Ntega : wanawake tisa waliuwawa na waume zao kwa kipindi cha mwaka mmoja
Wakaazi wa tarafa ya Ntega mkoani Kirundo (kaskazini mwa Burundi) waliomba adhabu ya kunyongwa iweze kurudishwa kwa ajili ya kushughulikia watu wote wanaofanya mauwaji. Ombi hilo limejiri baada ya mauwaji ya mwanamke mmoja mkaazi wa kijiji cha Monge, mauwaji yaliyotokea januari tarehe 23. Angalau wanawake tisa waliuwawa na waume zao katika tarafa hiyo kati ya januari 2022 na januari 2023. HABARI SOS Médias Burundi
Katika mkutano wa gavana wa mkoa wa Kirundo siku ya alhamisi iliyopita, wakaazi wa tarafa ya Ntega walijieleza kuhusu visa vya mauwaji vilivyoripotiwa katika miezi iliyopita ndani ya eneo hilo.
Akinama tisa waliuwawa na waume zao tangu mwaka wa 2022. Kisa cha hivi karibuni kilitokea siku ya jumatatu iliyopita. Askali jeshi wa Burundi Pascal Bizimana mwenye cheo cha koporo alimuuwa mkeo.
Mahakama ya mkoa wa Kirundo ilimkatia adhabu ya kifungo cha maisha gerezani. Alitakiwa pia kulipa faini ya franka za Burundi milioni 25 kwa familia ya mkeo kama fidia.
Siku nane badaye, maiti ya mwanamke mwingine kwa jina la Sandrine Nibigira mwenye umri wa miaka takriban 30 iliogotwa. Mume wake ambaye anatuhumiwa mauwaji hayo ya mkeo, alitoroka maeneo ya Musumba ambako alikuwa anaishi. Polisi inafahamisha kuwa iko mbioni kumtafuta. Akimama hao wawili waliouwawa katika mwezi januari wanaongeza idadi ya wengine sita waliouwawa na waume zao pia katika mwaka wa 2022 kwa mjibu wa vyanzo katika utawala.
Wakaazi wa tarafa ya Ntega waliomba ” auwawe mara moja mtu yoyote anayefanya mauwaji”.
Wanasema kusikitika na kuona wahalifu wakiachiliwa huru kutoka jela kutokana na rushwa inayokabili sekta ya sheria.
” Sehemu kubwa ya visa vya uhalifu vinavyofanyika hutokana na hali ya kutoadhibu”, alisisitiza mwanamke mmoja katika viongozi wa tarafa hiyo.
Viongozi wa ndani wanakosoa mfumo wa sheria.
” Mahakama ya Kirundo inakabiliwa na rushwa” alilaani hadharani kiongozi mmoja.
Gavana wa mkoa wa Kirundo Albert Hatungimana anafafanua kuwa adhabu ya kunyongwa haiwezi kutekelezwa. Katiba ya Burundi iliondoa adhabu hiyo.
Asilimia 98 ya wakaazi wa tarafa ya Ntega waliohudhuria mkutano huo walichagua kwa kupandisha mikono irudishwe adhabu ya kuuwawa dhidi ya watu waliotekeleza mauwaji .
You might also like
Burunga : CNIDH calls attention to detention abuses and judicial pressure
SOS Médias Burundi Burunga, August 23, 2025 – The National Independent Human Rights Commission (CNIDH) is sounding the alarm : many citizens are spending long months in detention without any
Tanzania: authorities raise refugees’ awareness on the respect of the laws they constantly violate
Two weeks devoted to the sensitization on the national legislation and provisions governing refugees, in the Nduta and Nyarugusu camps. Refugees find that they are protected by good legislation, which
Rumonge : concern after two cases of sexual violence against minors in Buruhukiro
SOS Médias Burundi Rumonge, May 20, 2026 — Parents and child rights advocates in the district of Rumonge, in Burunga province in southwestern Burundi, are expressing grave concern over the
