DRC – Rutshuru : usalama wazidi kuwa mbaya katika kitongoji cha Busanza
Wakaazi wa kitongoji cha Busanza ndani ya kijiji cha Bwisha wilayani Rutshuru mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo walaani kuona visa vya usalama mdogo vikiendelea kushuhudiwa mnamo siku hizi katika baadhi ya maeneo ambako kunaripotiwa waasi wa M23 na makundi ya silaha ya ndani. Vyanzo mbali mbali vinasema kuwa uwepo wa makundi hayo mawili yanayozozana, huchangia katika kuleta hali ya usalama mdogo ndani ya maeneo hayo. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mujibu wa vyanzo eneo hilo, mapigano kati ya kundi la M23 na makundi ya silaha na waasi eneo hilo yanafanyika takriban kila siku. Baadhi ya wananchi hukimbia na kwenda nchini Uganda wakati wengine wakielekea kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.
” Kutokana na hali hiyo, shughuli za kijamii na kiuchumi zilisimama tangu miezi kadhaa. Mbali na hayo, maeneo hasa ya : Ruharashi, Kaitorea, Changwi, Kitagoma na Kavugizo yanaathiriwa zaidi na visa vya ubakaji, wizi wa mali, utekaji nyara dhidi ya wananchi. Wakimbizi wa ndani ” wanadai kuwa serikali ya Kongo iliwasahau “.
Wakimbizi hao wanaoishi kwenye mpaka baina ya Kongo na Uganda wanaomba viongozi wenye nguvu kuhusishwa ili amani iweze kurudi katika maeneo hayo ya mkoa wa Kivu kaskazini.
You might also like
Goma: kuanza tena kwa mapigano makali kati ya M23 na jeshi la Kongo linaloungwa mkono na wanamgambo wa ndani
Takriban watu kumi waliuawa Jumatatu hii katika eneo la kichifu la Bashali katika uhasama kati ya waasi wa M23 na jeshi la Kongo linaloungwa mkono na wanamgambo wa ndani wanaodumishwa
Burundi: Mamlaka za Burundi zinakaribisha viongozi wa FLN na FDLR-pariah kutoka kanda ndogo
Kwa zaidi ya wiki moja, kumekuwa na taarifa za kuwepo kwa viongozi wa FLN (National Liberation Front) na FDLR (Democratic Forces for the Liberation of Rwanda) katika ardhi ya Burundi.
DRC: Wanajeshi wa Burundi wauawa – vita siri, bila fidia au ukweli
SOS Médias Burundi Bujumbura, Januari 4, 2026 – Wakati mamlaka ya Burundi ikiendelea kuhalalisha uwepo wa jeshi la Burundi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kupitia madai ya “mshikamano
