Bururi : gereza limezidiwa na idadi kubwa ya wafungwa
Gereza la Bururi (kusini mwa Burundi) linawahidhi wafungwa ambao wanazidi uwezo wake kwa mjibu wa vyanzo katika idara ya magereza. Inawapa hifadhi watu 383 wakati uwezo wake hauzidi watu 250. HABARI SOS Médias Burundi
Viongozi wa idara ya magereza wanasema mazingira gerezani ni mabaya. Waziri wa sheria analaani kuona kuna watu wanaozuiliwa jela wakati hawatakiwi kukaa jela. Anaomba mahakama kuwajibika ili kupunguza msongamano katika magereza.
Msongamano katika magereza mkoani Bururi unathibitishwa na vyanzo vya wizara ya sheria, watetezi wa ndani wa haki za binadamu na watu wa karibu ya wafungwa.
” Gereza ambalo lina uwezo wa kuwapokea watu 250 sasa linawapa hifadhi wafungwa 383. Hali hiyo inasababisha mazingira mabaya gerezani, wanasema.
Kulingana na vyanzo, gereza lina wafungwa 117 waliokatiwa kesi, wanaosalia wote bado ni watuhumiwa.
Bururi na katika magereza mengine nchini, msongamano wa wafungwa ni changamoto kubwa ambayo inasababisha hasara kubwa kwa serikali, kulingana wa waziri wa sheria.
“[….] Kuanzia malaazi, chakula na huduma za afya, hayo yote yanagharimu kitita kikubwa serikali […] alifamisha Domine Banyankimbona katika tamko lake la tarehe 31 oktoba.
Anawaomba kujirekebisha wadau wa sheria na majaji wanaosababisha ongezeko la wafungwa magerezani kwa kuwatuma gerezani watu waliofanya ” makosa madogo”.
Domine Banyankimbona anaomba majaji kushughulikia kwa makini faili za makosa madogo na zile za watu ambao kesi zao hazijakatwa.
You might also like
Karusi: a man admitted after being stabbed by an Imbonerakure
Prosper Bitangayezu was seriously injured in the abdomen stermming from a stabbing by an Imbonerakure (member of the CNDD-FDD youth league, the presidential party). The incident took place on the
Crisis in eastern Congo : a blue helmet killed and another seriously injured in an attack against a Monusco plane
The Monusco (Mission of the United Nations organization in the DRC) announced the death of its blue helmet in a press release. It informs that he died following an attack
Geneva : the term of the UN Special Rapporteur on the situation of human rights in Burundi renewed
The vote took place on Thursday. Of the 47 states that make up the Council, 22 voted in favor of the reappointment of Fortuné Gaétan Zongo. Burundian authorities had not
