Kivu-Kaskazini: mashirika ya kujitolea ya ndani yanatahadharisha juu ya mazingira mabaya ya maisha ya waliokimbia vita ya Rutshuru
Shirika la shughuli za kijamii kwa ajili ya maendeleo ya wote ASDI- RDC hivi karibuni lilifanya ziara kwenye kituo cha wakimbizi wa ndani eneo la Rwasa 2 katika wilaya ya Rutshuru. Ni katika mkoa wa kivu kaskazini mashariki mwa DRC. Katika ziara hiyo shirika hilo linafahamisha kuwa lilishuhudia kuwa wakimbizi hao wanaishi katika mazingira mabaya tangu vita kati ya jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo na waasi wa kundi la M23 kuanza. HABARI SOS Médias Burundi
Viongozi wa shirika hilo la ASDI-RDC wanathibitisha kuwa wakimbizi hao hawana chochote.
” Dharura kwa waathiriwa hao ni kuwapa msaada wa chakula, matibabu, elimu na wa kiusalama” walisema hayo.
Kituo cha Rwasa 2 kinawapa hifadhi takriban familia elfu saba. Ni wakimbizi wa vita na wakimbizi raia wa Kongo waliofurushwa kutoka Uganda.
” Tuko kwenye hatua ya kukadiria mahitaji ya wakimbizi hao wa ndani. Ni zoezi la msingi linalotuwezesha kujuwa aina ya mahitaji muhimu ya watu hao. Kwa wakati baada ya kujuwa mahitaji yao na misaada iliyotolewa na mashirika mengine ya kihisani, sasa tunatathimini njia yetu ya kuwahudumia”, alifahamisha kiongozi wa shirika hilo na kuwaombea msaada kwa serikali, mashirika mengine ya kihisani na kila mtu mwenye nia ya kuwasaidia wakimbizi wa vita.
Tangu miezi mitatu iliyopita, hali ya usalama na kiutu imesalia kuwa ya kusikitisha katika maeneo mengi ya Bwisha wilaya ya Rutshuru, kivu ya kaskazini.
Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, ma elfu ya wakimbizi wa ndani waliotoroka mapigano kati ya jeshi la FARDC na waasi wa kundi la M23 katika wilaya ya Rutshuru, wanaishi katika mazingira mabaya ndani ya vituo vya wakimbizi na familia zilizowapokea.
Kundi la M23 linadhibiti mji wa mpakani wa Bunagana tangu miezi mitatu iliyopita. Mapigano makali yaliyoibuka wiki moja iliyopita yalipelekea ma elfu ya wakaazi wengine kutoroka makaazi yao. Baadhi walielekea nchini Uganda na tayari walitumwa katika kambi ya Nakivale, mbali na mpaka.
You might also like
Rwanda-DRC: Congolese fighter plane once again violated Rwandan airspace
The Rwandan government has announced that its airspace has been violated by a DRC (Democratic Republic of Congo) fighter plane. The Rwandan authorities describe the incident as “provocations” which go
Gasorwe: mufuasi wa chama cha CNL atekwa nyara
Viateur Nzigo, mufuasi wa chama cha CNL (kongamano la kitaifa kwa ajili ya uhuru) alitekwa nyara kutoka nyumbani kwake tarafani Gasorwe mkoa wa Muyinga (kaskazini mwa Burundi) asubuhi ya jumatano
Masisi: the rebellion next to the guarantor of world peace
The M23 rebels who took control of the city of Kithanga in the territory of Masisi, in the province of North Kivu eastern DRC, have installed new positions to secure
