Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Muili wa Gilbert Ndacayisaba mwenye umri wa miaka 47 ulipatikana katika shamba la miti ya mikaratusi alhamisi mchana. Mkaazi huyo wa kijiji cha Karungura tarafani Mwumba mkoa wa Ngozi (Kaskazini mwa Burundi), alikuwa mmoja kati ya viongozi wa chama hicho cha upinzani katika eneo hilo. Watu wake wa karibu wanadai kuwa huenda aliuwawa na Imbonerakure (wajumbe wa tawi la vijana wa chama cha CNDD-FDD). Wawili kati ya Imbonerakure wanne wanaotuhumiwa mauwaji hayo walikamatwa. HABARI SOS Médias Burundi
Muili wake ulikuwa ndani ya mfuko wakati ulipogunduliwa na watoto waliokuwa wakitafuta kuuni za kupikia.
” Tuliona mfuko ambao ndani yake kulikuwa kitu. Tuliangalia na tukagundua kuwa ndani kuna maiti. Tulipata woga, tukatoa taarifa kwa wakaazi”, alieleza shahidi mmoja katika wale waliofanya ugunduzi huo wa kutisha.
Kwa mjibu wa mfuasi wa chama cha CNL katika kijiji hicho cha Karungura, marehemu alikuwa miongoni mwa viongozi wa chama hicho cha upinzani eneo hilo. Huenda aliuwawa kutokana na msimamo wake wa kisiasa.
” Mara nyingi alifanyiwa vitisho na Imbonerakure wa kijiji cha Karungura ambao nia yao walitaka ajiunge na chama tawala cha CNDD-FDD lakini bila kufanikiwa. Waliahidi hata kumupa adhabu. Hatukuamini kuwa wangefikia hata kumumalizia maisha”, walieleza wafuasi wa chama hicho.
Imbonerakure wawili walikamatwa, wawili wengine walikimbia. Wanatuhumiwa kuhusika na mauwaji hayo.
Waliokamatwa, wanazuiliwa katika kamishena ya polisi ya Mwumba.
Polisi inahakikisha kuwa uchunguzi unafanyika.
Gilbert Ndacayisaba alitoweka jumatano tarehe 6 aprili jioni wakati akielekea nyumbani kwake kwa mjibu wa watu wa karibu yake. Wanaomba ufanyike uchunguzi huru.
You might also like
Burundi: “Miaka mitano ya ahadi, miaka mitano ya ugumu” – Huko Bujumbura, wakazi wa Jiji wachora tathmini ya kufisha juu ya utawala wa Ndayishimiye
SOS Médias Burundi Bujumbura, Juni 19, 2025 Miaka mitano baada ya kuchukua madaraka nchini Burundi, Rais Évariste Ndayishimiye anajikuta akikabiliana na watu waliokatishwa tamaa. Huko Bujumbura – mji mkuu wa
Burundi: Serikali yazindua mashine ya uchaguzi ya 2027 na inatoa wito wa uhamasishaji mkubwa
SOS Médias Burundi Gitega, Aprili 22, 2026 — Rais Évariste Ndayishimiye alitoa wito wa kuhamasishwa kwa umma kwa nguvu kwa ajili ya uchaguzi wa 2027, akisisitiza haja ya mchakato wa
Bubanza: Wapiga kura waliokatishwa tamaa na uchaguzi walichukuliwa kuwa hitimisho lililotangulia
SOS Médias Burundi Bubanza, Mei 14, 2025 – Wakati kipindi cha kusambaza kadi za wapigakura kinakaribia kwisha, hisia kubwa ya kujiuzulu inazidi kuenea katika sehemu ya idadi ya watu wa
