Mebeba (Zambia) : HCR inakwenda kinyume na haki kuwazika wakimbizi

Mebeba (Zambia) : HCR inakwenda kinyume na haki kuwazika wakimbizi

Tangu muda mchache , HCR haotowi misaada kwa ajili ya mazishi kama ilivyokuwa kawaida. Wakimbizi wanaodai kuishi Katika mazingira magumu wanaomba shirika hilo la umoja wa mataifa kurejelea hatua hiyo. HABARI SOS Medias Burundi

Kisa cha hivi karibuni ni kile cha mkimbizi aliyefariki siku chache zilizopita. Familia ilimufanyia mazishi mjumbe wao katika mazingira magumu kutokana na uwezo mdogo.

” Mazishi ya Innocent mwenye asili ya mkoa wa Gitega ( kati kati mwa Burundi) yaliwagusa wote isipokuwa tu HCR. Raia huyo wa Burundi kwanza alikufa kwa sababu ya uzembe wa wauguzi katika kambi ya Meheba D Clinic. Harafu HCR haikufanya chochote ili kumuzika kwa heshma . Tulijipanga lakini hatuna uwezo wa kutosha, juhudi zetu hazikuweza kukidhi mahitaji ya mazishi ya heshma “, wanaeleza wakimbizi wa Burundi.

Na kulaaani : ” kawaida, HCR ingetakiwa kutuazima gari ya kusafirisha maiti, kutoa sandugu na kununua mashuka na blanketi, yaani vitu vya msingi. Lakini haikufanya chochote.

Huduma mbaya ya matibabu

Kwenye kituo cha afya kinasimamiwa na HCR eneo la Meheba ambalo kinakabiliwa na msongamano mkubwa, huduma za matibabu ni mbaya.

” Hakika, bora kliniki hiyo ifungwe sababu haitusaidii kitu. Kawaida ingetakiwa kuwa ya umma lakini inawapokea chini ya watu kumi wanaolazwa kwa miezi mitatu. Haileweki ! Mwishoni mwa wiki, wauguzi hawafanyi kazi, tunajiuliza iwapo na wagonjwa wanachukuwa likizo ! wakimbizi wa kambi ya Meheba wanasema.

Kwa mjibu wa vyanzo hivyo, kliniki hiyo pia inakosa madawa.

” ina na vidonge vya paracétamol hata waliojeruhiwa au mgonjwa anayesumbuliwa na matatizo yoyote anapewa kidonge hicho. Tulifahamu kuwa madawa yaliuzishwa “

Wakimbizi wana hasira dhidi ya HCR. Wanaomba shirika hilo la umoja wa mataifa na serikali ya Zambia kubadili mwenendo na kuhakikisha ulinzi wa wakimbizi katika nyanja zote.

Kambi ya Meheba ina zaidi ya wakimbizi elfu 27 wakiwemo warundi elfu tatu wenye asili ya Burundi

Previous Kesi-Bunyoni : sheria nchini Burundi yafunga akaunti za waziri mkuu wa zamani
Next Burundi : Imbonerakure zapewa sifa na kuhitajiwa

You might also like

Wakimbizi

Nakivale (Uganda): Benki ya Dunia inaunga mkono uwezeshaji wa kina mama wakimbizi

Nakivale (Uganda): Benki ya Dunia inaunga mkono uwezeshaji wa kina mama wakimbizi SOS Médias Burundi Nakivale, Mei 8, 2025 – Benki ya Dunia imezindua mradi katika kambi ya Nakivale, Uganda,

Wakimbizi

Tanzania: Kuongezeka kwa uhalifu kuzunguka kambi ya Nduta, wakimbizi wa Burundi wahusika

SOS Médias Burundi Nduta, Julai 14, 2025 – Msururu wa mashambulizi makali katika siku za hivi majuzi katika kambi ya wakimbizi ya Nduta kaskazini-magharibi mwa Tanzania yanazua wasiwasi miongoni mwa

Wakimbizi

Bwagiriza: kutoweka kwa mkimbizi wa Kongo

Tabaro Jean Bosco, mkimbizi kutoka kambi ya Bwagiriza, aliripotiwa kutoweka Jumatatu hii, Machi 31, 2025. Akiwa mjini Bujumbura, jiji la kibiashara la Burundi ambako alifanya kazi ili kukidhi mahitaji ya