DRC – Rutshuru : usalama wazidi kuwa mbaya katika kitongoji cha Busanza
Wakaazi wa kitongoji cha Busanza ndani ya kijiji cha Bwisha wilayani Rutshuru mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo walaani kuona visa vya usalama mdogo vikiendelea kushuhudiwa mnamo siku hizi katika baadhi ya maeneo ambako kunaripotiwa waasi wa M23 na makundi ya silaha ya ndani. Vyanzo mbali mbali vinasema kuwa uwepo wa makundi hayo mawili yanayozozana, huchangia katika kuleta hali ya usalama mdogo ndani ya maeneo hayo. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mujibu wa vyanzo eneo hilo, mapigano kati ya kundi la M23 na makundi ya silaha na waasi eneo hilo yanafanyika takriban kila siku. Baadhi ya wananchi hukimbia na kwenda nchini Uganda wakati wengine wakielekea kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.
” Kutokana na hali hiyo, shughuli za kijamii na kiuchumi zilisimama tangu miezi kadhaa. Mbali na hayo, maeneo hasa ya : Ruharashi, Kaitorea, Changwi, Kitagoma na Kavugizo yanaathiriwa zaidi na visa vya ubakaji, wizi wa mali, utekaji nyara dhidi ya wananchi. Wakimbizi wa ndani ” wanadai kuwa serikali ya Kongo iliwasahau “.
Wakimbizi hao wanaoishi kwenye mpaka baina ya Kongo na Uganda wanaomba viongozi wenye nguvu kuhusishwa ili amani iweze kurudi katika maeneo hayo ya mkoa wa Kivu kaskazini.
You might also like
Bukavu: Banyamulenge wanaendelea kuwa wahanga wa kunyanyaswa na Wazalendo
Bukavu, Juni 12, 2025 – Ghasia mpya ziliripotiwa Jumatano hii katika eneo la Uvira, Kivu Kusini, mashariki mwa Kongo. Maafisa wa polisi wa Banyamulenge, walimu, na wanawake waliokuwa wakisafiri kwenda
Goma: karibu wakazi 25,000 walifukuzwa kutoka kwa nyumba zao
Takriban wakazi 25,000 wa maeneo tofauti katika kikundi cha Bambo katika eneo la Rutshuru wamefukuzwa kutoka kwa nyumba zao tangu wiki iliyopita. Iko katika mkoa wa Kivu Kaskazini mashariki mwa
Nyarugusu (Tanzania) : wakimbizi wawili kutoka Burundi wakufa kutokana na na maji ya mvua
Mvua kubwa zilizonyesha katika mkoa wa Kigoma (kaskazini magharibi mwa Tanzania) ambako kunapatikana kambi ya Nyarugusu nchini Tanzania zilisababisha vifo vya watu. Nyumba nyingi zilibomoka. Angalau wakimbizi wawili walifariki baada
