Kivu-Kaskazini: mashirika ya kujitolea ya ndani yanatahadharisha juu ya mazingira mabaya ya maisha ya waliokimbia vita ya Rutshuru
Shirika la shughuli za kijamii kwa ajili ya maendeleo ya wote ASDI- RDC hivi karibuni lilifanya ziara kwenye kituo cha wakimbizi wa ndani eneo la Rwasa 2 katika wilaya ya Rutshuru. Ni katika mkoa wa kivu kaskazini mashariki mwa DRC. Katika ziara hiyo shirika hilo linafahamisha kuwa lilishuhudia kuwa wakimbizi hao wanaishi katika mazingira mabaya tangu vita kati ya jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo na waasi wa kundi la M23 kuanza. HABARI SOS Médias Burundi
Viongozi wa shirika hilo la ASDI-RDC wanathibitisha kuwa wakimbizi hao hawana chochote.
” Dharura kwa waathiriwa hao ni kuwapa msaada wa chakula, matibabu, elimu na wa kiusalama” walisema hayo.
Kituo cha Rwasa 2 kinawapa hifadhi takriban familia elfu saba. Ni wakimbizi wa vita na wakimbizi raia wa Kongo waliofurushwa kutoka Uganda.
” Tuko kwenye hatua ya kukadiria mahitaji ya wakimbizi hao wa ndani. Ni zoezi la msingi linalotuwezesha kujuwa aina ya mahitaji muhimu ya watu hao. Kwa wakati baada ya kujuwa mahitaji yao na misaada iliyotolewa na mashirika mengine ya kihisani, sasa tunatathimini njia yetu ya kuwahudumia”, alifahamisha kiongozi wa shirika hilo na kuwaombea msaada kwa serikali, mashirika mengine ya kihisani na kila mtu mwenye nia ya kuwasaidia wakimbizi wa vita.
Tangu miezi mitatu iliyopita, hali ya usalama na kiutu imesalia kuwa ya kusikitisha katika maeneo mengi ya Bwisha wilaya ya Rutshuru, kivu ya kaskazini.
Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, ma elfu ya wakimbizi wa ndani waliotoroka mapigano kati ya jeshi la FARDC na waasi wa kundi la M23 katika wilaya ya Rutshuru, wanaishi katika mazingira mabaya ndani ya vituo vya wakimbizi na familia zilizowapokea.
Kundi la M23 linadhibiti mji wa mpakani wa Bunagana tangu miezi mitatu iliyopita. Mapigano makali yaliyoibuka wiki moja iliyopita yalipelekea ma elfu ya wakaazi wengine kutoroka makaazi yao. Baadhi walielekea nchini Uganda na tayari walitumwa katika kambi ya Nakivale, mbali na mpaka.
You might also like
Beni: several Christians killed in a bomb explosion
Another bloody attack occurred this Sunday in the territory of Beni, in the city of Kasindi, bordering Uganda, in the province of North Kivu, eastern DRC. Several people (all Christians)
Nairobi: the protagonists in the Congolese crisis meet without the M23
Since Monday, November 28, a meeting is talking place in Nairobi, for six days without the M23, to deal with the Congolese crisis. The M23, a rebel movement which seized
Musasa – Kinama : refugees elect their representatives in a context of crisis
In the Musasa and Kinama refugee camps, respectively in the Ngozi and Muyinga provinces (north and northeast Burundi), refugees, mostly Congolese, elected their representatives on September 26, 2024. These elections
