DRC – Rutshuru : usalama wazidi kuwa mbaya katika kitongoji cha Busanza
Wakaazi wa kitongoji cha Busanza ndani ya kijiji cha Bwisha wilayani Rutshuru mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo walaani kuona visa vya usalama mdogo vikiendelea kushuhudiwa mnamo siku hizi katika baadhi ya maeneo ambako kunaripotiwa waasi wa M23 na makundi ya silaha ya ndani. Vyanzo mbali mbali vinasema kuwa uwepo wa makundi hayo mawili yanayozozana, huchangia katika kuleta hali ya usalama mdogo ndani ya maeneo hayo. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mujibu wa vyanzo eneo hilo, mapigano kati ya kundi la M23 na makundi ya silaha na waasi eneo hilo yanafanyika takriban kila siku. Baadhi ya wananchi hukimbia na kwenda nchini Uganda wakati wengine wakielekea kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.
” Kutokana na hali hiyo, shughuli za kijamii na kiuchumi zilisimama tangu miezi kadhaa. Mbali na hayo, maeneo hasa ya : Ruharashi, Kaitorea, Changwi, Kitagoma na Kavugizo yanaathiriwa zaidi na visa vya ubakaji, wizi wa mali, utekaji nyara dhidi ya wananchi. Wakimbizi wa ndani ” wanadai kuwa serikali ya Kongo iliwasahau “.
Wakimbizi hao wanaoishi kwenye mpaka baina ya Kongo na Uganda wanaomba viongozi wenye nguvu kuhusishwa ili amani iweze kurudi katika maeneo hayo ya mkoa wa Kivu kaskazini.
You might also like
Uvira chini ya mvutano: mgomo wa jumla, vurugu, na kukataliwa kwa Jenerali Gasita katika jiji la kimkakati karibu na mlipuko.
SOS Médias Burundi Bukavu, Septemba 7, 2025—Kwa muda wa wiki moja iliyopita, jiji la Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, limekuwa likikumbwa na mgomo wa jumla unaodhoofisha na
Kirundo: vitisho vya kifo dhidi ya wale wanaopinga michango ya kulazimishwa katika wilaya ya Ntega
Wakaazi wa eneo la Murungurira, katika wilaya ya Ntega, ambao hawajakubali kulipa mchango unaodaiwa na msimamizi wa jumuiya hiyo na katibu wa jumuiya wa chama cha CNDD-FDD wote wanatishiwa kuuawa.
DRC: Mashambulio ya mabomu, mivutano ya kijeshi, na mashindano ya kikanda katika kiini cha mapigano ya muda mrefu mashariki mwa nchi.
SOS Médias Burundi Bukavu, Machi 22, 2026 – Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wimbi jipya la shutuma za milipuko ya mabomu inayolenga raia linazidisha hali ya wasiwasi katika
