kwa kisingizio cha kupigana dhidi ya ujenzi usiodhibitiwa. Kulingana na wakimbizi,
Kulazimishwa kurejeshwa makwao kwa zaidi ya wakimbizi 80,000 wa Burundi: Wasiwasi na kutokuelewana ndani ya taasisi za Burundi.
SOS Médias Burundi Ngozi, Novemba 30, 2025 – Tangazo la kulazimishwa kuwarejesha makwao zaidi ya wakimbizi 80,000 wa Burundi wanaoishi Tanzania linaendelea kuibua wasiwasi mkubwa miongoni mwa watetezi wa haki
Nyarugusu (Tanzania) : misaada yasimamishwa kwa wakimbizi zaidi ya 200 wenye uraia wa Burundi wanaotembea na ulemavu
Idadi kubwa ya wakimbizi wenye uraia wa Burundi wanaoishi na ulemavu hawakupata msaada wao wa mkaa. Zaidi ya 200 kati yao hawakuona majina yao kwenye orodha ya wanaohitaji misaada. Wanakosoa
