Bururi : gereza limezidiwa na idadi kubwa ya wafungwa

Bururi : gereza limezidiwa na idadi kubwa ya wafungwa

Gereza la Bururi (kusini mwa Burundi) linawahidhi wafungwa ambao wanazidi uwezo wake kwa mjibu wa vyanzo katika idara ya magereza. Inawapa hifadhi watu 383 wakati uwezo wake hauzidi watu 250. HABARI SOS Médias Burundi

Viongozi wa idara ya magereza wanasema mazingira gerezani ni mabaya. Waziri wa sheria analaani kuona kuna watu wanaozuiliwa jela wakati hawatakiwi kukaa jela. Anaomba mahakama kuwajibika ili kupunguza msongamano katika magereza.

Msongamano katika magereza mkoani Bururi unathibitishwa na vyanzo vya wizara ya sheria, watetezi wa ndani wa haki za binadamu na watu wa karibu ya wafungwa.

” Gereza ambalo lina uwezo wa kuwapokea watu 250 sasa linawapa hifadhi wafungwa 383. Hali hiyo inasababisha mazingira mabaya gerezani, wanasema.

Kulingana na vyanzo, gereza lina wafungwa 117 waliokatiwa kesi, wanaosalia wote bado ni watuhumiwa.

Bururi na katika magereza mengine nchini, msongamano wa wafungwa ni changamoto kubwa ambayo inasababisha hasara kubwa kwa serikali, kulingana wa waziri wa sheria.

“[….] Kuanzia malaazi, chakula na huduma za afya, hayo yote yanagharimu kitita kikubwa serikali […] alifamisha Domine Banyankimbona katika tamko lake la tarehe 31 oktoba.

Anawaomba kujirekebisha wadau wa sheria na majaji wanaosababisha ongezeko la wafungwa magerezani kwa kuwatuma gerezani watu waliofanya ” makosa madogo”.

Domine Banyankimbona anaomba majaji kushughulikia kwa makini faili za makosa madogo na zile za watu ambao kesi zao hazijakatwa.

Previous Bururi: prison house overcrowded
Next Lusenda: Burundian refugees asked not to leave the camp

You might also like

Human Rights

Burundi: the relegation of the CNIDH to B status undermines its credibility

The Independent National Human Rights Commission in Burundi, CNIDH, has once again lost its “A” status reserved for National Commissions which have proven their impartiality in relation to the powers

Human Rights

Burundi : Burundian President pardoned journalist Floriane Irangabiye

This presidential pardon measure was issued on August 14, according to a decree signed by President Évariste Ndayishimiye. Floriane Irangabiye was serving a 10-year jail. INFO SOS Médias Burundi According

Human Rights

Nakivale (Uganda) : humanitarian aid for malnourished children suspended

The UNHCR has temporarily suspended its assistance to malnourished children and pregnant women. The measure follows the decree of the U.S. president who ordered the suspension of foreign aid programs.